VPL leo tar. 21/04/2015: Yanga vs Stand United

Stend united mmetangulia tu,
tutawakuta na kuwaacha hapo hapo mlipo.
 
Asanteni Stand United.. Waongezeni kingine.
 
Goooooooa!!
Amiss tambwe.
Yanga 1-1 stand
 
... wazee wa kucheza ndondo ili kudunduliza pesa za kulipa posho wachezaji
Ndio akili za wabongo zilipoishia, wanadhani mfadhili atakuwa anatoa hela siku zote tu. Mpira ni uwekezaji, na uwekezaji unahitaji fedha nyingi. Bila vilabu kutumia potential zilizopo (washabiki) katika kuingiza mapato, tutaendelea kutegemea wafadhili tena wasiotabirika. Mwaka jana Yanga walilazimika kumpigia magoti tajiri mmoja aendelee kuwa kiongozi ili awe karibu na timu.

Wenzetu akina TP Mazembe na akina Etoile walifanya hivi; walikusanya vyanzo vya mapato (wafadhili, viingilio, wadhamini, mikopo) wakawekeza katika kusajili na kuandaa wachezaji bora kabisa kutoka pande mbalimbali za Afrika. Timu zao zikaanza kuingia nane bora, wakati mwingine nne bora, halafu mabingwa. Ukiingia nane bora kwenda juu unapata ruzuku ya mamilioni ya CAF. Ukiingia mara nne mfululizo unakuwa na hela za kutosha kusajili kwa kiwango kile kile kwa kutumia hela za CAF na wadhamini bila ya kutegemea vyanzo vya wafadhili na viingilio. Kuanzia hapo klabu inakuwa inajiendesha kwa faida na si rahisi kuporomoka tena kwani inakuwa na hela za kusajili akina Samata na akina Frank Kom.

Lakini kwa Yanga, mawazo yote ya hela yanaangukia kwa mfadhili, na bahati mbaya mara zote timu inatolewa raundi ya kwanza!
 
Yanga daima mbele, nyuma mikia.

Yanga wabugize magoli, wapiga debe hao wa Stand. Ubingwa uleeeeeeeeee
#teamyanga #
 
Kuna goli zinakuja kwa stend united.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…