Vitambi kwa viongozi wa mpira sio uanamichezo.

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Itatia shaka na kichefuchefu kumuona kiongozi wa mpira ana tumbo kubwa linaloning'ia. Kiongozi wa hivi anakatisha tamaa na kuwatia uvivu wachezaji. Kiongozi wa hivi anatia mashaka juu ya umakini wake kwenye tasinia ya michezo. Kifupi hafai kuwa kiongozi wa timu wala chama cha michezo, maana anaonekana mzembe kwa kila MTU.

Hatuwezi kusisitiza fitness kwa wachezaji wakati kiongozi ana kitambi cha kufa mtu. Kiongozi kuwa na kitambi kikubwa wakati wachezaji wanakosa malipo yao inawatia Mashaka ya hela zao kuliwa na kiongozi.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Bila picha huu Uzi ni wakimichongo na mwandishi wake niwakimichongo!
 
Bora kiongozi wa mpira, vipi kuhusu Afisa wa polisi au mwanajeshi kua na kitambi?
 
Kuna watu wamekua lazy lakini still wamechafuka minyota mabegani na posho yao sio ya kitoto ila ukiwaambia pushups kumi hawaendi
Ivi vyeo huwa hawaangalii fitness ya mtu
 
Acha kabisa mkuu kuna watu wanavitambi lakini wako fit.
Sio kila mwenye ndambi ni goigoi.
Pia wapo wasio na vitambi lakini awapo fit.
 
Achana nao wamekaribia kufa kwa pressure au kisukari au heart attack
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…