Vodacom Tanzania
Official Account
- Aug 12, 2013
- 324
- 126
- Thread starter
-
- #1,541
Vodacom Tanzania naomba nijue ni akina nani ambao namba zao zimefutwa na still hela ipo maana tuna ndugu ambao hatujui kama wana line ya voda je zile zinazobaki hua zinapelekwa wapi BAK
Mi Binafsi Voda wananifurahisha sana. Kwanza kabisa wametoa fursa ya vijana kujiajiri kwa M pesa.
Lakin Jambo kubwa zaidi la kusikitisha wamewapa matapeli ulaji. Mfano ni Mim Binafsi niliomba uwakala toka mwaka Jana mwezi wa kumi na Moja mpaka leo ni nimeambulia patupu. Baada ya kufatilia kwa ukaribu nikagundua line (Till) yangu. Nilishindwa kushangaa!!! Nikawaeleza kwanin m2 atumie till kwa jina langu na document zangu kwa mwaka mzima. Na mim nimekaa mwaka mzima nyumbani sina Kazi. .Sasa wameniambia nikafanye SWAP Ngoja nione watachukua Muda Gan. Kwa hali hiyo voda Waliangalie kwa jicho la 3.
Habari Gwaje, tunapenda kukufahamisha kuwa tatizo lipo kwa wakala mkuu uliyempatia taarifa zako. Tumekuwa tukishirikiana na mawakala katika hili kuhakikisha wanapatiwa Till zako. Tutumie taarifa zako PM kwa msaada tafadhali.Voda wahuni hata nami hapa moro wameuza line yangu ya uwakala kwa wqtu wengine
Unaweza kuripoti kupitia kurasa zetu za Twitter na Facebook.@Vodacom Tanzani hivi hakuna njia nyingine mbadala tofauti na kupiga simu kama nataka kurudisha pesa nilioituma kimakosa kwa mpesa?
Habari kyumana, hali hii hutokea pale ambapo simu inaendelea kutumia kutumia huduma za intaneti mara tu unapoweka salio. Tafadhali hakikisha umezima huduma za mtandao (Mobile Data) weka salio kisha nunua kifurushi na ufungue mobile data.Ukiweka Salio ukataka kujiunga kifurushi unaambiwa salio halitoshi,ukiangalia Salio unakuta bado linatosha.Unaamua kuchagua kifurushi cha bei ya chini unaweka kifurushi inakubali,,lkn ukiangalia salio unakuta bado lipo ukikaa baada ya muda unakuta limepotea.
Hawa jamaa wanakata kushinda hata lile tozo la mwezi lililolalamikiwa kipindi kile bungeni.Hapa nasubiri kurenew laini yangu ya mtandao mwingine
Habari mkuu, itakuwa vyema tukapeana namba ya simu kwa msaada zaidi, tukifahamu siku/tarehe uliyonunua kifurushi itakuwa vyema.Kwanza habari za kazi kwenu nyote mnao husika?
Pili niende kwa linalo nisibu haijalishi mtanisaidia ama mtapotezea,mhimu kwangu mlitambue. Mnapo anzisha huduma zenye kulenga kumsaidia mteja kweli mlenge ktk hilo,siyo mnaanzisha ktk mfumo huo kumbe mpo ktk mfumo wa ninyi kujiingizia kipato{mauzo} kwa kiwango cha juu. Hapa naomba nigusie mfumo wenu wa cheka na hasa hii cheka bombastick na hasa inayo husu mitandao yote. Nimekuwa mhanga wa hili kwa kipindi kirefu sana. Imani kwamba dk.zote ninazo nunua ninazitumia haipo tena hapa kuna usanii flani unafanyika na mbaya zaidi ni kama umenunua kifurushi cha wiki au mwezi hapo sahau kufika nacho mwisho.Na kwa kuthibitisha hilo nimejaribu kununua kifurushi cha aina hiyo kwa mtandao mwingine na kingine chenye thamani kubwa tena kimoja kwa ajili ya off net & on net na kingine kwa ajili ya on net tu kwa upande wenu bado hivi vya kwenu vimeisha haraka ilihali kile cha mtandao pinzani mpaka leo natumia. Hebu jitathiminini kwa hili.
Lakini pia mna ugonjwa wa mtu kupiga simu kama ana kifurushi na kika isha ndani ya maongezi kama ana salio mstoe taarifa na wakati mwingine hata akipiga simu nyingine na pale salio liishapo tu ndiyo mnatuma taarifa ya kuisha kwa kifurushi. Maana yake nikanunue vocha nyingine. Kama hiyo ndiyo ilikuwa budget yangu ya vocha kwa siku,wiki ama mwezi! Niende nje ya budget si ndiyo? Na kama niko sehemu ambayo upatikanaji wa vocha ni mgumu? Nikae bila mawasiliano ama niwe nasubiri kupigiwa? Au ndiyo kunipeleka ktk huduma ya kunilazimisha nikope kutoka kwenu ili mtengeneze faida mara mbili kwa kupitia vocha nitakayo inunua kulipa na kunikata zaidi kutokana na mkopo wenu?
Hebu tuchukulieni kama wateja wenye kustahil huduma bora na siyo manyanyaso kwamba wamesha ingia wataenda wapi?
Ni hayo tu mnaweza kufanyia kazi ama kupotezea kama ikionekana hayana mashiko kwenu!
na mbona napata shida nikiwa huku Uganda napata network ya MTN lakini siwezi pata hudumma ya vodacom menue nataka kununua salio toka kwene m-pesa yangu na kila nikijaribu 0752-898906 *150*00# inajibu REQUEST NOT COMPLETE" AMA MENUE IMEBADILIKA KWA MTU ALIYE NJE YA NCHI?
sasa kweli mnategemea nifanye nini???????????
i need reliable service
Mko Poa sana kwangu nawasifu pamoja
Mimi siwaelewi hawa voda! Kila nikinunua LUKU kwa njia ya m-pesa wanachelewa sana. Na ukiwauliza wanakuambia kuna tatizo kidogo upande LUKU TANESCO. Na wakati huohuo ukinunua kwa mtandao mwingine unapata muda huohuo. Na wao watakurushia token baada ya masaa 6 au siku inayofuata. Hebu hapa toeni jibu niwaelewe. Maana mkisema kuna tatizo kidogo upande wa TANESCO, hawa airtel ukinunu kwao wanakupa muda huohu. Wao wanatoa wapi?
Habari kyumana, hali hii hutokea pale ambapo simu inaendelea kutumia kutumia huduma za intaneti mara tu unapoweka salio. Tafadhali hakikisha umezima huduma za mtandao (Mobile Data) weka salio kisha nunua kifurushi na ufungue mobile data.
Habari vodacom! Wiki iliyopita niliwasiliana nanyi kuhusu suala la mpawa, nikawapa na no yangu, mkasema mtanipigia simu, lakini hadi leo sijapata mawasiliano yoyote kutoka kwenu ili niweze kujua suala langu limefikia wapi, 0757 980 448. Naomba mnijibu ili niweze kujua km linawezekana au imeshindikana. Ahsante!
Nyie vodacom mbona mnaubaguzi kwa nin nasisi msituletee 3g huku boda kwetu wafanyakaz tupo wengi tunaitaji bhana pia sometimes network yenu inazengua msaada please mrongo border kaisho karagwe
habari, ningependa kujiondoa na huduma NIPASHE habari. Nimejaribu kujiondo kwa njia ya kutuma sms
"ONDOA au STOP" kwenda 15501. Inakuwa failed naomba msaada