Bavaria
JF-Expert Member
- Jun 14, 2011
- 53,092
- 53,496
​Kwa hiyo 18 ukacheza nazo mwenyewe! Hongera zako Mkuu.
Asante, nyingine nilirudisha home
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
​Kwa hiyo 18 ukacheza nazo mwenyewe! Hongera zako Mkuu.
Asante, nyingine nilirudisha home
ha ha haaaaa, hata mi ningekucheka swahiba
Besti upo?!
Nilikuwa naogopa mafuta yanayochemka na ukiweka maji. yanavyoruka
Hahahahaha nipo bhanaaaa, naona unasubiri kwa hamu kuu kusoma uborongaji wangu lol!!!
kabla ya kuwa mtaalamu jikoni lazima uboronge kwanza tena vingine hata haviliki ni vya kumwaga tu. Hongera kwa kumshawishi sister wako ajiunge hapa.[/quote BAK nawewe funguka basi uliburunga nini na wewe? Maana na wewe mtaalam wa mapishi sihaba, lazima utakuwa umepitia majaribu mengi
Mie nilikuwa sitaki kuwekewa ugali wa kuvaa koti. Hivyo nikaomba nionyeshwe namna ya kusonga. Basi nikitoka shule naingia jikoni nakorofisha ugali wangu napasha moto mboga iliyopo na kujichana kwa raha zangu. Wazazi wapo wanawajibika, sikutaka dada msaidizi anisaidie nilijiona mtaalamu. Siku moja mama akawepo home akasema nipike ugali mkubwa naye anataka kula alikuwa ananisubiri tule wote ila atakuja kuniangalia wakati nasonga.
Basi baada ya maji kuchemka nikamuita aje kuangalia. Nikakorofisha na kudai ugali tayari, mama akasema haujaiva huo basi ndio akaingia mwenyewe kufanya vitu vyake. Siku hiyo ndiyo nilijua rasmi namna ya kusonga ugali ulioiva. Nikamwamba mama basi siku zote hizi nilikuwa nakula ugali mbichi akaniambia kama usongaji wako ni huo basi ulikuwa unakula ugali mbichi. Zamani chuzi la BAK, acha!!! nyanya kule kitunguu kule hahahahaa lol!! vinaelea kiajabu ajabu hahahahahaha lol!!! lakini siku hizi mambo safi chuzi la BAK 🙂🙂🙂la uhakika nikiweka na nusu kilo ya ugali ulioiva 🙂🙂 mambo bam bam najichana kwa raha zangu.
Hahahahaha u made my day......u r so funny
Hahhahah lkn unaonaga aibu inaonekana...
Mrs Kharusy siku yako ya kwanza kupika mikate ya maji ilikuaje? Upishi ulinipa shida uleHahhahah lkn unaonaga aibu inaonekana...
Angel Nylon siku ya kwanza kupika ugali nlimkuta mama anapika nkamwambia leo niachie mie anakambia hutaweza nkwamwambia acha tu nakumbuka niko form 2 kipindi hiko loh nkaachiwa nlijuta kumbe upishi wa ugali unataka nguvu basi nkawa nasonga naona siwezi tu ugali mwingi kama nini maana twala watu tele home mwishowe nkashindwa nkamwambia malizia ila alinipa moyo nimejitahidi.....tangu siku hiyo sikusonga tena ugali second time nasonga ugali nimeshaolewa ila hata sio mzuri kiivo hadi leo msongaji hubby wa ugali unakuajee mtamu
Hahahaha zamanie nkikaanga samaki namieka alafu nakimbia alafi narudi tena au namrusha tu hii hatar zaidi....
Siku namkaanga pweza anaruka sana ukifanya masihara lazma uungue nlihairi nkaamua kula wa kuchemsha....
Ha ha haaaa, hio ya samaki na mie nlikua namrusha tu. Na kumbe ukimrusha na mafuta ndo Yana splash sana. Basi mama alikua ananionesha namna ya kumweka kwenye kikaango wallah nlikua namwona starring mana unaona kama vidole vinaingia kwenye mafuta ya moto
BAK katika upishi rahisi ni pilau kama la kuku ambae si mgumu kuwiva within 1 hour tayar kwa kuliwa.. . Yaani nikiwa na haraka zangu na lazma nipike basi upishi rahisi niunao ni pilauVyakula ambavyo sitaki kujifunza kupika ni chapati, pilau na vyote vya kukanda unga. Process yake ni ndefu sana ila navipenda sana kuvila lol!!!! Kisa cha kusukuma chapati 20 shapeless kama za Mkuu Bulldog lol! . Ndizi za kupika poa ila zinaniudhi kumenya. Mikate ya maji kama kawa. Mie dingi haoni noma kuingia jikoni kutengeneza kile akitamanicho kula nami sioni noma yoyote kwenye hii idara. Like father like son.
Du!. Acha niende kununua Nazi nikaiandaa vema na mchele nusu . Bwabwa likaiva haswa nikaliacha jikoni vizuri ili nipumzike kidogo kwa badae kui enjoy wa Nazi. Ajaja jamaa mmoja huwa tunamwita kaka pindi hicho anaishi home katoka huko na njaa mbaya kafikia jikoni acha aji servie akaukomba wote hadi kukokoa ukoko. Naamka naenda jikoni nakuta sufuria empty kuuliza naambiwa jamaa kala du iliniuma sana mpaka wa Leo rafiki zangu wakiniona wanacheka sana huku wakisema WA NAZI wakirefer msosi wangu ulioliwa . Du!.
shangazi yangu toka bara huko, mjomba alitoka pwani na nazi akafika pale na kipeto cha mchele na nazi kadhaa akatua mzigo kwasababu ya kiu akasema tutaongea baadaye ngoja nikapate kwanza komoni/pombe ila alimwambia shangazi kuwa nimekuletea mchele na nazi viko humo. alipoondoka tu shangazi kafungua kipeto alichoonyeshwa kuletewa nazi, akachukua mchele na kuchambua na kuupika ili kumfanyia saprise mjomba namna anavyojua kupika kwa nazi akapasua na kuyaweka yale maji ya madafu. jioni mjomba kurudi analetewa ubwabwa na shangazi anamwambia nimeweka na ile nazi. kula mjomba kasema mbona kama hamna iyo nazi?akasema nimeweka, kauliza makokwa yako wapi? akasema nimeshatupa nje, kwenda kuyachukua hajakuna nazi wala nini.alijua labda yale maji ndio ya kuungia.ha ha haaaa, inaelekea ushatupa vingi wewe