Vurugu Umbwe-Lyamungo: Miaka 12 baadae

Vurugu Umbwe-Lyamungo: Miaka 12 baadae

Jamaa walimuulia uwanjani karibu na bweni ka mkapa,. Niliposoma uzi huu nimejikita ninawaza mengi ila mkuu washule wa lyamungo kipindi hicho wandiba alikua mtu wa kuchochea ghasia maana ninakumbuka tulienda pale form 5 tukakuta o,lever wanapiga fimbo usiku kama nn ila wandimba alikua akituelezea komaa nyie ni wakiume. Dah ninatamani tuwasiliane na ww mtoa uzi wenda tuna fahamiana.
 
Ndiyo maana siku hizi watoto wa boarding wanawekewa mafuta ya taa kwenye chakula kwa makusudi kwa sababu inaaminika yana control hormones hizo za testosterone na adrenaline n.k kupunguza munkari.

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Nikikumbuka ni ujinga tu,Tambaza vs Azania....tukapigwa suspension mwaka mzima wa mwaka uliofuata tukaripoti shule za bweni tena za huko mbali kabisa,vijana kibao walishindwa kuendelea na shule,maana shule za karibu zote zilikatazwa kupokea wanafunzi kutoka Tambaza..
 
Jamaa walimuulia uwanjani karibu na bweni ka mkapa,. Niliposoma uzi huu nimejikita ninawaza mengi ila mkuu washule wa lyamungo kipindi hicho wandiba alikua mtu wa kuchochea ghasia maana ninakumbuka tulienda pale form 5 tukakuta o,lever wanapiga fimbo usiku kama nn ila wandimba alikua akituelezea komaa nyie ni wakiume. Dah ninatamani tuwasiliane na ww mtoa uzi wenda tuna fahamiana.
Sure bro yule mkuu wa pale alikuwa mtu fulani hivi wa kiburi..coz hata siku ile anakuja kuongea umbwe akuongea kwa staha.

DM please
 
Tulsimuliwa tulipofika lyamungo kusoma hakika lyamungo walikuwa ni wanajeshi wanaotumia falsafa za sun tuz wa art of war
Siyo kumbu kumbu nzuri sana; Lyamungo ni Jeshi maana hata Stream zilikuwa ni J,K & T badala ya A,B& C mlizizoea kwingine.Mazoezi yake ni Infrequent Soweto na kupakia lorry TX la Mzee Murri kwenda shambani Weruweru.Watu na majembe hupakiwa gari likiwa speed 50-60 km/h without injuries.
Inafikirisha lakini!
 
Way back wakati Niko uboyizini pale mbeya mjini.

Katika mashindano ya umiseta ulizuka mzozo Kati ya camp letu na watoto wa meta .

Kuna mwamba mmoja alikuwa anajiona gangwe kwakuwa ana mbavu Nene Sasa ana akawa anajipitisha mbele ya wanaume huku kapigilia pafyuma kavaa kitozi nyangema huku analeta Maneno mbofu mbofu.

Wana walimvumilia Ila wakasanda akatoa Jamaa mmoja nae mbavu Nene Lina makonfidensi Kama yote si unajua wanyakyusa wa tukuyu .

Akamtandika na mnyororo kichwani Jamaa damu hizi
Halafu msela akawa kajificha hamjui Nani kamchabanga na mnyororo kichwani .

Akaanza panic pale anataka kupigana na asie mjua

Walimu wake wakamtuliza Ila wapi eti akataka kuwachenjia walimu [emoji1787].

Like tukio na mengine nadhani yaliwapa warning watoto wa shule zingine pale mbeya kwamba "mkienda uboyizini kuweni wapole la sivyo mtapigwa"
 
Leo nimeamka na kuwaza kwa machungu sana na maumivu moyoni nikikumbuka vurugu zilizotokea kati ya shule niliyokuwa nasoma Umbwe Sec na Lyamungo Sec August 2009, vurugu zilizoacha vifo, majeraha na uharibifu. Shule mbili zilizopo katika wilaya mbili tofauti (Moshi Vijijini na Hai), zilizopo katika jamii mbili tofauti za wachaga zilizokuwa na mgogoro miaka ya nyuma (Wakibosho na Wamachame), Umbwe sec ikiwa na idadi kubwa ya vijana kutoka Arusha, Kilimanjaro, Singida, Manyara, kanda ya juu kusini, kanda ya ziwa kwa uchache ...Wakati Lyamungo ikiwa na idadi kubwa ya vijana kutoka Mara, mikoa mengine ya kanda ya ziwa, Arusha, Manyara Kilimajaro kwa uchache

Mzozo ulianza Umbwe Sec tulipoenda kucheza mechi na Lyaskika, shule ya kata iliyopo karibu na Lyamungo. Vijana wa Lyamungo walikuja kuishangilia shule ya lyaskika, wakiwa kwa uchache, kulianza mvutano wa maneno kati ya vijana Lyamungo na Umbwe. Kutokana na wingi wao, Vijana wa Umbwe waliweza kuwapelekesha vijana wa Lyamungo. Vijana wa Lyamungo waka-organize na kurudi shuleni kwao ambapo walienda kuwakusanya wenzao waliobaki shuleni na kurudi uwanjani wakiwa na mafyekeo, fimbo..etc. Walikuja kwa kwasi sana wakiwa na silaha. Hii ilwapelekea vijana wa Umbwe kukimbia hoe hae, wengine kwenye mashamba ya mahindi na coffee. Wachache waliweza kufikiana na kuanza kupigana huku vijana wa Lyamungo wakiwa na advantage kutokana na silaha zao. Katika harakati za mapigamo, kijana mmoja wa Lyamongo alizungushiwa waya ya senyenge shingoni na vijana wa Umbwe na kuivutia shingoni hadi ikatoka na nyama za shingoni.

Vijana wa Umbwe kwa kukimbia waliweza kurudi shuleni, tukiwa katika jaziba na hofu kuwa vijana wa Lyamungo wanaweza kurudi, wale ma-brother wakubwa walitupangia mawindo ya usiku kwa makundi kila kona ya shule. Na story kubwa iliyokuwepo ni kuwa ikifika asubuhi na mapema tunatakiwa kwenda kuwavamia Lyamungo shuleni kwao. Asubuhi ilifika kila mtu akiwa na silaha, tukiwa tumevalimia vitambaa vyeupe kichwani ili tutambuane na kupeane code names ili tusiweze kushambuliana kimakosa. Tukaanza safari, nakumbuka tulipita sehemu na mama mmoja alikuwa akipalilia shambani akaanza kulia na kutuomba tusiende ila vijana hatukuelewa tukazidi kwenda.

Tulipofika shuleni Lyamungo tukaingia kwa kasi sana na kuanza kuwashambulia vijana wa Lyamungo na kuharibu miundombinu yao. Nakumbuka kuna jamaa alikuwa akitumia kombeo alimlenga kichwani jamaa mmoja aiyekuwa ana piga mswaki dirishani. Tulifanya shambulizi kwa kasi sana na kurudi shuleni ambapo tulikuta polisi wameshafika shuleni Umbwe na tukakalishwa chini wote. Bila mategemeo wala kudhania, tukapata taarifa kuwa kuna mwanafunzi mwenzetu amefariki kutokana na kupigwa na wanafunzi wa Lyamungo. Maan, my whole world collapsed....baada ya siku kadhaa pia tukapata taarifa kuwa yule mwanafunzi wa Lyamungo aliyezungushiwa waya ya senyenge shingoni amefariki dunia.

Zile nyakati ni moja ya kati vitu vigumu vilivyowahi kutokea maishani mwangu. Nikikumbuka jinsi yule mama wa yule kijana aliyefariki alivyofika shuleni na kuanza kuangua kilio pale administration block, huwa naumia sana. Nikimfikiria kijana wa lyamungo aliyezungushia senyenge na baadae kufariki naumia pia. Nafikiria zaidi kuhusu familia zao, mategemeo waliyokuwa nayo juu yao.

12 years later, bado moyo wangu ni mzito, kama bado haukuwahi ku-experience vita usiombe iweze kutokea katika mazingira yako.

May the Lord grant us his Mercy.

View attachment 1824561
Dah aisee umenikumbusha mbali sana kipindi hicho nilikua form 3. Ila kuweka kumbukumbu vizuri hiyo ilitokea 26 May 2009 na siyo August. Na kuhusu huyo aliyezungushiwa seng'enge sidhani kama alifariki maana tungetangaziwa shuleni. Nakumbuka huyo mwanafunzi wa Umbwe aliyefariki alipigwa kama mwizi uwanja A pale. Na hiyo siku ilibidi tukeshe tukiwasubiria Umbwe waje. Dah ile siku ilikua kama jeshi sipatii picha Umbwe wangekuja usiku ule ingekuaje maana tulijiandaa kama jeshi. Tulikusanya mawe, mafyekeo na mipini. Tulijigawa magroup matatu geti kubwa, geti dogo na katikati ya uwanja. Yaana nia ilikua Umbwe wakitokea sehemu yoyote wanapigika na tulipeana signature kabisa ukiulizwa "Nyeto" unajibu "Ujinga" ukishindwa kujibu unakula kichapo maana utakua sio wa Lyamungo. Dah sitaisahau ile siku, ni stori ndefu kwa kweli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndiyo maana siku hizi watoto wa boarding wanawekewa mafuta ya taa kwenye chakula kwa makusudi kwa sababu inaaminika yana control hormones hizo za testosterone na adrenaline n.k kupunguza munkari.

Everyday is Saturday............................... 😎
Wakati tupo uboyzini kwenye school baraza,

Hoja ilitolewa na mwanafunzi,

Mwalimu wa biology atoke mbele aje athibitishe kitaam,

Kitu gani aambacho kipo kwenye mafuta ya taa Ni kwa namna gani kinaweza kucontrol hiyo mihemko

Ilishindikana,

Mwishowe uo utaratibu wa kuwekewa mafuta ya taa kwenye vyakula ukafutwa rasmi
 
Back
Top Bottom