Voices From Within: Je, wajua yuko Peponi, Mbinguni, Kwa Baba yake? Why kumshutumu, kumsakama na kumsimanga? Aachwe apumzike kwa amani

Voices From Within: Je, wajua yuko Peponi, Mbinguni, Kwa Baba yake? Why kumshutumu, kumsakama na kumsimanga? Aachwe apumzike kwa amani

K
Anayeleta ndiye ametwaa, anapoleta huwa hatoi sababu na anapotwaa pia huwa hatoi sababu, hivyo hakuna yeyote ajuaye for sure the exact reasons za kutwaliwa, ila pia tupo akina sisi, ambao kabla hajawa, tulisema kitu, Elections 2015 - Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John Pombe Magufuli
Aliposhinda uchaguzi ile 2015, tukasema kitu Elections 2015 - If you can't beat them, join them! He is the worst dictator. Let's pray for him!

Baada ya mtu kulalamikia matokeo pia tukasema kitu Elections 2015 - Kama Hii ni Kweli, Then, Serikali Yetu ni Serikali Dhalimu?, Haramu?. Hukumu ya Karma ii Juu Yake!

Kabla ya uchaguzi wa 2020 tukashauri Ombi Maalum, Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu wa 2020, Uendeshwe kwa Ceteris Peribus, Sio Kwa Mutatis Mutandis. Tutabarikiwa!

Baada ya kushuhudia rafu zilizochezwa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa 2019, tukasema kitu Ushindi mtamu ni ushindani katika uwanja sawa, sio ule wa mezani. Magufuli, kasi yako ni ushindi wa kishindo. Ruhusu ushindani wa haki, sawa na wazi

Kwenye hizo hoja zote, pia ninaweka kitu kinachoitwa causes and effects, kwenye effects naweka the consequences.

Kilichomuondoa Blaza ni the accumulation of bad karma "The Power of 'Karma'- Ndio Hukumu Pekee ya Haki Kamili Hapa Duniani!, Unahukumiwa kwa Matendo Yako!
Yaani ni karma imekula kichwa!.

Uzuri wa karma, ukiishalipa deni la karma, deni linakuwa limelipwa, unatakasika, unaingia peponi, ndivyo JPM alivyoingia mbinguni.
P
Kaka naamini ni mmoja ya watu unaelewa vizuri sana mambo ya karma na jinsi inavyofanya kazi.
🙌🙌🙌....

Naam sababu ya kutokea jambo ni huyo aliyeruhusu na kadhalika kutotokea ni huyo pia.

Binadamu hukumu zetu zinaongozwa sana na nyakati zilizopita ila Mungu nafikiri anahukumu kwa wakati uliopo sasa hapo ndio pagumu kuelewa iweje mwenye historia ya uovu akubalike na Mungu kumbe Mungu anahusika na wakati uliopo na hata sekunde chache kabla ya Roho na mwili kuachana Mtu anaweza kuiona Mbingu kutokana na neema.
 
K

Kaka naamini ni mmoja ya watu unaelewa vizuri sana mambo ya karma na jinsi inavyofanya kazi.
🙌🙌🙌....

Naam sababu ya kutokea jambo ni huyo aliyeruhusu na kadhalika kutotokea ni huyo pia.

Binadamu hukumu zetu zinaongozwa sana na nyakati zilizopita ila Mungu nafikiri anahukumu kwa wakati uliopo sasa hapo ndio pagumu kuelewa iweje mwenye historia ya uovu akubalike na Mungu kumbe Mungu anahusika na wakati uliopo na hata sekunde chache kabla ya Roho na mwili kuachana Mtu anaweza kuiona Mbingu kutokana na neema.
Ni kweli kabisa Mungu hutoa hukumu katika wakati uliopo sasa, haijalishi mtu alifanya makosa gani, ukitubu kabla hujafa, unasamehewa na unaingia peponi, ila kitu kikubwa zaidi ni "tunaokolewa kwa neema na sio kwa matendo". Neema hiyo imemshikia JPM.
P
 
Wanabodi,

Why watu wengine waendelee kumshutumu, kumsakama na kumsimanga?. Kwa nini asiachwe ajipumzikie zake kwa amani!. Mtu ameisha tangulia mbele ya haki, kwanini watu waendelee kumsema sema kwa ubaya.
nikaisikia sauti, voices from within kuwa JPM yuko peponi, ahera, mbinguni kwa Baba!

Nimejiridhisha bila chembe ya shaka, huyu mtu yuko mbinguni, peponi kwa Baba yake!, yuko na Baba yake!.

Hapa simaanishi kuwa JPM yuko peponi kwasababu he is perfect kama malaika, no!. JPM was a human being hivyo he is not perfect and no one is perfect, kilichofanya hiyo sauti ni despite his human mistakes JPM alitubu kabla ya umauti na kusamehewa dhambi zake zote na makosa yake yote, na ndio maana nimeambiwa, sasa he is in heaven now!.

Kwa bandiko hili, sasa ningewaomba watu humu, kutoendelea kumsakama, kumshutumu, kumsimanga na kuendelea kumsema vibaya, na badala yake tumwache apumzike kwa amani. Kama Mungu mwenyewe amemsamehe na kumuita kwake, who are you kuendelea kumsema sema vibaya?

Mungu Ibariki Tanzania

Paskali.
Ndiyo maana Mungu akamtupilia jehanam
Mkuu Stuxnet , huyu mwamba hakutupwa jehanam, alipitia toharani na sasa yuko mbinguni peponi!.
Sisi Wakristo, tunaokolewa kwa neema na sio kwa matendo!.
P
 
ushahidi uwepo au usiwepo, ukweli ni kwamba nchi hii ilishawahi kutawaliwa na mtu katili sana ambaye anajutia alichokifanya huko kuzimu hata sasaivi mnavyoandika. Mwogopeni Mungu, na ninyi mlio karibu nao washaurini vyema.
Mkuu Yesu Anakuja, Huyu ni Mkatoliki, Mkatoliki akipata sakramenti ya Upako Mtakatifu kabla hajafa, dhambi zake zote zinakuwa zimeondolewa!, hivyo akifa, haendi kuzimu, anakwenda toharani, kisha anaingia mbinguni!, hivyo saa hizi yuko peponi mbinguni kwa Baba yake, yuko na Baba yake!.
P
 
Mkuu Yesu Anakuja, Huyu ni Mkatoliki, Mkatoliki akipata sakramenti ya Upako Mtakatifu kabla hajafa, dhambi zake zote zinakuwa zimeondolewa!, hivyo akifa, haendi kuzimu, anakwenda toharani, kisha anaingia mbinguni!, hivyo saa hizi yuko peponi mbinguni kwa Baba yake, yuko na Baba yake!.
P
ndugu yangu pascal, mwanasheria mwenzangu, hii ndio sababu huwa tunasema muokoke, muachane na imani potofu kabisa ya shetani, aliyowadanganya kwamba ukipata sakrament unasamehewa dhambi, au ukiombewa vizuri siku ya maziko unasamehewa dhambi, au ukifa watakuombea ukiwa kaburini ukasamehewa dhambi. hii haijathibitishwa na eneo lolote la Biblia, na ni uongo wa shetani.

Biblia inasema, saa ya wokovu ni sasa, nia uishi ukijua kuwa, baada ya kifo ni hukumu, hakuna kutubu wala kutubiwa, na kila mtu atabeba mzigo wake mwenyewe, padre hawezi kutubu kwa ajili yako ukasamehewa. huu ndio ukweli mchungu. hii ndio sababu imefanya mapadre wa katoliki wanaishi kama miungu watu, kwa sababu wanaamini wameshika funguo za kukufanya uende mbinguni au motoni kwa kukuombea ukifa, na ndio fimbo wanapigia watu wasiohudhuria jumuia, wanaweza kuamua tu kwamba hawakuziki, na wanaamini wakifanya hivyo hautaenda mbinguni. wakati wao weneywe ni watenda dhambi wakubwa,wazinzi na wachawi.

WAEBRANIA 9:27 imeweka wazi kwamba, "baada ya kifo ni hukumu", nafasi yako ya kutubu ni sasa, wewe binafsi kutengeneza mambo yako na Mungu, ikitokea umetoka hata hapo nje ukagongwa na gari ukafa kabla ya kutubu, kifuatacho ni hukumu, hata wakikuombea maombi miliono its a waste of time.

kwa sababu ni usiku sana,ngoja nikuache na mstari huo, kesho nitakuletea mingine, God willing.
 
Wanabodi,

Nimesikia sauti ya Voices From Within ikiniambia JPM yuko Mbinguni kwa Baba, hivyo nauliza swali, jee wajua kuwa JPM yuko peponi, Mbinguni, Kwa BABA YAKE?

Why watu wengine waendelee kumshutumu, kumsakama na kumsimanga?. Kwa nini asiachwe ajipumzikie zake kwa amani!. Mtu ameisha tangulia mbele ya haki, kwanini watu waendelee kumsema sema kwa ubaya.
Hata ya kutoka kwa kitabu cha Eric Kabendera, hoja za bandiko hili bado zinasimama kwa mujibu wa maelezo ya Eric mwenyewe
View: https://youtu.be/HfQqupIGlKM kuwa JPM alitenda kwa hasira,baada ya kutenda alijutia,kwa sisi Wakristo Wakatoliki ukitenda dhambi,ukaenda kuungama,dhambi zako zinaondolewa,unatakasika。

JPM siku za mwisho alitubu dhambi zake zote,akasamehewa akapata sacrament ya mwisho ya upako mtakatifu, ndipo akatwaliwa, kwa vile wakati wa mpako mtakatifu ni tayari alikuwa kitandani,then alipotwaliwa alifikia toharani kwanza ndipo akaingia mbinguni。Hivyo JPM, yuko peponi,pia anakisoma kitabu cha Eric, kama kuna uongo wowote mtu anamsingizia marehemu ambaye hawezi kujitetea,sasa hivi mtu atanyakuliwa!。
P
 
Frm saba saba special miaka ya 2005 +ad kuja kua chawa wa Siasa za Ccm

Wacha nisome komenti kuna ving sana vyakujifunza
 
Hata ya kutoka kwa kitabu cha Eric Kabendera, hoja za bandiko hili bado zinasimama kwa mujibu wa maelezo ya Eric mwenyewe
View: https://youtu.be/HfQqupIGlKM kuwa JPM alitenda kwa hasira,baada ya kutenda alijutia,kwa sisi Wakristo Wakatoliki ukitenda dhambi,ukaenda kuungama,dhambi zako zinaondolewa,unatakasika。

JPM siku za mwisho alitubu dhambi zake zote,akasamehewa akapata sacrament ya mwisho ya upako mtakatifu, ndipo akatwaliwa, kwa vile wakati wa mpako mtakatifu ni tayari alikuwa kitandani,then alipotwaliwa alifikia toharani kwanza ndipo akaingia mbinguni。Hivyo JPM, yuko peponi,pia anakisoma kitabu cha Eric, kama kuna uongo wowote mtu anamsingizia marehemu ambaye hawezi kujitetea,sasa hivi mtu atanyakuliwa!。
P

Hii kisheria imekaaje!? Hawezi kishitakiwa na familia au serikali maana hizi ni Tuhuma nzito sanaa na kashifa kwa serikali. Vinginevyo labda kama kuna ushahidi wa kutosha.
 
Hii kisheria imekaaje!? Hawezi kishitakiwa na familia au serikali maana hizi ni Tuhuma nzito sanaa na kashifa kwa serikali. Vinginevyo labda kama kuna ushahidi wa kutosha.
EK ana ushahidi wa kuambiwa na mashuhuda, sisi waandishi tuna kinga ya kisheria, kutotaja ma source wetu inaitwa the confidentiality of the source, huyo aliyemwambia ni wale jamaa zetu wenye kinga ya kiofisi ya non disclosure, hovyo serikali ikimfungulia kesi ni itachafuka, inachoweza kufanya ni kuchutama tuu, msemaji
Wa serikali atakanusha tuu, lakini hakuna mashitaka yoyote yatafunguliwa.
P
 
Wanabodi,

Nimesikia sauti ya Voices From Within ikiniambia JPM yuko Mbinguni kwa Baba, hivyo nauliza swali, jee wajua kuwa JPM yuko peponi, Mbinguni, Kwa BABA YAKE?

Why watu wengine waendelee kumshutumu, kumsakama na kumsimanga?. Kwa nini asiachwe ajipumzikie zake kwa amani!. Mtu ameisha tangulia mbele ya haki, kwanini watu waendelee kumsema sema kwa ubaya.

Hapa simaanishi kuwa JPM yuko peponi kwasababu he is perfect kama malaika, no!. JPM was a human being hivyo he is not perfect and no one is perfect, kilichofanya hiyo sauti ni despite his human mistakes JPM alitubu kabla ya umauti na kusamehewa dhambi zake zote na makosa yake yote, na ndio maana nimeambiwa, sasa he is in heaven now!.
Paskali.
Ila heko sana Godbless lema alituambia utabili wote juu ya kaka alietwaliwa (shetani akateseke mbwa yule)
Huwezi kumuita binadamu shetani, huwezi kumtukana mtu mbwa!.
P
 
Huwezi kumuita binadamu shetani, huwezi kumtukana mtu mbwa!.
P
Huwezi mpangia alieumizwa na aliye juu ya sheria ajilipie vipi na kiasi gani kwa namna gani ,kwan sifungwi na maadili ya dini bali katiba ,mbwa haijakaa sawa nafuta ni kenge.
Biblia imeonya vikali juu ya kuambatana na mtu mbaya

Avoiding association with sinners
  • Psalm 1:1: "Blessed is the man who walks not in the counsel of the wicked, nor stands in the way of sinners"

  • 1 Corinthians 5:11: "Do not associate with anyone who bears the name of brother if he is guilty of sexual immorality or greed"

  • 2 Corinthians 6:14: "Do not be unequally yoked together with unbelievers"

  • 2 Corinthians 6:17: "Come out from among unbelievers, and separate yourselves from them"
So kama mkristo mwenzangu weka mbali bawa lako na yule muovu watu tumezika ndugu zetu .
 
Wanabodi,

Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa huwaletea makala zangu za Kwa Maslahi ya Taifa. Mada ya leo ni a bit abstract, ambapo Nimesikia sauti ya Voices From Within ikiniambia JPM yuko Mbinguni kwa Baba, hivyo nauliza swali, jee wajua kuwa JPM yuko peponi, Mbinguni, Kwa BABA YAKE?

Why watu wengine waendelee kumshutumu, kumsakama na kumsimanga?. Kwa nini asiachwe ajipumzikie zake kwa amani!. Mtu ameisha tangulia mbele ya haki, kwanini watu waendelee kumsema sema kwa ubaya.

Mimi mwana jf mwenzenu ni Mzee wa Sauti za Ndani "the inner voice", unafanya kitu fulani na mara unasikia sauti from within ikikuambia jambo fulani.

Angalizo kuhusu Abstract Topics.

Issues na mtu akiisha kufa, we all knows what happens to the body, but roho huwa inakwenda wapi, no one knows for sure, hivyo tunategemea mafundisho ya dini zetu.

Kuna sisi dini za wana wa Nabii Ibrahim, Wakristo na Waislamu tumefunzwa kuhusu mbinguni, peponi, ahera, jehanam ya moto wa milele, na kuna siku ya mwisho siku ya hukumu ya mwisho ya kiama atakapo rudi Mwana wa Adamu, ambapo kutakuwa na ufufuko wa miili na uzima wa milele.

Kuna wenzetu wa Buddhism na Hindu ambao ni waumini wa karma, wao wanaamini kwenye after life na incarnation.

Hakuna yeyote awaye yote aliwahi kufa akayashudia hayo na kurejea duniani kututhibitishia mbingu ipo, peponi kupo na motoni kupo, wala waumini wa reincarnation no one can say for sure alikuwa nani before, zaidi ya ushahidi wa deja vu, hakuna uthibitisho wowote wa reincarnation Ila kwa vile na mimi niliishi India, I know for sure karma ipo and it's for real!

Hivyo hii mada ni mada ya imani, kama wewe huamini, please keep your faith nakuomba usibeze imani za wengine, ukijiona huamini, nakuomba jipitie zako kimya kimya, tuache sisi waumini.

Leo asubuhi nilikuwa nasoma michango ya wachangiaji wa bandiko langu hili. "Mimi ni Mwenzenu Hapa, Sijabadilika ni Yule Yule "KaJoni" - Ni Maneno Simple, Humble and Down to Earth Yenye Maana Kubwa!

Sasa ni wakati nasoma bandiko lenyewe, na naomba nililete hapa bandiko lenyewe lote kwa faida ya wavivu to follow links.

Ndipo nikaisikia sauti, voices from within kuwa JPM yuko peponi, ahera, mbinguni kwa Baba!

Kwa kawaida ya sauti, huwa inakuambia tuu kitu na haikupi sababu, hivyo naomba msiniulize sababu, hapa kazi yangu ni moja tuu kuwaeleza kile nilichosikia Leo ni JPM yuko peponi!

Hivyo baada ya kuisikia hiyo sauti nikamsikiliza tena JPM kwa makini sana katika video hii
Nimejiridhisha bila chembe ya shaka, huyu mtu yuko mbinguni, peponi kwa Baba yake!, yuko na Baba yake!.

Hapa simaanishi kuwa JPM yuko peponi kwasababu he is perfect kama malaika, no!. JPM was a human being hivyo he is not perfect and no one is perfect, kilichofanya hiyo sauti ni despite his human mistakes JPM alitubu kabla ya umauti na kusamehewa dhambi zake zote na makosa yake yote, na ndio maana nimeambiwa, sasa he is in heaven now!.

Kwa bandiko hili, sasa ningewaomba watu humu, kutoendelea kumsakama, kumshutumu, kumsimanga na kuendelea kumsema vibaya, na badala yake tumwache apumzike kwa amani. Kama Mungu mwenyewe amemsamehe na kumuita kwake, who are you kuendelea kumsema sema vibaya?

Mungu Ibariki Tanzania

Paskali.

Voices from within-Advocate Mayalla
 
Voices from within-Advocate Mayalla
Voices from within ni kitu cha kweli, Mungu kweli yupo, ila pia na shetani yupo!, hivyo hizi voices from within, ni sauti ya YEYE aliye ndani yako!, ila pia hata yeye, naye pia yumo ndani yako, hivyo sauti nyingine zinaweza zikawa sio sauti za kwake YEYE bali ni sauti za yeye tuu!. Kama ni sauti ya YEYE, lazima itatimia!. Mfano mimi mpaka leo, mpaka kesho, bado naamini HII kitu ni sauti kwake YEYE!.
P
 
JPM alikuwa Rais katili kuwahi kutokea Tanzania, apumzike panapomstahili
Wanabodi,

Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa huwaletea makala zangu za Kwa Maslahi ya Taifa. Mada ya leo ni a bit abstract, ambapo Nimesikia sauti ya Voices From Within ikiniambia JPM yuko Mbinguni kwa Baba, hivyo nauliza swali, jee wajua kuwa JPM yuko peponi, Mbinguni, Kwa BABA YAKE?

Why watu wengine waendelee kumshutumu, kumsakama na kumsimanga?. Kwa nini asiachwe ajipumzikie zake kwa amani!. Mtu ameisha tangulia mbele ya haki, kwanini watu waendelee kumsema sema kwa ubaya.

Mimi mwana jf mwenzenu ni Mzee wa Sauti za Ndani "the inner voice", unafanya kitu fulani na mara unasikia sauti from within ikikuambia jambo fulani.

Angalizo kuhusu Abstract Topics.

Issues na mtu akiisha kufa, we all knows what happens to the body, but roho huwa inakwenda wapi, no one knows for sure, hivyo tunategemea mafundisho ya dini zetu.

Kuna sisi dini za wana wa Nabii Ibrahim, Wakristo na Waislamu tumefunzwa kuhusu mbinguni, peponi, ahera, jehanam ya moto wa milele, na kuna siku ya mwisho siku ya hukumu ya mwisho ya kiama atakapo rudi Mwana wa Adamu, ambapo kutakuwa na ufufuko wa miili na uzima wa milele.

Kuna wenzetu wa Buddhism na Hindu ambao ni waumini wa karma, wao wanaamini kwenye after life na incarnation.

Hakuna yeyote awaye yote aliwahi kufa akayashudia hayo na kurejea duniani kututhibitishia mbingu ipo, peponi kupo na motoni kupo, wala waumini wa reincarnation no one can say for sure alikuwa nani before, zaidi ya ushahidi wa deja vu, hakuna uthibitisho wowote wa reincarnation Ila kwa vile na mimi niliishi India, I know for sure karma ipo and it's for real!

Hivyo hii mada ni mada ya imani, kama wewe huamini, please keep your faith nakuomba usibeze imani za wengine, ukijiona huamini, nakuomba jipitie zako kimya kimya, tuache sisi waumini.

Leo asubuhi nilikuwa nasoma michango ya wachangiaji wa bandiko langu hili. "Mimi ni Mwenzenu Hapa, Sijabadilika ni Yule Yule "KaJoni" - Ni Maneno Simple, Humble and Down to Earth Yenye Maana Kubwa!

Sasa ni wakati nasoma bandiko lenyewe, na naomba nililete hapa bandiko lenyewe lote kwa faida ya wavivu to follow links.

Ndipo nikaisikia sauti, voices from within kuwa JPM yuko peponi, ahera, mbinguni kwa Baba!

Kwa kawaida ya sauti, huwa inakuambia tuu kitu na haikupi sababu, hivyo naomba msiniulize sababu, hapa kazi yangu ni moja tuu kuwaeleza kile nilichosikia Leo ni JPM yuko peponi!

Hivyo baada ya kuisikia hiyo sauti nikamsikiliza tena JPM kwa makini sana katika video hii
Nimejiridhisha bila chembe ya shaka, huyu mtu yuko mbinguni, peponi kwa Baba yake!, yuko na Baba yake!.

Hapa simaanishi kuwa JPM yuko peponi kwasababu he is perfect kama malaika, no!. JPM was a human being hivyo he is not perfect and no one is perfect, kilichofanya hiyo sauti ni despite his human mistakes JPM alitubu kabla ya umauti na kusamehewa dhambi zake zote na makosa yake yote, na ndio maana nimeambiwa, sasa he is in heaven now!.

Kwa bandiko hili, sasa ningewaomba watu humu, kutoendelea kumsakama, kumshutumu, kumsimanga na kuendelea kumsema vibaya, na badala yake tumwache apumzike kwa amani. Kama Mungu mwenyewe amemsamehe na kumuita kwake, who are you kuendelea kumsema sema vibaya?

Mungu Ibariki Tanzania

Paskali
 
PASKALI nimesoma andiko lako kwa tafakuri kubwa sana! Unaweza kuwa sahihi kwa sauti yako ya ndani ambayo iko juu ya uwezo wako kuweza kui control.. Lakini tukija kwenye uhalisia wa maandiko kwa imani ya mhusika ni kwamba wafu bado hawajafika peponi bali wote wako kaburini wakisubiri kiama ama mwisho wa dunia ambapo kila mtu atapewa hesabu yake
Niliwahi kuandika hapa kwamba zana ya pepo/peponi na Jehanum kuzimu iko pale kaburini, kwamba wale waliotenda mema roho zao ziko pale zimelala kwa utulivu lakini wale waliotenda mabaya (kwa tafsiri yoyote ya ubaya) roho zao zinahamanika na kuhangaika huko na huko, hiyo ndio tafsiri ya kuzimu/jehanum

Kwa upande wa karma.. Hii sote tunajua haikopeshi.. Tendo kwa tendo ..ubaya kwa ubaya na wema kwa wema.. Hivyo inategemea nani anaamini kwenye nini ndio atamuweka mhusika huko..

Kuna hili la mizania ya haki.. Hili hupimwa kwa matendo ya mtu mabaya na mazuri..Asili ndio huhukumu., hapa si dini bali ni asili, asili itakuchagulia njia yako kutokana na maisha uliyoishi kabla ya kifo

Hapa kuna ishu ya uumbaji ambayo kupitia mikono yake kwa tafsiri yoyote ile uumbaji huo uliumia, uliteseka na pengine kudhulumiwa haki ya kuishi.. Hapa ishu ni zile sauti zinazolia na kusononeka kwa namna yoyote ile.. Hapa ndio muunganiko wa mizania ya haki na asili hutokea... Kuna vitu viwili ambavyo kiimani vinapaswa kutendewa kwa tahadhari kubwa mno navyo ni uumbaji/uhai na ardhi.. Kwa waamini vitu hivi tumeonywa tusivichezee..!

LA mwisho ni hili la kuonya wadau wasiendelee kumsakama marehemu kwakuwa tayari alishafanya kitubio na yuko peponi..brother sidhani kama maneno yao yatakuwa na athari zozote kwenye hili.. Japo sasa kama ni kweli bado hata baada ya kufa watu wanaendelea kumsema vibaya basi lazima tutambue kuna tatizo kubwa mahali kuhusiana na yeye..!
Mshana Jr leo umeongea kama mtumish wa Mungu aliyepakwa mafuta. Ukiamua kujikita kusoma zaidi Biblia na kuifafanua unaweza ukawa mtumishi mzuri sana kuliko zile thread za ushirikina.

Mungu akupe neema yake.
 
Back
Top Bottom