Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)


Mi nilishawahama voda toka mwezi wa 11 mwaka jana. Wapuuzi sana.
 
Na kuna tabia ya baadhi ya wahudumu wenu kuswap line na kuanza kuhamisha pesa kwenye mpesa.pesa mnahamishia kwa mawakala hilo lipo na ushahid upoo
 
Habari Mtoboasiri tafadhali tutumie namba ya simu PM kwa msaada zaidi, pole sana
 
Last edited by a moderator:
Habari mkuu xyz123 namba hizi ndizo zinazosaidia katika kuanza na uchunguzi juu ya suala hili.
 
Last edited by a moderator:
Habari Mtoboasiri tafadhali tutumie namba ya simu PM kwa msaada zaidi, pole sana

Lakini mkuu, unaonekana una asili ya ubishi, umeshauriwa kurekebisha matatizo yenu yote kwa ujumla kwa kua humu jf watu tuliotoa malalamiko yetu ni sehemu ndogo tu ya jamii mnayoinyanyasa. Huko nje ya jf kuna watu wengi ni wahanga wa matatizo yenu, sasa unaposema utumiwe namba pm utatatua matatizo ya watu wangapi kati ya wengi walioko nje ya jf?

Tafadhali, acha siasa, wambie wakubwa wako washughulikie mfumo wenu wote ili mtatue tatizo kwa ujumla wala siyo kirejareja kama unavyofanya sasa. Ni mtazamo wangu tu kwa hiyo una hiari ya kuufanyia kazi ama la.
 
Last edited by a moderator:
Habari mkuu xyz123 namba hizi ndizo zinazosaidia katika kuanza na uchunguzi juu ya suala hili.

Sawa, kwa hiyo mnauamini mfumo wenu kwa asilimia 100 ndo maana mnakomalia kushughulikia hizi namba chache badala ya kuchunguza mitambo yenu kwa ujumla?
 
Last edited by a moderator:
Binafsi natumia Voda to 2006 sijawahi kukumbwa na tatizo kama hilo hata siku moja.

Yaelekea wewe ni mmoja wa wadau wa hiyo kampuni ya ovyo, wezi, vibaka na majambazi wasio na utu wala huruma kwa wananchi wa nchi hii.
Msidanganyike; ipo siku makampuni haya yaliyowaweka viongozi wa nchi hii mifukoni kwa vijirushwa rushwa yatakimbizwa na wananchi wenye hasira mara tu ukombozi na uhuru wa kweli utakapowaidia. CCM ni zaidi ya janga.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 

Huyo mdau uliyemjibu hata mimi nimemshangaa, yaani wizi wote unaofanyika yeye hauoni? Maajabu.
 
Binafsi nimeshaacha mtindo wa kuacha salio kwenye laini ya Voda kabisaaa tangu nilipoibiwa salio mfululizo! Kuna siku simu yangu ililala na salio la 7,000/= na asubuhi nikaongeza 4,000/= nikiwa na matumaini ya kununua kifurushi cha 10,000/= na kujibiwa "Huna salio la kutosha" nilipoangalia salio eti lilikuwa 4,4000/=! Nilipojaribu kuwatafuta ili kuwasilisha malalamiko nilielekezwa namba ya kulipia ili niongee nao na hakuna la maana walilonieleza kwa zaidi ya mara kumi; kucheki salio sasa lilisoma alfu tatu na ushee! Shit Vodacom!


Sent from my iPhone using JamiiForums
 

Mkuu nadhani hapa ulitaka kuandika 4,400/= ila ukateleza, tafadhali rekebisha ili hoja iwe na mantiki iliyokusudiwa.
 
Habari mkuu xyz123 namba hizi ndizo zinazosaidia katika kuanza na uchunguzi juu ya suala hili.

Hakuna cha kusaidia wala nini, system yenu ipo corrupt. Haya mambo siyo ya leo wala jana. Haya mambo yana zaidi ya mwaka.

Labda nikuulize kitu, tokea uanze kuomba namba za watu wenye matatizo, naamini umepata walau namba 5 kwa uchache, jee kati ya hizo namba (ukitumia kama sample) ni ngapi kweli zimekutwa na matatizo. Yaliyodaiwa.?

Msipoangalia mtaendelea kupoteza watu wengi sana.
 
Last edited by a moderator:
Mi ndio nisha wachoka mpaka basi wezi kweli.
 
Mkuu nadhani hapa ulitaka kuandika 4,400/= ila ukateleza, tafadhali rekebisha ili hoja iwe na mantiki iliyokusudiwa.

Sawa Mkuu. Ni 4,400/= naona button imeteleza.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Jaman voda kila siku bundle yao wanapunguza, leo nmeunga ile ya week (1999) dakika 30 badala ya 35 na 100MB badala ya 125! Nkimaliza bundle yangu narudi nyumbani tigo!
CC Vodacom Tanzania
 
Last edited by a moderator:
Jaman voda kila siku bundle yao wanapunguza,
leo nmeunga ile ya week (1999) dakika 30
badala ya 35 na 100MB badala ya 125!
Nkimaliza bundle yangu narudi nyumbani tigo!
CC Vodacom Tanzania
 
Habari Platnam, tafadhali tutumie taarifa zifuatazo PM kwa msaada zaidi.
Namba ya mtumaji
Namba ya mpokeaji
Muda ujumbe uliotumwa
Hili tatizo siyo mimi pekeyangu nakumbana nalo,nafikiri mmeshaona watu wengi tu wakiwa na same complain..kwanini msitatue haya matatizo kwa ujumla na kuacha kuulizia individual namba? Nishapiga kwa watoa huduma wenu mara tatu bado hakuna utatuzi..au nyie ni tofauti na tunaozungumza nao?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…