[emoji3533]USHOGA UMEINGIA TANZANIA[emoji3480]
[emoji273]Na :Shujaa[emoji2399][emoji2401][emoji3501]
Ni ukweli kwamba Sheria za Tanzania na Katiba ya Tanzania inapinga maswala ya Ushoga na Mapenzi ya watu wa jinsia moja ila ni wazi na dhahiri kivitendo kuwa Viongozi wa Serikali ya Tanzania na Serikali yenyewe wanasapoti vitendo vyote vya Wapenzi wa jinsia moja kutokana na kuruhusu viashiria fulani vinavyoonesha uwepo wa vitendo hivyo
[emoji2389]Serikali yenyewe kuthibitisha Uwepo wa Mapenzi ya watu wa jinsia moja pamoja vitendo vya ushoga kuongezeka zaidi Tanzania
Kuna wakati fulani Serikali ilisema tatizo la mapenzi ya watu wa jinsia moja (ushoga na usagaji), ubakaji na ulawiti ni kubwa nchini Tanzania na kuwataka watu kutoa ushirikiano kwa vyombo vya dola ili hatua za kisheria zichukuliwe.
Na Viongozi wenyewe wa serikali wamethibitisha kuwepo kwa shinikizo kutoka nchi za Magharibi la kutaka jamii ikubali ushoga na ndoa za jinsi moja kama haki za binadamu, nchi 38 kati ya 54 za Afrika zinapinga suala hilo. (
Serikali yasema tatizo la ulawiti na ubakaji ni kubwa Tanzania )
Hii ndio sababu ya Nchi yetu kushindwa kuwawajibisha watu wote wanajihisisha na vitendo hivyo wakihofia kukosa misaada na kushtakiwa katika jumuiya za kimataifa kwa hicho wanachokita haki za binadamu
Kitu pekee wanachoweza kufanya serikali ni kutishia tu watu na kuonekana wanakemea vitendo hivyo bila kuchukuliwa hatua stahiki na ndio sababu ya tatizo hili kushamiri sehemu nyingi za nchi yetu kwa kasi
Ubaya uliopo ni kwamba ikiwa atasimama Rais asiye na hofu ya Mungu, ni rahisi kuruhusu vitendo hivi vichafu kutokana na mianya ya mikataba mibovu ya kisheria waliyoingia serikali yenyewe ya kuruhusu haki za wapenzi wa jinsia moja kama masharti ya mikataba hiyo
[emoji2390] Kuwepo kwa bendera za LGBTQ (Wapenzi wa jinsia moja) katika Hospitali Kubwa za Kidini na Kiserikali Bila Serikali kupigwa Marufuku
Mfano mzuri na wa rahisi, wa kuangalia ni katika hii Hospitali ya yenye hadhi Kimkoa iliyopo singida ,
hospitali ya Mwenye heri Yoseph alamano Makiungu ilikuwa hospitali ya wilaya lakini kwa sasa wameifanya iwe hospitali ya Mkoa ndio inahusika kuruhusu Umoja wa nchi yetu ya Tanzania na Umoja wa wapenzi wa jinsia moja ambapo imepelekea kuwepo kwa bendera yenye rangi za Upinde wa mvua ambayo ni bendera ya huu umoja wa Wapenzi wa jinsia Moja (LGBTQ) ambayo imening'inizwa nje na ndani ya Geti la kuingilia hospitali ikiwa zinapepea pamoja na bendera ya nchi yetu ya Tanzania kama inavyoonekana katika video clip mojawapo iliyosambaa katika mitandao ya kijamii (Angalia video hiyo hapo chini )
Kuonesha Serikali yetu inasapoti hili, pamoja na kuwepo na ushahidi wa video zinazoonesha Hospitali hiyo kupepea bendera ya mashoga na wasagaji pamoja bendera ya nchi yetu, lakini bado hakuna hatua zozote za nchi yetu kupiga marufuku hiyo ya kuzuia bendera hiyo kupepea katika ardhi ya nchi yetu
Inasemekana Ujenzi wa Jengo la Hospitali hiyo ya Makiungu ni jengo lililojengwa na msaada wa wafadhili kutoka nje ya nchi wanaohusika wana kuhamasisha Mapenzi ya watu wa jinsia moja, na hii ndio moja ya masharti waliyopewa ili kupata ufadhili huo
[emoji2391]Kuwepo kwa ripoti nyingi na za wazi za vitendo vya Mapenzi ya watu wa jinsia moja bila kufanyiwa kazi na kutolewa hukumu za adhabu dhidi ya hao wanaofanya vitendo hivyo
Ndani ya Tanzania kumekuwepo na ripoti nyingi za kesi za hawa watu wanaofanya mapenzi ya jinsia moja, ya Kishoga na kiusagaji ambazo H
hakuna hata kesi moja iliyowahi kuhukumiwa sawa sawa na kanuni ya adhabu ya Tanzania kwa mtu anayekutwa anafanya mapenzi ya jinsia moja
Hakuna rekodi yeyote,popote ya mtu yeyote aliyeripotiwa kuhukumiwa adhabu kutokana na vitendo hivi vya mapenzi ya jinsia moja, pamoja na kuongezeka kwa kasi watu wanaofanya vitendo hivi
Mfano hapa majuzi,mwezi 2, 2023 kumekuwepo na kusambaa kwa video ya Askari mmoja wa Zanzibar ambaye anaonekana kushiriki hivi vitendo vya ushoga, ambapo inaelezwa kuwa bado jeshi la polisi zanzibar linaendelea na uchunguzi kadhaa kama kufanya vipimo ili kubaini ikiwa kweli anajihusisha na vitendo hivyo...
Ila tatizo lililopo sio kwamba taarifa za kesi za namna hii hazipo mahakamani ila zinaishia juu kwa juu na hautaona hatua zozote za kinidhamu au kisheria zikichukuliwa na ndio maana tuna ujasiri wa kusema Serikali inaruhusu vitendo hivi kwa kushindwa kuwawajibisha ipasavyo wahusika wa vitendo hivi kwa hofu ya kuonekana watavunja mikataba yao ya haki za binadamu walizo saini
Hivyo kama wananchi ni wajibu wetu kupaza sauti kukemea uchafu na vitendo hivi kwa wazi na kuitaka serikali kuweka mkazo katika kusimamia sheria zake wakishirikiana na Polisi wetu na kuhakikisha mahakama zetu zinatoa adhabu stahiki ili kuwafanya wengine waogope kuhalalisha na kuleta vitendo viovu kama hivi.Na tumtake Rais wetu atoe msimamo wa wazi kama alivyofanya Rais wa Kenya,William Ruto na kuitangazia dunia kuwa uchafu huu na vitendo hivi viovu haviwezi kuingia katika nchi yetu hata kama tutakosa misaada bado Yupo Mungu atatupa misaada au tutatumia Rasilimali zote tulizo nazo....
[emoji273]Na:Shujaaa[emoji2399][emoji2401][emoji3501]
0712054498
stmwaisembac@gmail.com