Mnamo March 2024, nilituma hela kwa mtu nkaambiwa haikufanikiwa kwenda. Baada ya siku kama kumi, nikagundua Salio langu limepungua tofauti na transactions nilizofanya, Baada ya kujiridhisha nikawapigia simu huduma kwa wateja wakaniambia hela ilienda ila haikukatwa kwenye account yangu, nikahoji mbona notification ilisema hela haijaenda na kweli Salio langu lilibaki kama lilivo? Nilijibiwa hela ilienda na haiwezi kurudishwa . Sikuridhishwa na majibu ya huduma kwa wateja nikaamua kwenda ofisini kwa maeneo ya Posta.
Baada ya kuwaelezea wahudumu wa ofisini nikaambiwa mtandao ulikuwa mbovu siku hiyo ila hela ilienda, nikawauliza mbona niliambiwa TRANSACTION FAILED, na Salio langu lilibaki kama lilivo.
Mwisho wa yote nikaambiwa watafatilia hela yangu itarudishwa kwenye account yangu lakini Baada ya siku nikaambiwa imeshindikana.
In short ubovu wa mtandao wao ulinigharimu Mimi Elfu arobaini ambayo haikuwa kwenye budget ya matumizi yangu.
Baada ya kuwaelezea wahudumu wa ofisini nikaambiwa mtandao ulikuwa mbovu siku hiyo ila hela ilienda, nikawauliza mbona niliambiwa TRANSACTION FAILED, na Salio langu lilibaki kama lilivo.
Mwisho wa yote nikaambiwa watafatilia hela yangu itarudishwa kwenye account yangu lakini Baada ya siku nikaambiwa imeshindikana.
In short ubovu wa mtandao wao ulinigharimu Mimi Elfu arobaini ambayo haikuwa kwenye budget ya matumizi yangu.