Vitu ambavyo Mwanaume au Mwanamke mwenye akili timamu kamwe hawezi kufanya

Vitu ambavyo Mwanaume au Mwanamke mwenye akili timamu kamwe hawezi kufanya

Ngano ina shida gani ?
Kwa kukusaidia kiafya ni bora ukaepuka matumizi ya ngano maana ndiyo chanzo cha magonjwa mengi mtambuka yasiyoambukiza yanayotukabili wengi wetu hivi sasa.

Hivyo badala ya kubugia ngano nyingi kisha ukaanza kulalamika uzito uliopotiliza, kiungulia, vidonda vya tumbo, sumu kuzidi mwilini n.k bora ujielekeze kula vifuatavyo;

1. Mayai ni mazuri kwa afya ya ubongo wako.

2. Maji ni mazuri kwa ajili ya afya ya figo zako.

3. Kabeji ni nzuri kwa afya ya Maini yako.

4. Matango ni mazuri kwa afya ya Ngozi yako.

5. Machungwa ni mazuri kwa afya ya utumbo mpana.

6. Karoti ni nzuri kwa afya ya Macho yako.

7. Tangawizi ni nzuri kwa afya ya mapafu yako.

8. Parachichi ni zuri kwa afya ya Moyo wako.

9. Nyama ni muhimu kwa maendeleo ya seli, enzymes na homoni mwilini.

10. Pilipili nyekundu ni nzuri kwa afya ya mapafu.

11. Maharage ya kijani ni mazuri kwa afya ya mifupa.

12. Mazoezi ni mazuri kwa afya ya mwili mzima.

13. Kusoma ni jambo zuri la kiafya kwa ubongo wako.
 
Nimesoma Zaidi ya Mara sita Nikagundua Umetaja AI generated Men and Women...

Maana hao wote ni watu wa kufikirika na sio wa kweli hata kidgo...

Tatizo langu lipo kwenye 4,7,8 ,34 na 37...

Mimi na utu uzma wangu sijawahi kujua kuna vyakula vya kuvuta vinavyotoka viwandani

Ngono zembe na ngono zisizo na malengo tofauti yale ni nini? Na saba na nane ina tofauti gani..?

34.....Unajua Kazi ya Sidiria [emoji28][emoji28]

37. umesemaasichunguze simu ya mumewake halafu tena asimuache mumew atumie WhatsapGb sasa hapo mbona mtihani atajuaje kama anatumia Mods whatsapp bila kugusa simu...

Anhaaa kumbe hii Ni forum ya Jokes [emoji28][emoji28][emoji28]
Bhasi sawa

Maswali yako mengi hayana mantiki ila ntakujibu;

1. Umesema kwa umri wako ulionao leo hii mtu akisema neno "UVUTAJI" katika masuala yahusuyo afya ya mwili uelewi anamaanisha nini hili pia unataka nikujibu[emoji848]!!?

2. Ngono zembe na zisizo na malengo au maana, ni zile ngono holela zisizojali unafanya ngono kwa malengo yapi ilimradi mihemko, sifa za kijinga na hujali kuhusu matokeo, na inapotokea matatizo unaanza majuto.

Kuhusu ngono bila kinga ni aina mojawapo ya ngono zembe lakini hapa mtu anaweza kuwa na utashi na dhamira ila akaacha kutumia kinga kwa sababu mbalimbali ikiwemo za kisaikolojia, influence au kuzidiwa maarifa na hisia zake, nimeiweka isimame kama point kwa ajili ya msisitizo.

3. Unaulizia kazi ya sidiria..!? Kwa jinsi unavyojieleza wewe ni mwanaume (samahani kama nitakuwa nimekosea)..kiufupi uwezi jua kiundani mambo yote ya jinsia isiyo yako ndiyo maana unauliza swali jepesi la namna hii. Nikujibu tu kuwa walengwa ambao ni wanawake endapo ningekuwa nimekosea wangekuwa wa kwanza kukosoa na siyo wewe.

4. Swali lako la mwisho pia halina maana kabisa ya kulijibu yaani mtu ana mwenza wake na asiwe anamwona au kuchat naye WhatsApp? Vilevile haikatazwi hata kubofya au kutumia simu ya mwenzi wako "kwa ruhusa yake" kuchat au kuwasiliana.

kuhusu kugusa simu kunakomaanishwa hapa kwa wenza ni ile tabia ya kumfuatilia mwenzio kisirisiri kwa kila anachokifanya kwenye simu yake especially mawasiliano yake na watu wengine.
 
Haya Ndo Madhara Ya Kuvutia Bangi Chooni Bangi Inachanganyikana Na Kinyesi Ni Lazima Utubu Usijifiche.Ungesema Jingine Lakn Sio La Kuacha Kula Vitu Vya Ngano Na Sukari,Kwa Hyo Watu Tusile Chapati Kwa Chai
Katika miaka ya 90s huko vyakula kama vile mikate endapo ingeachwa kwa walahu siku moja pasipo kutumika kesho yake ungeikuta tiyari ime-grow moulds (imeharibika).

Lakini mikate ya ki-leo inadumu mno pasipo kuharibika au kutengeneza ule utando mweusi haraka na hii yote ni kwa sababu ya Calcium propionate.

Calcium propionate huzuia utando ule mweusi (moulds) kukua na hivyo hupelekea tatizo la gesi tumboni (gastritis).

Watu wenye addiction na ulaji wa mikate mara nyingi ni wenye ku-complain kuhusiana na matatizo ya kiungulia lakini uishia kutatua tatizo lao kirahisi kila mara na anti-acids wakifikiria wanakomesha tatizo.

Ukiambiwa unywe chai (yenye madhara kidogo au isiyo kabisa na nikotini na sukari ya viwandani) pamoja na mihogo ya kuchemsha, viazi vitamu, magimbi, maboga, mahindi ya kuchemsha, karanga za kuchemsha, makande, n.k unaona ni u-primitive na pia tunakuonea wivu unavyofaidi maisha.

Na kwa sababu maisha ni yako na ikiwa kigezo ni sisi sote tutakufa basi endelea na mwendo wa kujipiga plastering tumboni mwako kwa kula hiyo GYPSUM ndani ya hiyo mikate yako, na usije sema ukuambiwa.

FB_IMG_17008120773817891.jpg
 
Asante Mungu bangi sijaona [emoji848][emoji848]au sijasoma vzr wakuu
[emoji23] Naomba nitoe angalizo: Tafadhali angalia usivute sana bangi na kisha ubugie mipombe. Bangi huzuia mtu kutapika pindi kilevi kinapomzidia mwilini. Badala yake atazidi kulewa mpaka pale sumu ya pombe itakapokuwa hatari na isiyomithilika tena mwilini. Kifuatacho utakufa kwa haraka kama kuku mwenye mdondo.[emoji124][emoji124][emoji124]
 
[emoji23] Naomba nitoe angalizo: Tafadhali angalia usivute sana bangi na kisha ubugie mipombe. Bangi huzuia mtu kutapika pindi kilevi kinapomzidia mwilini. Badala yake atazidi kulewa mpaka pale sumu ya pombe itakapokuwa hatari na isiyomithilika tena mwilini. Kifuatacho utakufa kwa haraka kama kuku mwenye mdondo.[emoji124][emoji124][emoji124]
NB: situmii kilevi chochote, ila heshimu bangi nasema heshimu bangi narudia heshimu bangi nasisitiza heshimu bangi nakazia heshimu bangi
 
Eti kuwa na mtoto mmoja kama kifaru[emoji1787][emoji1787]
[emoji23] Sasa kwanini ubanie watoto wengine kuliona jua ikiwa wewe mwenyewe kwenu mlizaliwa kumi na mbili, na bado sehemu kubwa ya central na west Tanga-NYIKA iko tupu ni vichaka na mibuyu na hakuna watu wa kuishi huko[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Vitu ambavyo kamwe MWANAUME mwenye akili timamu hawezi kufanya.

1. Kunywa pombe.

2. Kutumia sukari.

3. Kutumia bidhaa zinazotokana na ngano.

4. Kula soseji, uvutaji na kula vyakula vya viwandani.

5. Kuchangisha mahari kupitia makundi ya WhatsApp.

6. Kuvuta kile kijiti cha Kansa a.k.a sigara.

7. Kufanya ngono zembe na ngono zisizo na malengo.

8. Kufanya ngono bila kinga. Dunia imeoza utaliwa na wadudu.

9. Kutumia WhatsApp GB.

10. Kuwa na miito ya nyimbo kwenye simu.

11. Kununua vyakula supermarket.

12. Kuingia jikoni. Labda itokee jiko lishike moto.

13. Kucheza kamari.

14. Kutoa CJs na Kupokea BJs. STD, zitakuhusu.

15. Kuvaa chupi na vipensi vifupi.

16. Kujichua/punyeto.

17. Kumwita mkeo sijui swiry , sweetie, my better half, Hun, the love of my life etc. Muite mkeo kwa majina yake; Nyangige, Rhoda, Mwanahawa, Mariam, Pendo, Bhoke, Manka n.k

18. Ku-date na Mwanamke mlevi.

19. Kulala na mke wa mtu.

20. Kuzaa watoto wawili au mmoja kama vile kifaru. Mwanaume kidume lazima uwe na watoto walahu sita.

21. Kumkumbatia mama mkwe.

22. Kulala ukweni. Walichokupatia ni idhini ya kulala na binti yao na siyo kujamba ndani ya nyumba yao.

23. Utamaduni wa kutojisomea.

24.Utamaduni wa kurudi nyumbani baada ya saa 3 za usiku.

Vitu ambavyo Mwanamke mwenye akili zake timamu kamwe hawezi kufanya;

1. Kunywa pombe.

2. Kujichora tattoo mwilini. Graffiti ni kwa ajili ya daladala za huko Nairobi, Accra na Lagos na si kwa ajili ya kuchora mwilini.

3. Kumwita mwanaume amefulia au masikini. Mwanaume huwa hafulii. Mwanaume daima upambana na uendelea kujitafuta mpaka makamo ya miaka 80.

4. Kununua vyakula supermarket.

5. Kumpikia mumeo vyakula vinavyotokana na ngano.

6. Ku-date zaidi ya mwanaume mmoja kwa wakati mmoja.

7. Kuzaa watoto na baba zaidi ya mmoja.

8. Kulala na watu unaofanya nao kazi iwe ni bosi au mfanyakazi mwenzako.

9. Kulala na watoto wa kiume wenye rika la wanao. Mwanamke anatakiwa ku-date mwanaume anayemzidi umri tu si vinginevyo.

10. Kufanya mapenzi bila kinga. Dunia imeoza.Na soko la mapenzi linanuka.

11. Kutoa BJs au kupokea CJs. STIs na HPV zipo kweli.

12. Kuendekeza au kufikiria kufanya uovu wa kipumbavu wa threesomes.

13. Kuangalia porn.

14. Kutumia dildos.

15. Kumruhusu Mwanaume wako kuchangisha watu mahari kupitia WhatsApp.

16. Kuruhusu mbegu zako za uzazi kurutubishwa na mbegu za mwanaume dhaifu.

17. Kucheza kamari.

18. Ku-date na mume wa mtu.

19. Ku-date na wanaume wanene au wenye addiction na kula.

20. Utamaduni wa kutojisomea.

21. Kuwa mropokaji au mwongeaji kupita maelezo (kama cherehani). Mwanamke ufundwa.

22. Kwenda nyumbani na nguo za ndani chafu au zilizo loa baada ya kukesha huko ulikokuwa usiku mzima. Mwanamke unapaswa kujiheshimu.

23. Kujikwatua na make up kulikopitiliza.

24. Kutumia vifaa vya kisasa vya uzazi wa mpango. Njia bora zaidi ya uzazi wa mpango ubakia kuwa ile ifundishwayo katika dini zetu.

25.Kutumia GB WhatsApp.

26. Kufanya vitendo vyenye ashirio la dharau kwa mumewe iwe ni hadharani au faraghani.

27. Kumruhusu mwanamume wako kupika au kufua.

28. kuvalia G strings and thongs. Mwanamke anapaswa kuheshimu na kuujali uanamke wake.

29. Kuwa na watoto wawili au watatu bila matatizo yeyote yale ya kiafya. Mwanamke mwenye utimamu anapaswa walahu kuwa na watoto sita.Kisingizio cha uchumi si kigezo mjarabu cha kupanga uzazi. Watoto wawili waachie njiwa na mtoto mmoja ni kwa ajili ya kifaru. Hivyo kamwe kama binadamu usishindane na hao wanyama na ndege.

30. Kumwita mumeo husband ,sweetie , swiry, my hubby, bae or Daddy. Muite kwa majina yake; Mburumatare, Sorongai, Nyang'ombe, Magagula, Muochi,n.k

31.Uvutaji wa aina yeyote ile au matumizi ya shisha nakuzalisha moshi mkubwa kama lori lililochoka la mwaka 1910.

32. Ku-date na mwanaume mwanasiasa na kutegemea awe mwaminifu.

33. Kuomba nauli ili ukaonane na mwanaume wako. Kama una nauli, tembea, kimbia au kaa katika jiko la mama yako na ujifunze namna ya kuosha vyombo.

34. Kutumia sidiria (push up bras) kubusti maziwa yaliyolala. Wanaume siku zote uheshimu wanawake wenye kuonyesha hali ya umama (motherhood). Wanawake wenye majeshi yaliyolala uvutia kwa kuwa wameleta uhai duniani. Ni wavulana pekee ndiyo wenye matamanio na chuchu sindano.

35. Kuonesha uchi wako kwa kutembea bila kufuli au kuvalia kanga tupu (going commando) au kuonesha watu sehemu ya juu ya maziwa yako (Exposing your cleavage). Mwanamke ni kujiheshimu. Heshimu uanamke wako.

36. Kula ovyo mitaani.

37. Kuchunguza simu ya mumeo. Hiyo kwa pamoja ni dhambi na uhalifu.

[emoji23]Jamani kwa wale wenye don'ts zingine, kwa kuzingatia jinsia, tamaduni zetu na maswala ya kiafya wasiache kuongezea[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
38. Kuwa mwanachama wa CCM
 
Kuna watu maisha mnsaafanya magumu sana
Ukiyafanya sasa kuwa maraisi ikifika 60s. Karibu tukuhudumie, kwa maana mavidonge na sindano tunazo za kushesha ni wewe tu na kile ulichotuchumia ujanani mwako, njoo tubadilishane, utupatie pesa siye tukulishe misumu.
 
Undava King ehhh,vipi kuhusu utelezi wa wale madada wa kusaidia kazi home? Sema tu kina maza house siku hizi wanakuletea weusi tiiii kama wa Sudani aise. Hawachagui siku hizi. Vipi! Ni halali tuendelee?
Ogopa sana kuonekana "Mume wa Ovyo" mbele ya mkeo na jamii[emoji24] na kisha wanawake kukunyooshea vidole upitapo mitaani.."ndiyo huyo yule mbaba aliyempatia mimba mdada wake wa kazi[emoji23] afu hata alijiheshimu na umri huo jamani!?[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Heeh watoto sita na huu uchumi,

Nyanya za.mia tano unapewa nyanya NNE yaani ile 1,2,3,4 [emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
We unazungumzia kipato, wakati wapo watu wanamiliki matrilioni na wana vitoto viwili kama njiwa, kiufupi kuzaa ni uamuzi wa mtu binafsi kuliko kigezo cha uwezo kwa maana hata hao masikini wapo wenye watoto lukuki na haijalishi anawalea vipi wanae mwisho wa siku mwenye nacho anacho tu.

We zaa mwana wane yamemshinda Rihanna na Vanessa pamoja na ulimbwende wao wameamua kuachia vitu kwa mpigo itakuwa wewe, watoto ni zawadi ya pekee ya kukufariji uzeeni kamwe usiichezee nafasi hiyo.
 
Back
Top Bottom