Vodacom Premier League 'VPL' Mwadui FC yaituliza Simba SC kwa kuichapa kwa goli 1 - 0

Hakuna timu isiyofungwa duniani. Tena mara nyingi timu kubwa hufungwa na timu vibonde. Kwa Simba hii ni "wake up call" kuwa ligi ya mwaka huu sio nyepesi. Kama wanataka ubingwa wajipange hasa.

Lakini goli la jana la Mwadui halinishangazi sana kwani ni aina ya magoli anayofungwa Manula kila mara. Mara nyingi anakuwa na kiherehere cha kusogea hatua kadhaa mbele ya goli pasipo sababu ya msingi. Ndio maana Kaseja atamburuza sana kwenye timu ya taifa mpake aote mvi ndio Manula atakuja kupata nafasi tena ya kucheza timu ya taifa. Huwa najiuliza kocha wa makipa pale Simba bwana Muharami ameshindwa kabisa kumrekebisha Manula kwenye haya mapungufu ya kusogea hatua kadhaa mbele ya goli bila sababbu za msingi? Halafu Ndairagije akimwacha kwenye timu ya taifa mashabiki wanapiga kelele bila kujua mapungufu ya Manula ni nini ukimlinganisha na Kaseja.

Jambo la pili ni timu nzima ya Simba iache kudharau baadhi ya timu. Najaribu kuangalia jinsi Simba ilivyocheza mechi mbili na Azam (ligi na ngao ya jamii) na jinsi ilivyocheza na Kagera Sugar mwanzoni mwa ligi hapo Simba walikuwa bora sana. Halafu naiangalia Simba iliyocheza na Singida United pale Arusha pamoja hii ilivyocheza na Mwadui. Utaona kabisa baada ya Simba kushinda mechi za mwanzo basi wakaridhika. Kuanzia mchezo na Singida na huu wa Mwadui Simba walikuwa wanacheza tayari na matokeo mkononi' Hata Singida wangetulia wangeweza kushinda ile mechi ya Arusha kama walivyofanya wenzao Mwadui jana.

Ni wakati sasa Ausems na benchi zima la ufundi la Simba kufanya "rotation" kwa golikipa kama wanavyofanya kwenye nafasi nyingine ndani ya uwanja ili kuleta ushindani na kuondoa dhana ya mtu kumiliki namba.
 
Kama mwalimu kukosea kupo ila isiondoe maana kuwa Hatuwezi kupoteza mechi
Hatutakiwi kupoteza mechi kizembe hivi, tena na timu inayokimbia relegation kwa kutopanga timu accordingly.

Ule uwanja inatakiwa awe anawapanga madogo wa kibongo waliozoea viwanja hivyo.
 
Hapo kwa kipa naunga mkono hoja. Aussems akimpa nafasi Beno kucheza mechi ya kirafiki anafunika vibaya sana na huwa nawaza next match atapewa kudaka,

unashangaa bado anasugua benchi.
Inahuzunisha sana kipa wa kiwango cha Beno anawekwa benchi na kipa wa kiwango wa Manula, absolutely incredible!
 
Muda waliotumia Wasafi FM 88.9 kuchambua kipigo cha Simba dhidi ya Mwadui na muda waliotumia kuichanachana Yanga dhidi ya Pyramids unasema mengi. Niishie hapo tu.
Kila mtu mtamuona mchaw sas hivi ila ndo hivyo mwadui al kasusu(kitenge)
 
Kikosi changu mechi na Mwadui
1. Beno Kakolanya
2. Haruna Shamte
3. Gadiel Michael
4. Hassan Mlipili
5. Kennedy Juma
6. Hamis Ndemla
7. Dillunga
8. Muzamiru
9. Kagere
10. Ajib
11. Miraji Athuman
Subs
1. Manula
2. Rashid Juma
3. Fragha
Toa Kennedi weka Nyoni ....We Kocha vipi?
 
mechi ya jana kwanza ingawa wengi wanamlaumu Manula lile halikuwa kosa lake kutokana na movement ya mpira ilivyokuwa ni wazi Manula alipaswa asogee kosa la kwanza lilianzia kwa Shamte mara nyingi alikuwa anatokwa kiasi cha kuwafanya mabeki wakati wavutike lakini pia position aliyokuwepo Gadniel Michael haikuwa sahihi alikuwa nyuma ya mshambuliaji alipaswa awe naye ambuguzi ili asiwe huru kupiga kichwa kama alivyofanya.
Kosa jingine walilofanya ni mabadiriko ya mpigo jana Mzamiru hakuwa katika kiwango chake alipaswa atolewe mapema pia Dilunga na Miraji walioingia wote ni wazuri kucheza kutokea pembeni kwa hiyo pale kati paliachwa wazi na kuwafanya mwadui kuwa na ulinzi wa ziada.
ila hiyo ni wake up call kwa Simba bado tunayo matumaini ya ubingwa
 
Mimi ninayo matokeo ya kirumba tu, kama unahitaji nikupatie.
Furaha yenu imebaki siku mbili iishe, kama unavyojua jumapili ni kilio kingine.
Kila lakheri Pyramid fc
Kila lakheri Shadeeya
Hahahaaa. Nikwambie kitu Mtani weka akiba ya maneno sababu tunaenda kutoka sare kule. 😎😎😎
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…