VoA watolea ufafanuzi taarifa ya Masharti ya Mkopo wa Korea Kusini kwa Tanzania

VoA watolea ufafanuzi taarifa ya Masharti ya Mkopo wa Korea Kusini kwa Tanzania

WATANZANIA TUSIPOTOSHWE KUHUSU HATI ZA MAKUBALIANO KATI YA TANZANIA NA KOREA KUSINI

Na Amosi Richard

Hivi karibuni baada ya Mhe.Rais.Dkt. Samia Suluhu Hassan Pamoja na Ujumbe wake kuwasili nchini Korea Kusini kwa ajili ya Ziara Rasmi na ya Kikazi na kusaini hati za makubaliano kati ya Tanzania na Korea zitakazoiwezesha Tanzania Kupata Mkopo wenye Masharti nafuu wa shilingi trilioni 6.8 kumetokea wapotoshaji kuanza kusema mambo ya uongo wakitaja kuwepo masharti yanayohusu kuuzwa kwa Madini na Bahari.
Naomba kufahamu hiyo riba ya asilimia 0.01 ni kwa kipindi chote cha miaka arobaini au itakuwa miaka 65?
Tukiangalia na inflation inaweza kuwa riba ndogo kweli
 
anasikika Msemaji wa Serikali akisema hati za makubaliano zinajumuisha ushirikiano katika uchumi wa bluu,
Uchumi wa BLUU maana yake ni Zanzibar.
Je, Zenji itahusika pia katika kulipa huo mkopo?
 
Gas ya Mtwara tuliambiwa ni yetu, Magufuli akasema HATUNA gas kule watu waliishalipwa pesa na waliuza kila kitu.
Hata hili ni muda tu, siku moja atakuja mwenye ujasiri na atatuambia ukweli.
 
Matinyi amesema kuwa Mkopo huo utaanza kulipwa baada ya miaka 25 na utalipwa kwa kipindi Cha Miaka 40.
Habari zenu zinazidi kutuchanganya, Kitila Mkumbo kasema mkopo utaanza kulipwa 2026 wewe unasema utaanza kulipwa baada ya miaka 25 na utaisha ndani ya miaka 40, kipi ni kipi sasa?
 
Sijui tumelaaniwa na nani..... Tumekuwa na viongozi bogus wanao sahau kuwa wote tutakufa.... Mbaya zaidi tuta acha vizazi vyetu vikiendelea kuteseka kwa utumwa....

Kwanini usiwe wewe kiongozi?
 
I am very skeptical about the terms and conditions of this loans.
 
Majizi yana umoja mno
Sema wewe ni mpuuzi mmoja..
Ile Gang ya mwendazake hakika imekuathiri sana.
Ila ni aibu kubwa kuendelea kukopa..as if hatuna wataaluma waliobobea...

Ni upumbavu mkubwa.
The Way We Behave At This Era.
 
Aidha katika taarifa hiyo, anasikika Msemaji wa Serikali akisema hati za makubaliano zinajumuisha ushirikiano katika uchumi wa bluu, ikiwemo masuala ya Uvuvi na utafiti katika masuala ya madini ya kimkakati yakiwemo lithium na grafti. Makubaliano hayo pia yanatarajiwa kujumuisha ujenzi wa bandari ya Bagamoyo, mradibutakaogharimu Dola za Kimarekani milioni 156.5 ikiwa ni Moja ya sehemu ya mradi wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania ikishirikiana na Jamhuri ya Korea.
hili ndio fumbo la imani
 
Siku moja baada ya kutoa taarifa inayoeleza masharti ya mkopo ambao Tanzania imeupokea kutoka Korea Kusini hivi karibuni (Soma hapa). Shiriki la Habari la Sauti ya Marekani (VoA) limeibuka na kutafuta ufafanuzi wa kina wa taarifa ya mkopo huo kutoka Serikalini. Habari hiyo inaeleza:


Serikali ya Tanzania imetolea ufafanuzi juu ya Mkopo waliopokea kutoka Korea Kusini ulioambatana na makubaliano ya ushirikiano katika Sekta ya Uvuvi pamoja na madini huku wachumi nchini wakiitaka Serikali kujenga utaratibu wa kutoa taarifa za kitaalamu Kabla ya kuingia kwenye Mikopo. Kueleza manufaa yatakayopatikana kutokana na Mikopo hiyo.

Mwandishi wa VoA anaripoti kuwa, kwa mujibu wa Msemaji wa Serikali Mobhare Matinyi amethibitisha Tanzania kuingia Mkataba na Korea Kusini, utakayoiwezesha Tanzania kupokea kiasi cha Dola za Kimarekani Bilioni 2.5 kwa Kipindi Cha Miaka mitano kuanzia 2024 mpaka 2028. Matinyi amesema kuwa Mkopo huo utaanza kulipwa baada ya miaka 25 na utalipwa kwa kipindi Cha Miaka 40.

Mkopo huo unatarajiwa kuwa wenye riba nafuu ya asilimia 0.01. Katika habari hiyo Msemaji wa Serikali ya Tanzania Mobhare Matinyi amesikika akisema

Mkopo huu utaanza kulipwa baada ya miaka 25 yaani ukifika mwaka wa 26 baada ya kuwa umemaliza kutolewa 2028. Tutapewa Kipindi Cha Miaka 40 kuulipa. Riba ya Mkopo huu ni 0.01%.


Tanzania kushirikiana na Korea kusini kujenga bandari ya uvuvi Bagamoyo
Aidha katika taarifa hiyo, anasikika Msemaji wa Serikali akisema hati za makubaliano zinajumuisha ushirikiano katika uchumi wa bluu, ikiwemo masuala ya Uvuvi na utafiti katika masuala ya madini ya kimkakati yakiwemo lithium na grafti. Makubaliano hayo pia yanatarajiwa kujumuisha ujenzi wa bandari ya Bagamoyo, mradibutakaogharimu Dola za Kimarekani milioni 156.5 ikiwa ni Moja ya sehemu ya mradi wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania ikishirikiana na Jamhuri ya Korea.

Hata hivyo Dkt. Bravious Kahyoza ambaye ni mchambuzi wa masuala ya uchumi amesema ni muhimu serikali kuweka utaratibu wa kufanya uchambuzi yakinifu kabla ya kuingia kwenye mikopo kuonyesha namna ambavyo taifa litakwenda kunufaika na mikopo hiyo.

“Serikali ni muhimu kuwa na utaratibu wa kufanya uchambuzi yakinifu na kuonyesha ni kitu gani kinakwenda kutokea, ni kwamba serikali ifanye uchanganuzi makini wa kuonyesha ni kitu gani tunakwenda kukifanya na kitakwenda kutoa matokeo gani kwa umma.” Amesema Kahyoza.

Matinyi amemalizia kwa kusisitiza mkopo huo ni mkopo nafuu na hauna mashariti yoyote yanayohusisha kutoa sehemu ya bahari na madini.

PIA SOMA
- Prof. Kitila Mkumbo akanusha masharti ya Mkopo wa Korea Kusini. Asema utalipwa kwa miaka 40

- VoA: Tanzania imepokea mkopo kutoka kwa Korea Kusini na kutoa sehemu ya bahari na madini

- Ziara ya Rais Samia Korea Kusini atasaini Mkopo wa Tsh. Trilioni 6.51

- Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi azungumza na waandishi wa habari kufafanua kuhusu Mkopo wa Korea Kusini
 

Attachments

  • IMG_20240605_072933.jpg
    IMG_20240605_072933.jpg
    287.4 KB · Views: 2
Nimeshasema hao wanatakiwa waombe msamaha kwa serikali na kwa Rais wetu. Wasipende chokochoko kwa Taifa letu na kuleta uchonganishi wao hapa.
Umeshasema we kama nani mla mihogo tu nani anayekujua zaidi ya kujipendekeza?!.
 
Sijui tumelaaniwa na nani..... Tumekuwa na viongozi bogus wanao sahau kuwa wote tutakufa.... Mbaya zaidi tuta acha vizazi vyetu vikiendelea kuteseka kwa utumwa....
Wewe umewajengea nini wanao? hujakopa? utakufa na watu wako watakulipia madeni pia. acheni kujifanya mna uchungu sana unafiki wa kiwango cha juu. Hata sisi tumelipa madeni ya wazee wetu waliyokopa miaka ya 60 kama nchi na watakuja kizazi kingine watalipa. Ila watakuta barabara na miundombinu ipo kwa hiyo watazalisha na watalipa.

Tupunguzeni kidogo kujuwa hebu tuambie nchi gani haina madeni. Bwana mkubwa USA ana madeni mpaka halipiki sembuse sisi.
 
Madogo waliosomea Uvuvi wapewe kipaumbele sio wanawekana wekana wenyewe tu km kwenye HIZO Safari zao wanachomekana chomekana tu Q.umalamake ZAO wasengerema, madogo wamesomea Uvuvi wanasota tu mtaani HUKU trillion 6.5 mkazifanyie usenge usenge wa kuchomekana chomekana
100%
 
Mimi ni lazima niwe fair pamoja na kutofautiana na serikali tena kwenye mengi uamuzi wa kuchukuwa mkopo wa $2.5B ni mzuri kwasababu zifuatazo
1. Mkopo wa muda mrefu
2. Riba nafuu
3. Nchi itaingia uchumi wa kati na itakuwa ngumu baadae kupata mikopo hii

Sehemu ambayo nina wasiwasi ni matumizi. Kuchukuwa mkopo na kwenda kununua magari hapo ndipo matatizo ya naanza. Serikali hii matumizi yake sio mazuri kabisa

Lakini kwenye mkopo wenyewe wanafikiri vizuri
 
Mimi ni lazima niwe fair pamoja na kutofautiana na serikali tena kwenye mengi uamuzi wa kuchukuwa mkopo wa $2.5B ni mzuri kwasababu zifuatazo
1. Mkopo wa muda mrefu
2. Riba nafuu
3. Nchi itaingia uchumi wa kati na itakuwa ngumu baadae kupata mikopo hii

Sehemu ambayo nina wasiwasi ni matumizi. Kuchukuwa mkopo na kwenda kununua magari hapo ndipo matatizo ya naanza. Serikali hii matumizi yake sio mazuri kabisa

Lakini kwenye mkopo wenyewe wanafikiri vizuri
Mkopo ni matumizi hata kama riba ni ndogo,hayo matumizi yataongeza gharama nyingine ambazo serikali hii hii itakopa Tena kwa hayo matumizi
 
Bora hata wange'boost kwa kutoa mikopo yenye riba nafuu, ku'subsidize kikokotoo, mishahara na kandarasi za ndani ili hela ishuke kwa wananchi, ku'stimulate uchumi
Magari is mad NONSENSE
 
Back
Top Bottom