Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Kuna wizi mkubwa kwa fedha za salio za wateja unaoendelea sasa hivi katika mtandao wa Vodacom.
Kwa vile hili si jungu bali ukweli nimisha report wizi huo katika kitengo cha malalamiko TCRA kwa hatua zaidi.

Nimeweka salio la Tsha 10,000 mchana wa leo kwa Mpesa ref Y23SY687 na baada ya muda mfupi nikakuta salio langu la maongezi ni sifuri.

Nikanunua vocha na kutumiwa tshs 10,000 na hela yote imekatwa tena.

Wateja wa Vodacom jihadharini, kuna mwizi kaingia mtandaoni Vodacom

UPDATE
=====
VODACOM wamefanya ustaarabu wa kunipigia baada ya kuona detail ya transaction hapo juu, na kuiona kwenye mtandao wa Jamiiforums.
Kimsingi wameapologise kwa mtafaruku uliotokea lakini wamenieleza nifike ofisini kwao kuona aian ya simu ninyotumia isije ikawa data apps ziko wazi.
Na kweli baada ya maongezi ya kuchunguza, mobile data setting ilikuwa ON, na mimeizima sasa.

Hata hivyo ni vema nitaenda kupata maelezo ya kuyeyuka kwa salio langu , karibu 20,000, kwa siku moja.
Wanabodi mtajulishwa inawezekana kuna wenye tatizo kama langu.

inawezekana wewe umepoozwa tu mimi wameniibia tshs 30337 na 600mb eti wananiambia zimetumika kwenye data ndani ya saa tatu na ni kwenye simu..voda ni waizi..na ninahamia airtel..
 
Hili jambo lilinitoke hata mimi majuzi tuu, kila nikitaka kujiunga kifurusha ina kataa lakini salio lina katwa hadi likaisha. nili kerwa sana siku hiyo lakini niliwapigia tuka yamaliza na customer care.

Vodacom ni wasikivu sana.

voda ni waizi majambazi kama ccm, tarehe 28.12.2013 wameniibia 30337 na kifurushi cha 600mb ndani ya saa tatu na ni kwenye simu, nimefatilia mpaka nimechoka nimeamua kuwa hama tu...
 
Airtel ya tosha, nyingine za nini? buku tu unapewa dkk 40 za kupiga mitandao yote bila kusahau internet na sms
 
Siwezi kubisha. Utamu wa fweza umewakolea wahudumu wa mtandao huu! Dawa ni kuhama tu.
 
Uzembe wako mwenyewe afu wawalaumu voda, wakuibie wewe una nini cha kuibiwa
 
nachokiona voda hawana cha kupoteza kutoka kwa mteja mmojammoja wa eneo lenye ushindani km dar ambako watu wanabadilisha line kila kukicha.

wateja wao wengi ni makampuni 'corporates' na wana hazina ya wateja wengi wa muda mrefu 'royal' hasa mikoani.huko ndo wanapiga hela ndefu na ya uhakika.
 
vodacom ni wezi sana mi nilishawafata hadi oficini kwao ubungo na kuwatishia kuwapeleka Tume ya mawasiliano. yaani wanaiba sana hela zilizo kwenye mpesa, wakikutumia hata msg ya matangazo yao ukiangalia balance kwenye mpsea utakuta wamekuchagi
 
Heheheee... JF ni balaa... Customer Care kasepa.. Waja leo warudi leo..
 
Unajiunga ktk promosheni zao, wanakuambia piga namba fulani kisha aidha ujiunge na cheka time au internate masaa 24, unaambiwa subiri ujumbe mfupi utajibiwa. Unasubiri weee! Hakuna kitu, ukiangalia salio limekatwa! Na hakuna huduma hiyo wala nini! Ni kwa nini hamtuhurumii wateja wenu?

Niliona wametoa tangazo kule twitter wakisema UKIWA NA SALIO LAKO HAKIKISHA UMEZIMA INTERNET KWANZA AU USWITCH OFF NDO UNUNUE KIFURUSHI, Jaribu hiyo, ila mimi Niko Airtel Mkuu,


Halafu Nyie Watumiaj wa Voda Threads zenu zmezd humu kulalamika kila uchao harafu hamchukui action Hameni Bwana!!
 
wadau vodacom sasa hivi nao ni wanasiasa,nimenunua umeme kwa m-pesa tangu saa mbili mpaka sahvi wamechukua pesa yangu hawajanitumia namba zangu za umeme nawapigia wananipa majibu kama ya mawaziri mizigo,,,ah tanzania kiboko.
 
Mkuu nijulishe kuhusu internet unapewa mb ngapi?

Mb 300 kama sijakosea, ila kuna cha watumiaji wa kawaida na wenye kipato cha kawaida kama sisi 3000 unapata Dk 100 kwenda mitandao yote, Mb 400 utumie ndani ya wiki
 
Pole sana ndugu, kunakipindi walikula hela yangu na umeme sikupata kabisa. Tangu kipindi hicho nimeshapata somo.
 
Jana nilipigwa buki tatu kwa dizaini hiyo na mtandao nimeshahama,nipo baba lao
 
Kuna kitu nadhani watu wengi wanaolalamika kuwa wanaibiwa mnakosea. Kama unatumia smartphone na hujajiunga na bando la internet ni lazima pesa yako itaendelea kuliwa taratibu hadi iishe. Cha msingi kama wewe hutumii inernet nenda kwenye mobile network then iweke off! Otherwise applications ambazo zinafanyakazi katika background zitamaliza pesa yote.

Mbona mitandao mingine haiwi hivo
 
Mimi nilihama huko siku mingi sana baada ya kuona mitandao mingine inanafuu zaidi, na washkaji kibao wameshaga hama pia baada ya kugundua wanakatwa hela bila kuelewa wametumiaje
 
TCRA wana mtindo wa kukalia malalmiko ikipita wiki mbili hawakujibu wakilisha malalamiko kwenye tume yaa ushindani ofisi zao ziko ubungo

Vodacom wameiweka serikali hii mfukoni. Hakuna cha wizara ya mawasiliano wala hiyo TCRA wala Polisi, wote wamevimbiwa sumu waliyokula - "Rushwa".

Haiwezekani nchi nzima walalamike na wahuni hawa wajifanye hawasikii!
Nyerere alisema ukishapokea rushwa unageuka mtumwa, na sasa tumeyaona. Haya ni matokeo ya viongozi kuhongwa hisa na kuwa "wadau" wa makampuni ya kitapeli kama hawa Vodacom na Tigo.

Washenzi hawa wanafanya dhambi ambazo wangezifanyia huko wanakotoka wangeaibika hata wakose pa kuficha sura zao.

Ni wajibu wa TCRA kuhakikisha usalama wa wananchi dhidi ya wizi unaofanywa na makampuni yaliyosajiliwa nayo.
Wanawafumbia macho tu kwa sababu wao ni wanufaika wa hujuma hizo.

Huu wizi ulianza kwa hela ndogondogo kama sh. 20/=, 50,100 na sasa hata 10000/=! Serikali "sikivu" bado imelala kitandani kimoja kimahaba na wahalifu hawa. Hawa hawana tofauti na vibaka wa mitaani ni lazima washughulikiwe na serikali au sisi wenyewe.
 
Back
Top Bottom