beny jr
JF-Expert Member
- Jul 15, 2018
- 849
- 1,168
DaaahHow would you feel.
Not How will you feel.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
DaaahHow would you feel.
Not How will you feel.
Musoma Tech na Boda Boda 2011. Tuliweka lindo Uwanjani karibu na Mutex kuwasubiri bodaboda waje.
Unaongea sana kwa ufahari wakati ni upumbavu unao dhania, hakuna cha kujivunia kwenye ujinga ule, yule jamaa wa senyenge alifariki dunia na kiongozi kutoka shule alienda kushiriki kwenye msiba, very sad hizi shule zimetuathiri maisha na kuwa wajinga hiviDah aisee umenikumbusha mbali sana kipindi hicho nilikua form 3. Ila kuweka kumbukumbu vizuri hiyo ilitokea 26 May 2009 na siyo August. Na kuhusu huyo aliyezungushiwa seng'enge sidhani kama alifariki maana tungetangaziwa shuleni. Nakumbuka huyo mwanafunzi wa Umbwe aliyefariki alipigwa kama mwizi uwanja A pale. Na hiyo siku ilibidi tukeshe tukiwasubiria Umbwe waje. Dah ile siku ilikua kama jeshi sipatii picha Umbwe wangekuja usiku ule ingekuaje maana tulijiandaa kama jeshi. Tulikusanya mawe, mafyekeo na mipini. Tulijigawa magroup matatu geti kubwa, geti dogo na katikati ya uwanja. Yaana nia ilikua Umbwe wakitokea sehemu yoyote wanapigika na tulipeana signature kabisa ukiulizwa "Nyeto" unajibu "Ujinga" ukishindwa kujibu unakula kichapo maana utakua sio wa Lyamungo. Dah sitaisahau ile siku, ni stori ndefu kwa kweli.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mwanafunzi analazwa polisi analazwa.....Naikumbuka KIBITI.... Hizi shule dahhhh
Miaka 12 baadae bado una uumbwe na ulyamongo..very stupid of youYap, alijikuta captain akaendelea kurusha mawe watu wakaanza kumkimbiza akafika uwanjani alipigwa mtama hapo ikawa kila aliyemkuta anapiga sio mwenye fyekeo, mwenye mpini, mwenye jiwe, wengine walimkanyaga dah so sad mpaka akakata kamba. Kuna mwenzake nae alikimbilia nyumbani kwa mpishi alichomolewa akaletwa pembeni ya mwenzake. Nae alikula kichapo ila wakamuonea huruma. Akapelekwa KCMC ila nadhani alipona. Na kama alipona nadhani alipata kilema cha maisha.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hahha kiLe kituo nshawahi lala mule.... Japo tulisingiziwaMwanafunzi analazwa polisi analazwa.....
Kibiti boizi🙌🙌🙌
Sio kwa ufahari mkuu mimi kama mimi nilibaki nimeduwaa maana iliniathiri mpaka baadhi ya walioshiriki nilikua nawaogopa.Unaongea sana kwa ufahari, hakuna cha kujivunia kwenye ujinga ule, yule jamaa wa senyenge alifariki dunia na kiongozi kutoka shule alienda kushiriki, very sad hizi shule zimetuathiri maisha na kuwa wajinga hivi
Hivi unadhani hao walioshiriki kumuua yule kijana kwa sasa hawana Guilty mioyoni mwao, hata kama alishiriki kupiga teke, itakaa moyoni mwake milele...
Sasa ukweli si ndo huo mkuu mbona kama umepaniki? Pia kuna washkaji kibao waliumia nashukuru Mungu sikupata hata jeraha. Kuna marafiki zangu kibao wana makovu mpaka leo. Na je? Wewe uliona ni sahihi kuja shuleni kufanya fujo? Nadhani uliona maamuzi yaliyotolewa. Nyie mlilipa faini ya uharibifu tsh.53,000/= sisi hatukulipa hata mia.Miaka 12 baadae bado una uumbwe na ulyamongo..very stupid of you
Fikiria wewe ni ndugu wa yule jamaa aliekufa alafu unasoma comment ya kijinga kama hii
Kweli unasema alijikuta captain, kweli marehemu, miaka 12 baadae bado unapumba za uboizini
Siyo kumbu kumbu nzuri sana; Lyamungo ni Jeshi maana hata Stream zilikuwa ni J,K & T badala ya A,B& C mlizizoea kwingine.Mazoezi yake ni Infrequent Soweto na kupakia lorry TX la Mzee Murri kwenda shambani Weruweru.Watu na majembe hupakiwa gari likiwa speed 50-60 km/h without injuries.
Inafikirisha lakini!
Sure mkuu hii kitu inaniuma sana..Sio kwa ufahari mkuu mimi kama mimi nilibaki nimeduwaa maana iliniathiri mpaka baadhi ya walioshiriki nilikua nawaogopa.
Sent using Jamii Forums mobile app
Haha maji bariiid kama nn alafu nikapelekwa gwatanamo bweni likikua karibu na tacr mh mbona nilitaman kurud hom!Ahaa haaa bila shaka nilikuogesha kwenye ule mfereji uliopita kati ya uwanja na mabweni [emoji1787][emoji1787][emoji1787]. Yaani akili za kitoto bhana. Ilikua principle form five wakishareport tunawamsha kuwakaribisha uboyzini.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ofcos nimepanic mpumbavu ww..Sasa ukweli si ndo huo mkuu mbona kama umepaniki? Pia kuna washkaji kibao waliumia nashukuru Mungu sikupata hata jeraha. Kuna marafiki zangu kibao wana makovu mpaka leo. Na je? Wewe uliona ni sahihi kuja shuleni kufanya fujo? Nadhani uliona maamuzi yaliyotolewa. Nyie mlilipa faini ya uharibifu tsh.53,000/= sisi hatukulipa hata mia.
Sent using Jamii Forums mobile app
Tuliza munkari broo. Umeshakua mtu mzima wewe. Yaliyopita yameshapita either bad or good memories.Ofcos nimepanic mpumbavu ww..
Sijaandika hapa kujivunia na chochote umbwe walichofanya zidi ya lyamungo..
Angalia sasa unavyozidi na ujinga wako , eti nyie mlilipa fine na sisi hatukulipa, mjinga sana wewe hauhitaji reply yoyote ile..jibu chochote unachojua ili tambua wewe ni mentally retarded..yani baada ya miaka 12 bado unachagua upande.. manina
Pole mkuu yale maji unaganda, ilikua ukijifanya kuwatetea na wewe unachanganywa huko. [emoji3][emoji3][emoji3]Haha maji bariiid kama nn alafu nikapelekwa gwatanamo bweni likikua karibu na tacr mh mbona nilitaman kurud hom!
Jamaa wa Lyamungo walikuwa informed kuwa umbwe watakuja usiku ko walichofanya ni kujificha kweny mashamba ya kahawa wakiwa na slashers,wanafunz wa umbwe walitekwa na kuingizwa ndan ya gate na hapo ndo kichapo kilianza,yulr jamaa alieuawa alionekana ni mvuta bangi sanaa na aligoma kuchwapwa slasher ya mat..n ambayo kwa muda huo ilikuwa kama passward ya kuingia ndan ya gate ..nawahurumiwa sanaa wazaz wa jamanaa cz walimtuma akasome ila yy akawa ndo organizer wa fujoLeo nimeamka na kuwaza kwa machungu sana na maumivu moyoni nikikumbuka vurugu zilizotokea kati ya shule niliyokuwa nasoma Umbwe Sec na Lyamungo Sec August 2009, vurugu zilizoacha vifo, majeraha na uharibifu. Shule mbili zilizopo katika wilaya mbili tofauti (Moshi Vijijini na Hai), zilizopo katika jamii mbili tofauti za wachaga zilizokuwa na mgogoro miaka ya nyuma (Wakibosho na Wamachame), Umbwe sec ikiwa na idadi kubwa ya vijana kutoka Arusha, Kilimanjaro, Singida, Manyara, kanda ya juu kusini, kanda ya ziwa kwa uchache ...Wakati Lyamungo ikiwa na idadi kubwa ya vijana kutoka Mara, mikoa mengine ya kanda ya ziwa, Arusha, Manyara Kilimajaro kwa uchache
Mzozo ulianza Umbwe Sec tulipoenda kucheza mechi na Lyaskika, shule ya kata iliyopo karibu na Lyamungo. Vijana wa Lyamungo walikuja kuishangilia shule ya lyaskika, wakiwa kwa uchache, kulianza mvutano wa maneno kati ya vijana Lyamungo na Umbwe. Kutokana na wingi wao, Vijana wa Umbwe waliweza kuwapelekesha vijana wa Lyamungo. Vijana wa Lyamungo waka-organize na kurudi shuleni kwao ambapo walienda kuwakusanya wenzao waliobaki shuleni na kurudi uwanjani wakiwa na mafyekeo, fimbo..etc. Walikuja kwa kwasi sana wakiwa na silaha. Hii ilwapelekea vijana wa Umbwe kukimbia hoe hae, wengine kwenye mashamba ya mahindi na coffee. Wachache waliweza kufikiana na kuanza kupigana huku vijana wa Lyamungo wakiwa na advantage kutokana na silaha zao. Katika harakati za mapigamo, kijana mmoja wa Lyamongo alizungushiwa waya ya senyenge shingoni na vijana wa Umbwe na kuivutia shingoni hadi ikatoka na nyama za shingoni.
Vijana wa Umbwe kwa kukimbia waliweza kurudi shuleni, tukiwa katika jaziba na hofu kuwa vijana wa Lyamungo wanaweza kurudi, wale ma-brother wakubwa walitupangia mawindo ya usiku kwa makundi kila kona ya shule. Na story kubwa iliyokuwepo ni kuwa ikifika asubuhi na mapema tunatakiwa kwenda kuwavamia Lyamungo shuleni kwao. Asubuhi ilifika kila mtu akiwa na silaha, tukiwa tumevalimia vitambaa vyeupe kichwani ili tutambuane na kupeane code names ili tusiweze kushambuliana kimakosa. Tukaanza safari, nakumbuka tulipita sehemu na mama mmoja alikuwa akipalilia shambani akaanza kulia na kutuomba tusiende ila vijana hatukuelewa tukazidi kwenda.
Tulipofika shuleni Lyamungo tukaingia kwa kasi sana na kuanza kuwashambulia vijana wa Lyamungo na kuharibu miundombinu yao. Nakumbuka kuna jamaa alikuwa akitumia kombeo alimlenga kichwani jamaa mmoja aiyekuwa ana piga mswaki dirishani. Tulifanya shambulizi kwa kasi sana na kurudi shuleni ambapo tulikuta polisi wameshafika shuleni Umbwe na tukakalishwa chini wote. Bila mategemeo wala kudhania, tukapata taarifa kuwa kuna mwanafunzi mwenzetu amefariki kutokana na kupigwa na wanafunzi wa Lyamungo. Maan, my whole world collapsed....baada ya siku kadhaa pia tukapata taarifa kuwa yule mwanafunzi wa Lyamungo aliyezungushiwa waya ya senyenge shingoni amefariki dunia.
Zile nyakati ni moja ya kati vitu vigumu vilivyowahi kutokea maishani mwangu. Nikikumbuka jinsi yule mama wa yule kijana aliyefariki alivyofika shuleni na kuanza kuangua kilio pale administration block, huwa naumia sana. Nikimfikiria kijana wa lyamungo aliyezungushia senyenge na baadae kufariki naumia pia. Nafikiria zaidi kuhusu familia zao, mategemeo waliyokuwa nayo juu yao.
12 years later, bado moyo wangu ni mzito, kama bado haukuwahi ku-experience vita usiombe iweze kutokea katika mazingira yako.
May the Lord grant us his Mercy.
View attachment 1824561
Yaan alipigwa na kila kitu unachokijua ww,daah!ila roho za wanafunz wa bweni nazo ni za kibandidu sanaaKuna jamaa alisimulia jinsi uyo mchizi wa umbwe alivyuouawa, aisee ni mateso makali jamaa alipitia.