Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke

Nabii Pascal Mayalla ambaye pia ni mjukuu wa Ng'wana Malundi.Umesomeka,usiyejulikana kuwa unanasaba na Eagle House ambaye utakuja kujulikana🤣🤣🤣
 
Bado nawaza kwa nn tuna Imani na viongozi wa CCM? Kwa nn hiyo 2025 asiwe kiongozi kutoka chama kingine?
 
Kwa sababu wachache mnalamba asali? Kwa hiyo mnaona sawa tu hadi 2040?
 
Kazi ya msingi ya kiongozi ni kutatua matatizo, siyo kwenda kunywa chai Ikulu.

Anaposhindwa kutatua matatizo automatically anakosa sifa ya kuendelea kukalia hicho kiti.

Hivi kuna Rais anapenda madaraka kama Samia? Au ulikuwa wapi kipindi kile hadi anatetemeka kisa Ndugai anam-challenge?

Ulikuwa wapi wakati Prof. Kabudi na Lukuvi wanatolewa kisa anahisi ni tishio kwenye Urais wake wa 2025?

Ulikuwa wapi wakati CHADEMA wanapewa kesi ya Ugaidi kisa wanadai Katiba Mpya ambayo itampunguzia madaraka?

Kikatiba, kipindi chake kinaisha 2025 boss, na hakuna mtu atambugudhi kabla ya hapo.

Kuhusu Membe na Kinana tunaheshimu mawazo yako.
 
Soma between the line ,sio sauti kutoka within amesema sauti imesema manake wenye nchi wamesema na kuamua mwinyi awe Rais wa Tz .
 
Bado nawaza kwa nn tuna Imani na viongozi wa CCM? Kwa nn hiyo 2025 asiwe kiongozi kutoka chama kingine?
Tatizo lililopo mpaka sasa kwa viongozi wa vyama vya upinzani ni kukosekana kwa umoja na mshikamano baina yao!

Halafu wengi wa viongozi wa hivyo vyama ni mamluki wa CCM! Imagine mtu kama John Cheyo, John Shibuda, Augustino Lyatonga Mrema, Seif Rashid Mohamed, Prof. Ibrahim Lipumba, huyu mwamba Zitto Kabwe, nk.

Kiukweli hawaaminiki hata kidogo! Chadema nao wanaamini sana katika siasa za harakati kuliko zile za maridhiano! Yaani kukaa meza moja na CCM kwao wanaona kama ni jambo lisilo wezekana kabisa! Mwisho wa siku CCM inazidi tu kuneemeka kutokana na haya mapungufu ya wapinzani.
 
hahahahaha bila shaka wazo lako ndio kitakachotokea... CCM wajanja sana...hii ndio karata yao 2025 -2030-2035....Upepo utakuwa umetulia halafu mnaletewa christiana na watakuwa wameshajipanga tena..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…