Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Vodocom wanaibiwa sana MPESA ila kwa kuogopa kuchafua jina lao wanakaa kimya na kuamua kulipiza kwa kuumiza wateja wao.
Hapo umenunua haiji, ikija ukijaribu kuunga kifurushi watakuambia mtandao unasumbua ili mradi tu pesa yako iliwe (ikiwa hujazima mobile data), badae wadakuambia huna salio la kutosha kujiunga na kifurushi.
Sasa kma kujiunga mtandao unasumbua, huo mtandao wakati pesa yako inaliwa taratibu unatoka wapi?
ndicho kilichonitokea mm jana hadi choz lililenga...kwa kweli niliwamind sana hawa waduanzi...inawezekana wanaset vitu vyao...!!!?
 
Hawa wezi wamekuwa wakiniibia MB zangu mara nyingi tu. Nimehamia SMART.....so far so good!
sasa sijui tutahamahama hadi lini hii mitandao??...na ukihamia mwingine karibisha mteja siku ya 1,2 3 wanakuumiza kama kawa!!
aaaaaaaaaaaaaaaaarggh!!!
 
Hawa wezi wamekuwa wakiniibia MB zangu mara nyingi tu. Nimehamia SMART.....so far so good!


Naafikiana nawe SMART wapo smart labda waingiliwe na politicians.

Nilichojifunza vodacom kuna udokozi dokozi wa kijinga sana siku moja nilikwenda ku renew line yangu pale Morogoro nikaambiwa Tshs 3000, muda huohuo akaja mteja mwingine kwa mhudumu mwingine next kwa yule aliyekuwa ananihudumia, nasikia anaambiwa Tshs 1000, niliondoka hata line sikuchukua na alikuwa ameibandua tayari
 
nisaidien voda wana nifirisi yaani jana nilikopa 900 leo nimelipa1000 deni lao lakini kila nikiweka vocha wanakata nimeweka hadi 4000 zote wanakata nikijaribu kukopa wanasema lipa mkopo wako wa awali kwanza nimechoka jamani na hawa wezi
Habari Pampula jr tafadhali tunaomba namba ya simu PM kwa msaada zaidi.
 
Last edited by a moderator:
Wakuu; nimepigiwa na customer service ya Vodacom (at least ndivyo alivyojitambulisha kwangu baada ya kunipigia kwa namba iliyo-display kwangu +25576670). Kaniambia kuwa ili bundle uliyonunua itumike ni lazima uwe na salio litakalo (kwa maelezo yake) back-up bundle ulilonunua, otherwise hata kama umenunua bundle la mwezi hutalitumia. I stand to be corrected na wahusika.
 
Mkuu hawa jamaa nishawahama mwaka huu, line yangu ya Voda ilikuwa na tatizo la kutopiga simu ila kupokea simu pamoja na kuandika sms na kutumia net ilikuwa poa, nilihangaika na customer care mpaka nikakata tamaa, siku nikaamua kuwaibukia pale mlimani city, nikawaambia tatizo, mwisho wa siku eti wananiambia niformat simu ndo ina tatizo, sasa nikawa najiuliza kama simu ndo tatizo mbona line za mitandao mingine zinafanya kazi vizuri, kuanzia hapo nikawatema, jana tu dada yangu alikuwa analalamika anasalio la kutosha lakini kila akijaribu kuunga kifurushi anaambiwa hana salio la kutosha

Shida ya voda na mitandao mingine pia wanaajiri customer care si kwa vigezo sifa na ujuzi bali kwa mwonekano na hili tatizo haliko mitandao ya simu tuu ni almost kila mahali ni Mara chache mno kukutana na cc mjuzi na mwenye kujua shida ya mteja wake
Kwa ufupi ni kwamba customer care nyingi ni majanga hasa hapa kwetu
 
Habari tzbiz pole sana kwa suala hili na tunaomba kufafanua namna Happy Hour inavyokuwa. Ni kwamba huduma hii inakupa dakika 60 kupiga simu kuanzia muda uliojiunga, hii inaamanisha kuwa ukijiunga saa 2 asubuhi huduma yako itakwisha dakika 60 kutoka saa 2 asubuhi kwa maana ya saa 3. Ukipiga simu saa 2 dk 40 unakuwa umebakiza dakika 20 kufikia mwisho wa kifurushi chako.

Kwahiyo kifurushi ulichojiunga saa 1:30 cha dakika 20 ilikuwa ni sahihi kupokea ujumbe kuwa kifurushi chako kimekwisha dakika 30 baada ya kujiunga.Tunaimani maelezo haya yamefafanua vyema suala hili


haya nilikuwa nje ya mtandao. nimerudi, nimesoma maelezo, na nimekuelewa. Kwa nini msibadili mtindo kuleta thamani ya fedha ya watumiaji wa mtandao wenu? huoni kama huo mtego wa kusema dakika 60 unadangaya watu kwa kuwa hakuna kipengele cha kusema LAZIMA UANZIE MWANZONI MWA HIYO SAA?

Kwanini msiweke hiko kipengele kuokoa watu wanaojiamulia kununua hiyo happy hour bila kuangalia kama wamenunu dakika ngapi ndani ya muda?

Wewe Vodacom tanzania hapo bado haujakwepa lawama ya udanganyifu hata kidogo.... Hiyo katika marketing inaitwa Deceptive Advertising, na ni jinai ya kibiashara hivyo. Badilikeni!
 
vodacom tanzania we are sick and f@$$/@ na service zenu zimejaa dhuluma ....zishatolewa lawama nyingi kuhusu nyinyi na huduma zenu lakini hamjirekebishi.....gadamn
 
Je Wajua?

VODACOM ndiyo Pekee mtandao wa simu Tanzania isiyogawa 3G network Dar es salaam?

Mitandao iliyobaki wote wamegawa kuna sehemu zina 2G, 3G na sehemu zingine huduma za internet hakuna kabisa.

BIG up Voda kwa internet ya uhakika.

Hakuna kizuri kisicho na Kasoro
 
Hiyo mitandao karibu yote ni kama majambazi vile.

Hasa hasa wizi mkubwa unafanyika kwenye vifurushi vya masaa 24, na mitandao inayoongoza kwa wozi wa vifurushi vya masaa 24, ni voda na tigo.

Mara nyingi mimi nimejiunga kwenye kwenye vifurushi vya masaa 24, kwenye mitandao hiyo, lakini cha kushangaza sijui wao saa zao 24 wanazihesabuje?

Ni mara nyongi nimekuwa nikijiunga vifurushi hivyo vya masaa 24, lakini mara nyingi pia, less than 3 hours, nimekuwa nikipokea meseji ya kifurushi chako kimekwisha, hsta kabla sijapiga simu yoyote kwenye kifurushi hicho.

Mimi naona makampuni pekee, yanayomaintain masaa 24 ya ukweli, ya vifurushi vyao ni Zantel na Airtel.
 
haya nilikuwa nje ya mtandao. nimerudi, nimesoma maelezo, na nimekuelewa. Kwa nini msibadili mtindo kuleta thamani ya fedha ya watumiaji wa mtandao wenu? huoni kama huo mtego wa kusema dakika 60 unadangaya watu kwa kuwa hakuna kipengele cha kusema LAZIMA UANZIE MWANZONI MWA HIYO SAA?

Kwanini msiweke hiko kipengele kuokoa watu wanaojiamulia kununua hiyo happy hour bila kuangalia kama wamenunu dakika ngapi ndani ya muda?

Wewe Vodacom tanzania hapo bado haujakwepa lawama ya udanganyifu hata kidogo.... Hiyo katika marketing inaitwa Deceptive Advertising, na ni jinai ya kibiashara hivyo. Badilikeni!

Habari tzbiz maelezo kuhusu huduma yapo, ukipiga *149*01# ukachagua Happy Hour utakutana na taarifa kama jinsi zinavyoonekana katika picha hizi.
 

Attachments

  • 2014-07-31 09.12.29.png
    2014-07-31 09.12.29.png
    19.1 KB · Views: 107
  • 2014-07-31 09.12.42.png
    2014-07-31 09.12.42.png
    9.2 KB · Views: 114
Last edited by a moderator:
haya nilikuwa nje ya mtandao. nimerudi, nimesoma maelezo, na nimekuelewa. Kwa nini msibadili mtindo kuleta thamani ya fedha ya watumiaji wa mtandao wenu? huoni kama huo mtego wa kusema dakika 60 unadangaya watu kwa kuwa hakuna kipengele cha kusema LAZIMA UANZIE MWANZONI MWA HIYO SAA?

Kwanini msiweke hiko kipengele kuokoa watu wanaojiamulia kununua hiyo happy hour bila kuangalia kama wamenunu dakika ngapi ndani ya muda?

Wewe Vodacom tanzania hapo bado haujakwepa lawama ya udanganyifu hata kidogo.... Hiyo katika marketing inaitwa Deceptive Advertising, na ni jinai ya kibiashara hivyo. Badilikeni!
Nadhani mnajua kuwa huu ni mtandao wenye watu wengi tanzania kwa hiyo wanajua advantage yao sokoni. Kila mtu anaelewa ukisema uwingi kwa watz inaimply kwn v2 vikuu vitatu. 1. ignorance 2. non educated 3. njaa. Popote penye watz kwa wingi ujue v2 hivyo vipo
 
Leo nimejiunga na kifurushi cha cheka bombastic cha sh. 3499 badala ya kupata Mb 300 za internet nimepata Mb 200. Tamaa itawaponza vodacom maana watu wengi mtaani wanawakimbia
 
nimekuwa mteja wako kwa muda mrefu sana lakini sasa naona ni muda mwafaka kukuhama..

mimi ni mtanzania ambae ninataka mtandao wenye garama nafuu za mawasiliano..

lakini hata kama nimekuwa mteja wako hujanifunga kiasi cha kuendelea kuung'ang'ania wakati naona kuna uhuru kwingineko..

1.siku hizi kupiga simu voda huduma kwa wateja UNALIPIA.. UJINGA HUU.. mbaya zaidi wahudumu wanabaki kukupiga bla blaaa na kukata simu bila kupata huduma inavyostahili na ukirudia kupiga unalipia tena na tenaaa..

2. Huduma ya m-pesa imebaki kuwa juu kuliko mtandao mwingine hapa tz kama airtel money na tigo pesa.

3. huduma za cheka bombastick zimepanda bei hasa ya kupiga mitandao mingine.. MNAKAZANA KULETA HUDUMA ZISIZO NA MASHIKO KAMA CHEKA ZOGO YA KUPIGA VODA KWENDA VODA. hupati sms wala mb za internet ukiwa na cheka zogo.. huu ni usen........ na mtapigwa bao huku mkijifanya mtandao unaoongoza tz
mitandao mingine kama airtel wameleta hadi vocha za extreem tu mfano sh 500 unapata dk 15 mitandao yote MB na sms kibao.. NITAWAACHA

CHA KUFANYA HAPA NI KUBORESHA HUDUMA VINGINEVYO KAZI ITAKUWA KWANGU KUONDOKA KWENDA KWENYE MITANDAO YENYE HUDUMA NAFUU..
 
Back
Top Bottom