Vitendo SACCOS - kukopeshana bila riba



Ninahisi kuwa kuna tofauti na namna ulivyoelezea, mfumo wa "Islamic Finance" nilivyouelewa ni kuwa, tuseme unataka kukopa million kumi kwa ajili ya biashara.

Kwanza itabidi hiyo biashara itazamwe mwenendo wake, unaweza kuleta faida au hapana, upo kihalali na unafata sheria za nchi au hapana, ni biashara ambayo ipo tayari na unaongeza unataka kuongeza mtaji au ni mpya na vigezo vingine ambavyo wataalamu wa biashara watavitazama kiundani, kuna "proper study" au hapana ya hiyo biashara. Ukikidhi vigezo vyote basi "financiers" wanaingia ubia na wewe. Na pesa watakazotoa ni mtaji wao na wako, mtaji wao utakuwa unawaingizia faida kutokana na asilimia ya faida kama taji wao ulivyo, na wewe unaingiza faida kwa mtaji uliopatiwa. Katika faida yako utakuwa unarudisha mtaji uliopewa kidogo kidogo kwa kadiri mlivyokubaliana mpaka urudishe mtaji kama ulivyopewa, bila ya wewe kuongezea hata senti moja ya riba.

Utaona kuwa "financiers" wanapata faida kutokana na mtaji waliowekeza na hakuna riba waliopokea wala kutoa.

Halafu tofauti nyingine na "financiers" wa riba, ni muda wa mkopo unaotakiwa ulipe utapokwisha riba hupanda na kuendelea kupanda. Tofauti na "financiers" bila riba, huwa hakuna riba inayoongezeka.

Wenye ujuzi zaidi wanaweza kuweka sawa zaidi au kusahihisha tulipokosea.

Asante.
 

Underlying Conditions for Success in Islamic Finance

“In the Islamic financial system, money does not earn any return without being legally converted into actual capital in collaboration with effort. The proportionate returns for the investor, who provides part of the actual capital to undertake an investment project, and the bank which, on behalf of the depositors, provides the remainder, depends upon several factors such as the priority of the project in terms of value added or increase in employment, the degree of risk involved, social interests, and the like. We will say more about these issues later.

Source: Collateral in Islamic Finance - IslamicBanker.com
 


Nionavyo ni tofauti sana, kukopa kama mkopo na kuulipia riba upate faida upate hasara pasi na mwenzako kuufanyia kazi yoyote ni tofauti na kukopa kwa kutafuta mtaji na anaekupa mtaji anaingia ubia na wewe na faida na hasara mnagawana.


Ninakusihi isome article hii: Collateral in Islamic Finance - IslamicBanker.com
 
ivi Zainab Tamim kwa nini tusiiweke katika mfumo wa SACCOS?

Najaribu kuwaza tu!


Ni wazo jema sana na mpaka sasa tunahisi itakuwa ni saccos itoayo mikopo bila riba.

Mjadala mpana unahitajika kwa njia sahihi na zisizovunja sheria na kanuni unahitajika ili tufikie huko.

Tunakaribisha maoni, ushauri, maswali ili tufanikiwe.
 
Tatizo Watalaamu wa Masuala Ya Fedha Hawaonekani,,,Labda Ndo Kasumba Yetu Watz Kutotoa Madini Tuliyonayo Kisa Atafaidika Fulani?
Tuacheni Jaman Fikra Hizo,,, Huu Ni Muda Wa Kujenga Taifa Lenye Umoja Na Mshikamano Na Ndio Tutafikia Malengo Makubwa.

Wazee Wa Zamani Walisema UMOJA NI NGUVU NA UTENGANO NI UDHAIFU,,, tukisaidiana wote kwa pamoja itafika muda kila mmoja wetu ana uwezo wa kusurvive,
Ni ushaur tu lakin msichukie!
 
Hapana labda unifafanulie kidogo?

Kuna hii ya zamani, nimeiona:

 
Kuna tofauti mkuu, riba haiangalii hasara, upate hasara au upate faida ni lazima ulipe riba na inachajiwa kila mwaka, na pia lazima ulipe kile ulichokopa.
Mfumo wa Islamic Finance ni tofauti, wao ni kama wanatumia mfumo wa hisa katika biashara kwa muda maalumu mtakaokubaliana kisha baada ya hapo unaachiwa biashara inakuwa yako peke yako. Mfumo huu wa kiislamu hasara ikipatikana wewe uliokopeshwa hutadaiwa kwasababu hiyo ni biashara yenu wote kwa muda maalum. Mnachogawana ni faida ya biashara husika mpaka yule aliyekukopesha atakaporudisha pesa yake na faida kidogo kisha anakuachia biashara inakuwa yako peke yako kama mlivokubaliana. Mfano ni wa kuwapa vijana bodaboda kwa mikataba, huu mfumo ni kama kumkopesha kijana bila riba yeye anapata kitu kwa biashara ile kila siku na wewe unapata na baada ya muda maalumu mliokubaliana kijana anabaki na pikipiki yake. Jee hii ni riba?? Hii si riba bali ni faida ya biashara. Kuna tofauti ndogo kati ya faida na riba, usipokuwa makini utachanganya hivi vitu viwili.
 
Ndio Yale yale
Sio yaleyale mkuu hiyo si kweli. .mfanya biashara hununua bidhaa kwa bei fulani na kuuza kwa bei ya juu kidogo, unataka kusema hiyo ni riba?? Laa, hiyo si riba bali hiyo ni faida ya biashara. Ndivyo mfumo wa islamic financing ufanyavyo kazi. Taasisi inakupatia bidhaa fulani kwa faida fulani ambayo wao wanapata. Ni kama vile wamekuuzia kwa mkopo. Na kama tujuavyo ukinunua kitu kwa mkopo bei inakuwa juu kidogo tofauti na ukinunua kwa cash. Tufahamu kuwa unapokopa kwa riba, ukishindwa kulipa katika muda uliowekwa deni lako linaendelea kuongezeka kila mwezi na kila mwaka, Suala hili kwenye Islamic finance halipo kabisa. Ukifungua uelewa wako utaelewa tofauti hizi japo ni ndogo lkn umuhimu wake ni mkubwa sana katika ulimwengu wa biashara na mikopo. Na usipoamua kuelewa, hutaelewa kwakuwa umeamua iwe hivyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…