Chagu wa Malunde
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 8,734
- 5,750
Msema kweli wahenga walisema ni mpenzi wa Mungu. Chadema imekuwa na kasumba mbaya sana ya kuendesha siasa. Imekuwa na tabia ya kuendekeza vurugu na na hili sio jambo jema.
Ikumbukwe kuwa watanzania ni watu wastaarabu na watu waliozoea amani. Na misingi hii ya kuishi kwa ustarabu na amani ndio imelifikisha hapa hili taifa letu. Ndio maana tunashuhudia nchi ikipata maendeleo.
Kabla ya Dk Slaa kuondoka Chadema kwa kweli hiki chama kilikuwa na misingi mizuri sana ya kufanya shughuli za siasa. Hata alipokuwa akitoa hotuba zake mara nyingi umma uliokuwa ukimsikiliza ulikuwa ukipata jazba na mihemuko, lakini alikuwa akiwatuliza.
Maana hizo zilikuwa ni nyakati ambazo watanzania walikuwa wanapandwa na jazba kiasi cha kutaka kuponda mawe magari ya serikali pale walipo kuwa wakisikia jinsi nchi yao ilivyokuwa inaibiwa. Lakini mara kwa mara Dk Slaa alikuwa akiwatuliza na kuendelea kumwaga sera za chama na kuiumbua CCM iliyokuwa imeteleza kidogo na kuharibu nchi.
Ameobdoka Dk Slaa CHADEMA imekuwa chama cha kihuni na wapenda vurugu. Kampeni zao zimekuwa za kulalama tu na kutukana viongozi. Kampeni zao zimekuwa za kufukuza na kuwafanyia vurugu waandishi wa habari. Na hili hawajaanza mwaka huu.
Hata mwaka 2015 walimfanyia vurugu aliyekuwa nguli wa habari Marin Hassaan (RIP) wa TBC. Mwaka huu wamerudia yale yale tena kwa makusudi bila sababu za msingi.
Mwenyekiti wa CHADEMA bila aibu anajitetea kwa kuigiza eti alikuwa driven na umati? Mbona akina Dk Slaa walikuwa hawawi driven na umati? Pamoja na kuwa kipindi hicho watu walikuwa na hasira na mihemuko ya hali ya juu! Ukweli ni kuwa CHADEMA ni chama ambacho kimekuwa na asili ya vurugu na viashiria vya kuchafua amani ya nchi yetu.
Na kwa mantiki hii adhabu wanayostahili ni kupigwa kwenye box la kura hata diwani mmoja wasipate. Maana dalili ya mvua ni mawingu na huko mbele watatuharibia nchi yetu.
Ikumbukwe kuwa watanzania ni watu wastaarabu na watu waliozoea amani. Na misingi hii ya kuishi kwa ustarabu na amani ndio imelifikisha hapa hili taifa letu. Ndio maana tunashuhudia nchi ikipata maendeleo.
Kabla ya Dk Slaa kuondoka Chadema kwa kweli hiki chama kilikuwa na misingi mizuri sana ya kufanya shughuli za siasa. Hata alipokuwa akitoa hotuba zake mara nyingi umma uliokuwa ukimsikiliza ulikuwa ukipata jazba na mihemuko, lakini alikuwa akiwatuliza.
Maana hizo zilikuwa ni nyakati ambazo watanzania walikuwa wanapandwa na jazba kiasi cha kutaka kuponda mawe magari ya serikali pale walipo kuwa wakisikia jinsi nchi yao ilivyokuwa inaibiwa. Lakini mara kwa mara Dk Slaa alikuwa akiwatuliza na kuendelea kumwaga sera za chama na kuiumbua CCM iliyokuwa imeteleza kidogo na kuharibu nchi.
Ameobdoka Dk Slaa CHADEMA imekuwa chama cha kihuni na wapenda vurugu. Kampeni zao zimekuwa za kulalama tu na kutukana viongozi. Kampeni zao zimekuwa za kufukuza na kuwafanyia vurugu waandishi wa habari. Na hili hawajaanza mwaka huu.
Hata mwaka 2015 walimfanyia vurugu aliyekuwa nguli wa habari Marin Hassaan (RIP) wa TBC. Mwaka huu wamerudia yale yale tena kwa makusudi bila sababu za msingi.
Mwenyekiti wa CHADEMA bila aibu anajitetea kwa kuigiza eti alikuwa driven na umati? Mbona akina Dk Slaa walikuwa hawawi driven na umati? Pamoja na kuwa kipindi hicho watu walikuwa na hasira na mihemuko ya hali ya juu! Ukweli ni kuwa CHADEMA ni chama ambacho kimekuwa na asili ya vurugu na viashiria vya kuchafua amani ya nchi yetu.
Na kwa mantiki hii adhabu wanayostahili ni kupigwa kwenye box la kura hata diwani mmoja wasipate. Maana dalili ya mvua ni mawingu na huko mbele watatuharibia nchi yetu.