Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Ndugu mteja,

Una tatizo lolote unapotumia mtandao wetu? Una ushauri wowote ili tuiboreshe huduma yetu?

Tafadhali itumie mada (thread) hii ili tukusaidie kwa urahisi.

Unapokuwa na tatizo, ili tukusaidie kirahisi zingatia haya:

  • Ni tatizo gani? (M-PESA, SMS, Calls, Internet, usajili, kukatika kwa mawasiliano n.k)
  • Maeneo gani? (Tukifahamu location, inakuwa rahisi kukuelekeza wapi uende ili upate physical assitance toka kwa vendor wetu aliye karibu nawe)
  • Tatizo limeanza lini na limejirudia au kuendelea kuwa kero kwako kwa muda gani?
  • Kama ni ushauri, zingatia ya juu lakini tutafurahi tukijua kwanini unapendekeza unachopendekeza
  • Kama ni pongezi, zingatia ya juu na tungependa pia upendekeze lipi tufanye kuzidi kuiboresha huduma kwako.

Karibu

Vodacom Tanzania
Vodacom mmeniboa Sana wafanyakazi wenu wanawaangusha hawapo kikazi ila kimaslahi zaidi Tatizo langu toka mwezi 5 baada ya kuwatafuta viongozi wajuu Jana ndo wanahangaika yaani nimekerekwa kweli.

Ushauri katika menu yenu ongezeni kipengele kitakacho mwezesha mteja kuripoti mwenendo mbuvu wawafanyakazi kweli mnakera,
 
Kuna wizi mkubwa kwa fedha za salio za wateja unaoendelea sasa hivi katika mtandao wa Vodacom.
Kwa vile hili si jungu bali ukweli nimisha report wizi huo katika kitengo cha malalamiko TCRA kwa hatua zaidi.

Nimeweka salio la Tsha 10,000 mchana wa leo kwa Mpesa ref Y23SY687 na baada ya muda mfupi nikakuta salio langu la maongezi ni sifuri.

Nikanunua vocha na kutumiwa tshs 10,000 na hela yote imekatwa tena.

Wateja wa Vodacom jihadharini, kuna mwizi kaingia mtandaoni Vodacom

UPDATE
=====
VODACOM wamefanya ustaarabu wa kunipigia baada ya kuona detail ya transaction hapo juu, na kuiona kwenye mtandao wa Jamiiforums.
Kimsingi wameapologise kwa mtafaruku uliotokea lakini wamenieleza nifike ofisini kwao kuona aian ya simu ninyotumia isije ikawa data apps ziko wazi.
Na kweli baada ya maongezi ya kuchunguza, mobile data setting ilikuwa ON, na mimeizima sasa.

Hata hivyo ni vema nitaenda kupata maelezo ya kuyeyuka kwa salio langu , karibu 20,000, kwa siku moja.
Wanabodi mtajulishwa inawezekana kuna wenye tatizo kama langu.

UPDATE
=====
Nimeonana na waheshimiwa sana wa Customer Care pale Block 4 Mlimani City.
Cha kusikitisha ni wao kushindwa kuchukua malalamiko yangu na kuyafanyia kazi, na hii ni licha ya kuwaelewesha kuwa hili tukio nalijawahi kunitokea na hii kuwa ni mara ya kwanza.

Hawa jamaa wa Customer Care ni kama mabalozi waliopewa jukumu la kusafisha kampuni ya VODACOM hata kama inanuka kwa wizi uliodhahiri.
Kitu ambacho hawajui ni kuwa nilifanya due diligence kupitia wafanyakazi ndani ya VODACOM walionidhihirishia kuwa kuna wafanyakazi wasio waaminifu ambao wana access na personal security settings za wateja.

Na wafanyakazi hao huwa "wapiga kishenzi" fedha za wateja.

Kwa kifupi mtu wa Customer Care ameshindwa kuniconvince na maelezo yake ya upotevu wa Tshs 20,000 katika mtandao wa VODACOM.
Hilo lipo maana siku narusha salio ili ninunue mda wamaongezi imekatwa nawapigia wanasema ulikopa mda WA maongezi nawauliza lini.

Najibiwa hawawezi kata Kama huna Deni.
 
Vodacom mnatuibia sana kwenye M-Pesa. Unatoa pesa kidogo tu lakini makato elfu nane. Siku moja nimetoa milioni mbili kwenye akaunti yangu ya M-Pesa lakini nilichokiona sikuamini asilani. Nilikatwa elfu nane, jambo ambalo kama ningetolea ATM kwa mikupuo mitatu ningechajiwa elfu 4000 au chni ya hapo.

Kwa hili la M-Pesa mnakera sana na wizi wenu huu wa wazi wazi na msipobadilika watu wengi sana watawakimbia pale tu mtakapogundulika na watanzania walio wengi ambao kwa sasa bado hawajajua namna mnavyowapiga wazi wazi kiasi hiki
 
Kumekuwa na tahadhali kutoka mitandao ya simu hasa Vodacom (M-PESA) kwamba wakala ukimuwekea pesa mtu ambae yupo mbali hautalipwa kamisheni yako ya muamala huo. Hii inaweza kuwa sawa kwasababu za kibiashara lakini kwa mawakala hili ni tatizo kwasababu mtu anaweza kudanganya kuwa anaweka pesa kwenye simu yake kumbe anamtumia mtu wa mkoa mwingine tofauti na alipo.


Kumbuka huwezi kumwambia mteja lete simu yako hapa nione kama SMS ya muamala unaingia kwako. Mwisho wa siku hii inakuwa imekula kwako wewe wakala kwa kukosa kamisheni yako.

Nini kifanyike?

Makampuni haya ya simu tengenezeni mfumo ambao utawawezesha mawakala kupewa WARNING wakati wanaweka pesa kwa mteja kama yuko mbali simu ikutahadhalishe kwamba "mtu unaemuwekea hela yupo mbali na eneo lako hivyo hautalipwa kamisheni yako, kuendelea bonyeza labda "1" kusitisha muamala bonyeza "2". Hii itasaidia kuwapatia kamisheni zinazostahili mawakala wanaowasaidia kuwafikishia huduma karibu na wananchi.


Asante. Natumaini maoni yangu yatafanyiwa kazi.
 
Nimejiunga GB 4 kwa week ila kesho yake tu ishaisha wakati sijadowload mavitu wala sijaangalia you tube. Nimekuwa nikivumilia ila hii imezidi. Imebidi nijaribu kwingine nikanunua GB 1 kwa siku tatu, imeenda vizuri leo siku ya tatu bado zimo 140 MB.

Kwaherini nyinyi si saizi yangu.
 
Nyie Vodacom mbona mnazuia ujumbe wenye jina Tundu Lissu kutoka,mna ajenda gani ya siri. Kwa nini mnajiingiza kwenye siasa
 
Vodacom ongezeni kwenye menyu yenu ya *149*01# command ya kurudi nyuma kila hatua unayokwenda kama mitandao mingine walivyofanya kuliko mtu kucansel kila mara anapotafuta aina ya vifurushi anavyotaka. Natumaini mtafanyia kazi.[emoji853]


Sent from cupboard using mug
 
Kwa nini mnafanya hivi Vodacom, kuanzia mwezi wa kumi, vifurushi vyenu havikai, mtu unanunua kifushi Cha wiki ndani ya saa au siku kimeisha wakati ujafanya chochote, kuweni na huruma kwa pesa za wenzenu, kwa nini nilipie wiki, na huruma iishe kabla, waliosomea Sheria msaada please,
 
Vodacom, hivi designer wa matangazo yenu ya sms mnazotutumia ni nani? ,mnaandika vitu vingine very nonesense hadi mnakera! kuna li sms mnalituma kila siku asubuhi limeandikwa "SHANGWE SHANGWENA" Ni nini hiki? mnakera na sms zenu za matangazo za hovyo hovyo, mnadhani wateja wenu wote ni wanafunzi wa sekondari au? nyie mnakera sana,,,nimebaki kuwa mteja wa MPESA tu kutokana na kua nafanya kazi sehemu ambayo wanatumia kampuni yenu kulipitisha miamala otherwise, i dont recomend mtu anunue sim card yenu!
 
Back
Top Bottom