Marais wa Nchi Hupangwa na Mungu, hata JPM alikuwa ni Chaguo la Mungu kwa Tanzanzia, ila Mungu huweza kulikatiza chaguo lake wakati wowote na kumchagua mwingine, hii haikuanza leo, toka enzi za Nabii Musa, alikatizwa hakuingia nchi ya ahadi Caanan, kwa sababu fulani. Everything happens for a reasons anazojua Mungu mwenyewe, hivyo hata Samia ni mpango wa Mungu kwa Tanzania labda hadi 2025 ni Mungu tuu mwenyewe anajua. Kama Samia ni mpango wa Mungu kwa Tanzania 2025 -2030, then Mungu atasema nasi hapa katikati kabla ya 2025, kwasababu hata JPM, hakuna aliyejua Mungu alipanga nini, vivyo hivyo kwa Samia 2025, ni Mungu tuu pekee ndiye ajuaye amepanga nini, lakini kwa utaratibu wa CCM, urais huu wa sasa wa Mama Samia ulioletwa kwa kudra tuu za Mwenyezi Mungu, hii ni awamu yake ya kwanza, hivyo kila mtu anajua utaratibu wa CCM, anajua uchaguzi wa 2025 ndio awamu yake ya pili ya Mama Samia but only if kama ndivyo Mungu alivyopanga.
Kwa vile hili ya yeye kugombea 2025, rais Samia mwenyewe aliisha liweka vizuri kabisa ile siku anahojiwa na Salim Kikeke wa BBC, baada ya kuhojiwa kama atagombea urais 2025, rais Samia alijibu vizuri kabisa kuwa "kwa sasa tufanye kwanza kazi, ya 2025 tumwachie Mungu maana no one is shure kufika 2025", hivyo hata rais Samia aliposema 2025 tutamchagua mwanamke, hajamaanisha lazima mwanamke huyo awe ni yeye!. Hivyo ni busara kwa rais wetu Samia, hili la ugombea wa 2025, asilizungumze zungumze sana kwa sasa, ni vyema akaendelea na msimamo wake ule ule wa kwenye BBC kuwa ya 2025 tumuachie Mungu. Kwa sasa, rais aendelee ku deal na haya ya Kaizari, kwa kuchapa kazi na kazi iendelee na yale ya Kimungu tumuachie Mungu mwenyewe.
Swali linabaki, Jee Samia ndio mpango wa Mungu kwa Tanzania, 2025 ....
Sasa kama mpangaji ni YEYE, na ndie amepanga 2025 ni yeye, then who are we to say no?.
2025 Twende na Mwanamke!.
Paskali