Vituo vya kujaza CNG kwenye magari vinavyotembea vitasaidia kujaza CNG kwenye magari kwenye mikoa mbalimbali

Vituo vya kujaza CNG kwenye magari vinavyotembea vitasaidia kujaza CNG kwenye magari kwenye mikoa mbalimbali

Meneja Wa Makampuni

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2020
Posts
7,899
Reaction score
10,415
Tahadhari ndugu msomaji andiko hili linaandikwa namimi mwenyewe ili kuwaonyesha kwamba vituo vya CNG vinavyotembea unaweza kuwa uwekezaji wa haraka sana utakao saidia watanzania kunufaika na CNG kwa katika mikoa yetu yote Tanzania.

Vituo vya kujaza gesi asilia iliyoshindiliwa kwenye magari vinavyotembea vitasaidia kuisafirisha gesi mikoa mbalimbali na kuwauzia watu ikiwa ndani ya magari maalumu ambayo yatasambazwa mikoa mbalimbali.

mobile.jpg
images.jpg
Mobile-CNG-Filling-Station-for-Sale.jpg
download.jpg
download.jpg
mobile-CNG-filling-station-1024x593.jpg
cng-filling-station-right-1024x683.jpg
NGV-2-filling-nozzle-1-1024x683.jpg


Gesi asilia iliyoshindiliwa kwa lugha ya kiingereza inaitwa compressed natural gas (CNG). Ni gesi inayotumika kwenye magari. Unaweza kuibadili injini yako ya petrol au dizeli ili iweze kutumia CNG.

Uzuri upo hapa unapoibadirisha gari yako ili itumie CNG unaweza pia ukaendelea kutumia petroli au dizeli endapo kama upo katika maeneo ambayo hayana CNG.

Uwekezaji pia nauona katika eneo hili la vituo vya kujaza CNG vinavyotembea. Na hili linatokana na ugumu uliopo katika kujenga mabomba ya kusambaza gesi asilia kutoka kwenye vituo vilivyopo Dar es Salaam kwenda kwenye vituo vitakavyo jengwa mikoani. Kujenga mabomba ya kusafirisha gesi mpaka mikoani kunahitaji uwekezaji mkubwa wa fedha, muda na nguvu kuliko uwekezaji wa vituo vya kujaza vinavyotembea.

Vituo vinavyotembea vya CNG ni magari maalumu makubwa yenye matanki yaliyobeba gesi iliyoshindiliwa huku yakiwa na pampu tayari na vifaa vyote vya usalama kwaajili ya kujaza gesi kwenye magari katika maneo mbalimbali.

Kwanini twende na miradi ya kuanzisha vituo vya kujaza gesi asilia iliyoshindiliwa kwenye magari vinavyotembea.

1. Gharama za kuendesha miradi zitakua ni ndogo sana kuliko kujenga mabomba ya kuifikisha gesi asilia kwenye maeneo hayo.

2. Gesi asilia iliyoshindiliwa itaweza kuwafikia wateja wenye magari ambao wako mbali ni kituo cha ubungo cha kujaza gesi ambacho hakitembei.

3. Itaokoa fedha nyingi kwasababu badala ya kujenga vituo vya kujaza gesi asilia kila mahali tutakua na vituo vichache tu ambavyo vitatumika kujaza gesi kwenye vituo vya gesi vinavyotembea ambavyo baada ya kujazwa gesi vitasambaza gesi mahali mbalimbali katika taifa letu.

Hivyo vituo hivyo ndivyo vitakavyotumika kujaza gesi kwenye magari mbalimbali katika maeneo ambayo hayana vituo ambavyo havitembei.

Mengineyo:
Karibu ujipatie gesi janja ya kupikia kutoka M-Gas.

M-Gas tunakupatia jiko la plate mbili kwa elfu 30 tu na mtungi uliojaa gesi wenye mita janja au smart mita.

Smart mita inakuwezesha kujinunulia gesi ya kuanzia kiasi cha Sh. 1000 tu
.
Unasubiri nini kuwahi ofa hii.
Kujiandikisha piga namba:
0747744895
Kumbuka kujiandikisha ni bure kabisa.

Kwa maelezo zaidi kuhusu teknolojia ya M-Gas, soma
Soma hapa,

Nakukumbusha tena nyumba yako itakua salama endapo kama mtungi wa gesi ya kupikia (LPG) utahifadhiwa mahali penye hewa ya kutosha nje ya nyumba yako, na kupitisha mpira wa gesi kupitia ukutani au dirishani mpaka kwenye jiko lako jikoni.

Pika salama lala salama kwa amani bila hofu.

Lakini pia kwa uhitaji wa kuandikiwa propozo za kuanzisha miradi ya vituo vya mafuta na kudizani ramani za vituo vya mafuta vidogo kwa vikubwa karibuni pia.

Kwa mawasiliano:
Call/WhatsApp 0687746471/0612607426
 
Sound tu hizo, bongolala ni business as usual, ukizingatia walamba asali wamerudi ulingoni.......waulize kama watakujibu ni lini usafiri wa SGR utaanza Dar-Moro.
 
Sound tu hizo, bongolala ni business as usual, ukizingatia walamba asali wamerudi ulingoni.......waulize kama watakujibu ni lini usafiri wa SGR utaanza Dar-Moro.
Sio sound boss, huo ndio ukweli uliopo, CNG ni seriously issue.
 
Inakaribia miaka 20 kituo cha kujaza kipo kimoja tu pale ubungo, hapa kati mchina ndo kaweka pale Tazara, hii inakupa picha gani.
Picha inayotolewa hapo ni watanzania wanatakiwa kuwekeza wenyewe kwenye CNG na sio kutegemea serikali wa wachina.
 
Lazima uwe na network ya refill stations za kutosha, siyo kutegemea ubungo pekee......hiyo itakuwa tafrani maana msururu wa magari binafsi tu kujaza pale ubungo huwa ni mkubwa sana.
Basi rudia kusoma nilicho andika boss ili upate kuelewa nimezungumzia nini
 
Back
Top Bottom