Vurugu za Bungeni: Tundu Lissu, Anastahili Adhabu Kali?!. Ni Mtundu Toka Shule!.

Vurugu za Bungeni: Tundu Lissu, Anastahili Adhabu Kali?!. Ni Mtundu Toka Shule!.

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,

Juzi katika kikao cha bunge, Spika wa Bunge, Mhe. Anne Maklnda, alimtaja Mbunge wa Singida, Mhe. Tundu kama ndie Mbunge anayeongoza kuwa chanzo cha vurugu za bungeni, kwa kuongoza kwa utovu wa nidhamu, kuleta fujo na vurugu mbalimbali za bungeni, hali ambayo sio tuu inahatarisha hali ya usalama, utulivu na amani bungeni, bali pia kumevuruga hadi baadhi ya ratiba za Bunge kulikopelekea Spika kufuta ratiba za Bunge ambazo zilikwisha ridhiwa na kuingizwa kwenye Order Paper ikiwemo kupokea hoja binafsi za wabunge, kwa kilichoelezwa kuepuka vurugu zaidi!.

Jana kikao cha kamati ya Uongozi kimekaa kujadili hali ya usalama Bungeni na matokeo yake, tutayapata kesho asubuhi baada ya kipindi cha maswali na majibu ya papo kwa papo kwa PM!, ni hakika rungu la kiti, lazima litamshukia Mhe. Tundu Lissu!.

Swali la kwanza ambalo wengi mtapenda kujiuliza ni, ni jee ni kweli, Mhe. Tundu ni mtundu na ndie chanzo cha utovu wote wa nidhamu wa bunge hili la kumi kama anavyoelezwa na Madam Speaker?!, au huo utundu wa Mhe. Tundu, sio utundu bali ni kusimamia haki na uzingatiaji wa kanuni za uendeshaji wa Bunge kwa haki, kufuatia Madam Speaker kuonyesha udhaifu mkubwa katika kuliendesha Bunge kwa kutokuzingatia, sheria, taratibu na Kanuni?!.

Kwa vile mimi ni mmoja wa watu tunaomfahamu vizuri Mhe. Tundu, tangu zamani tukiwa shuleni, Ilboru (sio darasa moja, mimi nikiwa A-level, yeye alikuwa O-Level) naomba kuchukua fursa hii kumfariji Mhe. Spika, kwa kumshauri na kumuomba asiumize sana kichwa chake kuendelea kubishana na Mhe. Tundu Lissu kuhusu kanuni za Bunge, ni kujipotezea tuu muda wake bure kwa kubishana na Lissu kwa kitu ambacho Lissu ana uhakika nacho 100/100!. Nashauri wala Bunge wasipoteze muda na kujisumbua kumuadhibu kwa jambo ambalo liko wazi kabisa watu wote wenye macho tunduizi tunaona wazi ni wapi udhaifu wa uendeshaji wa Bunge letu ulipo, sababu za udhaifu huo zinajulikana tangu chanzo chake, ulipo sasa na labda utaendelea kuwepo, hivyo hata Lissu akiadhibiwa vipi, kwa sababu Mhe. huyu ni mbishi hakuna mfano!, haswa pale anapokuwa na uhakika kuwa yuko right!.

Nashauri Mhe. Spika, lazima ufike mahali, umkubali huyu jamaa hivyo hivyo jinsi alivyo na lile jina lake la Tundu, sio jina tuu la kupewa, bali huyu bwana analiishi jina lake kwa kuwa ni mtundu kweli!, na haswa pale anapogundua kuwa katiba, sheria, taratibu na kanuni zinakiukwa na zinapopindishwa ili kufavour na kutoa mteremko kwa upande fulani mule Bungeni.

Nimebahatika kusoma na Mhe. Lissu shule moja kule Ilboru, (sio darasa moja) miaka hiyo enzi za Mkuu mmoja wa shule aitwae Mwalimu Mushi, kwa jina la utani, tulimuita Bino!. Huyu Bino alikuwa ni Mwalimu Mkuu bingwa wa nidhamu, ila kwa Tundu Lissu, alinyanyua mikono juu na kisha kuishusha chini, baada ya kuthibitika kuwa japo Tundu Lissu shuleni alikuwa "toto tundu", ila pia ndie aliyekuwa kipanga wa darasa lake!, kwani pepa alikuwa akizifumua, utadhani mtihani katunga yeye!.

Tundu Lissu alijiunga shule ya vipaji ya Ilboru akitokea Singida, wakati huo shuleni akiitwa Antipasi Tundu, na alikuwa ni mtoto mtundu kweli!. Wakati huo, O-Level ya Ilboru ilichukua wanafunz vichwa tupu wenyeji wa Arusha, Singida na Shinyanga!. Sisi Wasukuma tukiitwa "Wasukusu", wenyeji wakiitwa "wamenye" huku jamaa wa Singida wakijiita watu wa "Singapore", A-Level wakichukua vipanga wenye Div 1 kali, enzo hizo uji ukiitwa "sumu", na nje kulikuwa na kaduka kwa "Akwii".

Utundu wa Tundu Lissu ulkikuwa ni kwenye mishe mishe tuu hizi za zile, haijulikani alikuwa akisoma muda gani, ila pepa zikija, anafumua ile mbaya kama mitihani katunga yeye!, hivyo huyu jamaa ni kichwa, very bright and na very intelligent upstairs!.

Moja ya maeneo ambayo Tundu Lissu alikuwa ni mtundu au tusema ni mbishi, ni kwenye school debate!. Tundu Lissu alikuwa Bingwa wa school debate, akishakuwa na uhakika yuko right and on the right side and on the right track, ni mbishi hakuna mfano!.

Hata mimi nami sikuwa malaika, nilikuwa na matatizo yangu tangu shule, yale matatizo ya kawaida ya watu wa Kanda ya Ziwa, sisi Wasukuma wa Chapa Ng'ombe, tukiongoza, unapokutana bidhaa adimu za kumwaga!, vile vibinti vya vyeupe vya Kiarusha pale Mlimani Ilboru, ukigusa tuu...!, ukijumlisha na lile baridi kali la Ilboru , tena wakati huo, "bwawa bado halijaingia luba!'...

Tundu Lissu aliondoka Ilboru na Div. 1 kali ya point 7!, akaenda Galanos huko nako akafumua Div. 1 ya point 3!, na hatimaye kujiunga UDSM alikofumua upper 2nd Class (inasemekana alipata 1st class Ila wakambania). Sisi na vilaza wengine tukaishia kwenye vile vyuo vya mashenzini!.

Tulipoteana kwa kipindi cha takriban miaka 10!, tulikuja kukutana tena jijini Atlanta, nchini Marekani, yeye akiwa na yake nami nikiwa na yangu, ndipo akanieleza sasa yuko LEAT, na huko aliichachafya serikali vivyo hivyo kama anavyo mchachafya Madame Spika, kwa kumsulubu bila huruma!.

Pamoja na utundu wote huu wa Mhe. Tundu Lissu, kiukweli kabisa this guy is dam good upstairs tangu academically akiwa shule na kwa kujenga hoja akiwa wakili na hadi sasa mule Bungeni.

Hivyo wakati tukisubiria kusikia ni adhabu gani itamfika Lissu hapo kesho, kuna maswali matatu tujiulize!.
  1. Jee ni kweli Mhe. Tundu Lissu ni mtundu kihivyo na ndie mbunge anayeongoza kwa utovu wa nidhamu hadi kustahili adhabu kali?.
  2. Au ni Spika ndiye Spika dhaifu hadi kushindwa kulisimamia Bunge kwa kanuni, kuliendesha Bunge kwa haki hivyo Tundu Lissu akisisitiza kufuatwa kwa Sheria taratibu na kanuni, anaonekana kama analeta vurugu?.
  3. Baada ya kuthibitisha, Mhe. Tundu Lissu alikuwa ni mtundu toka shuleni, jee nani wa kubadilika kati ya Mhe Tundu Lissu na wabunge wa upinzani, yaani wakae kimya wakati sheria, taratibu na kanuni za Bunge, zikikiukwa, na kupindishwa?,
  4. Au Mhe. Spika ndie abadilike na kukuendeshea Bunge kwa mujibu wa kanuni na sio kujiendeshea Bunge kwa kuliburuza atakavyo, ili tuu kudumisha utii, na nidhamu ili Bunge liwe la amani?,
  5. My Take: It's about time, wakuu wa Bunge ndio wabadilike baada ya kugundua mule Bungeni wameingia wabunge vichwa makini wanaojua katiba, sheria, taratibu na kanuni, hivyo sio watu wa kupelekwa pelekwa!. Huwezi kuwaburuza kibwege bwege, hivyo lazima wabadilike na waliendeshe Bunge kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni kwa kutoa haki na usawa kwa wote, kwa vyama vyote, hivyo kupatikana kwa amani ya kweli ya kudumu mule Bungeni.
  6. Akifanya hivyo Mhe Madam Spika, atawathibitishia Watanzania kuwa hata yeye, japo ni Spika wa majaribio ya "jinsia" ,"ameweza" kuliendesha Bunge vizuri tuu, ambalo ni mhimili mmoja wa dola, hivyo 2015, hivyo kuuthibisha wanawake wakiwezeshwa, wanaweza, hivyo tunaweza kuendelea na majaribio ya "jinsia" kwa mihimili miwili iliyobakia, ili nchi yetu iwe ni nchi ya usawa halisi wa kijinsia.
Wasalaam

Paskali
(Skulu Meti wa Toto T).
 
Wanabodi,

Nashauri Mhe. Spika, lazima ufike mahali, umkubali huyu jamaa kuwa lile jina lake la Tundu, sio jina tuu, huyu bwana analiishi jina lake kwa kuwa ni mtundu kweli pale kanuni zinapopindishwa ili kutoa mteremko kwa upande fulani!.

Pasco.
(Skulu Meti wa Toto T).

Je Makinda naye ni Kinda bado katika uendeshaji wa shughuli za Bunge ?
 
Nadhani bunge letu ni la kistaarabu sana kulinganisha na bunge kama la uingereza, mi nadhani tunahitaji wabunge wanaozijua kanuni na kuzisimamia kama anavyofanya tundu lissu kwa sabbu itasaidia kuwafanya maspika kuwa na nidhamu katika uendeshaji wa bunge kwa kuhofia mabishano na mapambano yatayokayojitokeza endapo kutakuwa na upindishwaji wa mambo kwa misingi ya itikadi za vyama kama ilivyo sasa
 
Je Makinda naye ni Kinda bado katika uendeshaji wa shughuli za Bunge ?

Watanzania tuna matatizo ya kukubali na kuwathamini watu wanaotuzidi kiuwezo badala ya kujifunza kutoka kwao tunawaona kama ni maadui hivyo tunashndwa kujifunza. Pasco, nilikuwa napata tabu sana na mwl.wangu wa hesabu shule ya msingi hesabu zilikuwa hazipandi ukimkosoa tu anaamaki na kukuita wewe ni mkorofi yaani acha tu na mbaya zaidi mambo haya yameamia mpaka makazini kuna wakina makinda wengi sana.
 
Mh. Tundu Lisu ananikumbusha mbali! Mwaka 1961 tukiingia Form 1, haikuchukua muda darasa letu, pamoja na kuwa vinyoya, likajulikana kama "siasa kali" (wakati huo hatujapata uhuru). Bahati mbaya wengi wa vipanga darasani walilazimika kuchukua masomo ya sayansi kwani huo uhuru wa kuchagua haukuwapo sana.

Nina hakika mtu kama Tundu Lisu, angesoma wakati huo, labda siasa angeisikia tu kwa mbali...sana sana angeishia kuwa Injinia au dakitari! Linalosikitisha ni kuwa wengi wa viongozi wa baadaye kutoka kundi letu (Wabunge na Mawaziri) ni wale ambao somo la "additional & applied mathematics" walikaa nao mbali kama ukoma. Kweli mambo yalikuja kubadilika!
 
Heshima yako mkuu Pasco.

Nafurahi kusikia kwamba ulisoma vipaji maalum..'special school'.

Nichangie kwenye andiko lako..LEAT sijafahamu ni nini.

Kuhusu Spika: watanzania tunaona lakini viongozi wetu wamejibinafishia hisia zetu, fikra zetu na mapenzi yetu. Wanachoona kwao ni sahihi ndio basi na kwa wananchi kitakuwa ni sahihi tu. Soma signature yangu..they give us what they think we deserve and not what we want (not what we desire to have).

Bunge la sasa limepelekea hata lile kosa la 'kulidanganya Bunge' sasa lionekana halina nguvu kulinganisha na enzi 'mhe. naomba uliza swali..' na enzi za 'standard and speed'.

Hili la mwisho la majaribio ndio umemaliza kabisa. Sumu haionjwi jamani! Hata madaktari wanaanza mafunzo ya upasuaji kwa panya, baadae wanaambatana na madaktari bingwa kabla ya kuruhusiwa kufanya wao wao peke yao. Haya majaribio napendekeza yawe kwenye UWT, viti maalum, Wilaya (DC) hata Mikoa (RC)!


Wanabodi,

Nimebahatika kusoma na Mhe. Lissu shule moja kule Ilboru, (sio darasa moja) miaka hiyo enzi za Mkuu mmoja aitwae Bino!. Huyu Bino alikuwa ni mwalimu mkuu bingwa wa nidhamu, ila kwa Tundu, alinyanyua mikono juu na kwisha kuishusha juu baada ya kuthibitika kuwa japo Tundu alikuwa "toto tundu", ila pia ndie aliyekuwa kipanga wa darasa lake!, kwani pepa alikuwa akizifumua, utadhani mtihani katunga yeye!.

Tundu Lissu alijiunga shule ya vipanga ya Ilboru akitokea Galanos, wakati huo akiitwa Antipasi Tundu, na alikuwa ni mtoto mtundu kweli!. Wakati huo sisi Wasukuma tukiitwa "Wasukusu", wenyeji wakiitwa "wamenye" huku jamaa wa Singida wakijiita watu wa "Singapore", uji ukiitwa "sumu", na nje kulikuwa na duka la kwa "Akwii".

Tulipoteana kwa kipindi cha miaka 10!, tulikuja kukutana tena mjini Atlanta, yeye akiwa na yeke nami na yangu, ndipo akanieleza yuko LEAT, na huko aliichachafya serikali vivyo hivyo kama anavyo mchachafya Madame Spika, kwa kumsubu bila huruma!.

Pamoja na utundu wote huu wa Mhe. Tundu Lissu, wakati tukisubiria kusikia ni adhabu gani itamfika hapo kesho, kuna maswali matatu tujiulize!.
  1. Jee ni kweli Mhe. Tundu Lissu ni mtundu kihivyo na ndio anayeongoza kwa utovu wa nidhamu hadi kustahili adhabu kali?.
  2. Au ni Spika ndiye dhaifu hadi kushindwa kumdhibiti Tundu Lissu na utundu wake?.
  3. Baada ya kuthibitisha, Mhe. Tundu Lissu alikuwa ni mtundu toka shuleni, jee nani wa kubadilika kati ya Mhe Tundu Lissu na wabunge wa upinzani, wakae kimya wakati sheria, taratibu na kanuni, zikikiukwa, na kupindishwa?, hivyo kumpatia fursa Mhe. Spika kujiendeshea bunge anavyotaka, ili kudumisha utii, na nidhamu, bunge liwe la amani?.
  4. Hivyo Mhe Spika kuwathibitishia Watanzania kuwa hata yeye ambaye ni Spika wa majaribio ya "jinsia" "ameweza" kuliendesha bunge vizuri tuu, ambalo ni mhimili mmoja wa dola, hivyo jee, 2015, tukamilishe majaribio ya "jinsia" kwa mihimili miwili iliyobakia?, ili nchi yetu iwe ni nchi ya usawa halisi wa kijinsia?.

Wasalaam

Pasco.
(Skulu Meti wa Toto T).
 
Sijaelewa why tumeamua ku-single out Lissu wakati we alls aw what happened

Kibaya zaidi ni naibu spika kushindwa kuweka wazi kifungu alichotumia in fact hakuna kifungu na mike zilikua zinadaka sauti live anahangaika kuomba kifungu, na kuuliziaulizia

Waanze na yule andunje asiyejua kuongoza bunge wala kanuni

Imagine Ndugai angekua ni pilot hiyo ndege ingetua salama kwa ukosefu wa knowledge ya vifungu?
 
Acha kupotosha watu wewe hujui Tundu ni litobo lililowazi.Halafu mtu mwenyewe anapenda kulialia mnajidai kumsifia

lissu 2.JPG
 
Makinda na Ndugai wapo remoted hata wabunge wa CCM hawana jipya ni mzigo hawa kina Rage na Maji Marefu uwezi fananisha na mtu kama Tundu Lisu
 
Heshima yako mkuu Pasco.

Nafurahi kusikia kwamba ulisoma vipaji maalum..'special school'.

Nichangie kwenye andiko lako..LEAT sijafahamu ni nini.

Kuhusu Spika: watanzania tunaona lakini viongozi wetu wamejibinafishia hisia zetu, fikra zetu na mapenzi yetu. Wanachoona kwao ni sahihi ndio basi na kwa wananchi kitakuwa ni sahihi tu. Soma signature yangu..they give us what they think we deserve and not what we want (not what we desire to have).

Bunge la sasa limepelekea hata lile kosa la 'kulidanganya Bunge' sasa lionekana halina nguvu kulinganisha na enzi 'mhe. naomba uliza swali..' na enzi za 'standard and speed'.

Hili la mwisho la majaribio ndio umemaliza kabisa. Sumu haionjwi jamani! Hata madaktari wanaanza mafunzo ya upasuaji kwa panya, baadae wanaambatana na madaktari bingwa kabla ya kuruhusiwa kufanya wao wao peke yao. Haya majaribio napendekeza yawe kwenye UWT, viti maalum, Wilaya (DC) hata Mikoa (RC)!
Mkuu Mpango, Ilboru ile ilikuwa ya vipanga wa kutoka kwenye umande na sio hii ya sasa ya spoon fed vipanga toka academy!.

Leat ni Chama cha Wanasheria wa Mazingira, wamefight sana ushenzi uliofanywa Loliondo, Yaeda Chini, sumu za Barick kule mto Tigiti na ushenzi mwingine wote tunaofanyiwa kwa jina au la hifadhi, au uwekezaji!.

Kuhusu sisi Watanzania, ni watu watulivu, watu wa upendo na mshikamano, hivyo viongozi wetu wanatutake for granted, hata wakifanya chochote, sisi ni yes man!, kuna wakati sikumbuki ni nchi gani, mkate ulipanda bei by 20%, maandanano nchi nzima, waziri mkuu wa nchi hiyo aling'olewa!. Sisi mtu anakufa mikononi mwa polisi picha zinasema kila kitu na wote wametulia tuu as if nothing happened. 1976 nikiwa mdogo bado, Mzee wangu aliwajibishwa kwa ile kesi ya mauji Mwanza, kuanzia Waziri wa mambo ya ndani na wa usalama, walijiuzulu, IGP, Boss wa TISS, walistaafishwa!, RPC, RSO, OCD, DSO walipandishwa kizimbani!. Leo tangu ile ya Maandamano Arusha, mtu kapigwa risasi stend, polisi wakatengeneza a make belive video kuwa wamewaua watu waliokuja kuvamia kituo cha polisi!, ya Mwangosi ndio usiseme, no one amewajibika as if nothing happened nasi tunawashangilia na 2015, tunawapa term nyingine tena!.

Tatizo sio viongozi wetu, tatizo ni sisi Watanzania, sisi ni mandondocha kabisa!, hatuchagui viongozi kwa sifa kwa sababu hata JK tulipomchagua kwa ile landslide tulimchagua kwa sifa zipi?. Spika Anne aliletwa ili kumkomoa Six awekwe bench ili kutoa fursa ya kumsafisha EL na dodoki litapita 2014!. Eti sifa kuu ni "gender!". Nimeshazisikia fununu kuwa kwa vile kuna mafahali wanapigana vikumbo kuigombania magogoni, kuna sketi nyingine inaandaliwa, ili kumleta a compromised candidate chama kisimegeke!. Ndani ya CCM, 2015 ni zamu ya Zanzibar, Shein is the man!, ila wanahofia wasiitoe magogoni kwa sadakawe kwenye upepo wa M4C!.

Amini nakuambia jinsi tulivyo mandondocha, hiyo 2015, hata tukiletewa sketi nyingine, tutaichagua tuu!, na ni CCM tena!.

Pasco.
 
Mh. Tundu Lisu ananikumbusha mbali! Mwaka 1961 tukiingia Form 1, haikuchukua muda darasa letu, pamoja na kuwa vinyoya, likajulikana kama "siasa kali" (wakati huo hatujapata uhuru). Bahati mbaya wengi wa vipanga darasani walilazimika kuchukua masomo ya sayansi kwani huo uhuru wa kuchagua haukuwapo sana. Nina hakika mtu kama Tundu Lisu, angesoma wakati huo, labda siasa angeisikia tu kwa mbali...sana sana angeishia kuwa Injinia au dakitari! Linalosikitisha ni kuwa wengi wa viongozi wa baadaye kutoka kundi letu (Wabunge na Mawaziri) ni wale ambao somo la "additional & applied mathematics" walikaa nao mbali kama ukoma. Kweli mambo yalikuja kubadilika!

Duh! Mag3 una wajukuu wangapi sasa?
 
Mh. Tundu Lisu ananikumbusha mbali! Mwaka 1961 tukiingia Form 1, haikuchukua muda darasa letu, pamoja na kuwa vinyoya, likajulikana kama "siasa kali" (wakati huo hatujapata uhuru). Bahati mbaya wengi wa vipanga darasani walilazimika kuchukua masomo ya sayansi kwani huo uhuru wa kuchagua haukuwapo sana. Nina hakika mtu kama Tundu Lisu, angesoma wakati huo, labda siasa angeisikia tu kwa mbali...sana sana angeishia kuwa Injinia au dakitari! Linalosikitisha ni kuwa wengi wa viongozi wa baadaye kutoka kundi letu (Wabunge na Mawaziri) ni wale ambao somo la "additional & applied mathematics" walikaa nao mbali kama ukoma. Kweli mambo yalikuja kubadilika!

Dah! Heshima Mkuu. Shikamoo.
 
Ni kweli Tindu Lissu ana kipande cha lawama katika hili, lakini ukiangalia kwa undani, tatizo ni baadhi ya wabunge kuingia kwenye mob mentality na deindividuation kuchukua nafasi huku wakiamini hakuna adhabu itakayotolewa kwa sababu inavyoonekana wanaamini kila lile alifanyalo Mh. Tindu Lissu ni kweli.

Ukiangalia video ya bunge la siku tatu zilizopita, baada ya Tindu Lissu kuanza kugonga meza na kuimba, Mh. Msigwa naye papo hapo akaungana naye na wengine wakafuatia.

Cha kushangaza, Naibu spika (Mh. Ndugai) ambaye ndiye alishiriki katika uandishi na utengenezaji wa kanuni za bunge, inafikia sehemu anashindwa hata kujua ni kanuni ipi inasimamia lipi kama ilivyoonekana siku tatu zilizopita alipokuwa akihangaika kuuliza kanuni kwa wasaidizi wake pembeni. Hii nayo inajenga picha kwa wabunge kama spika na naibu kile wakifanyacho wala hakieleweki.

Nashindwa kuelewa, kwa nini watu wanalinganisha bunge la kipindi cha Mh. Sitta na la sasa na wanaona utendaji wa Mh. Sitta ulikuwa mzuri wakati tofauti zake ziko wazi kabisa ambazo ni nje ya utendaji mahiri wa spika bali ni idadi, aina ya wabunge na utendaji wa serikali bungeni. Kipindi cha Mh. Sitta, hakukuwepo na Mh. Lissu, Mh. msigwa, Mh. Nasari n.k

Kwa majumuisho, lawama ziko pande zote, ila mwanzilishi mara nyingi wa mabishano ya kanuni (Mh. Lissu) ndiyo anaonekana kwa macho ya Watanzania kama analeta vurugu kwa vile wananchi hawajawa na mazoea ya kuona bunge makini la vyama vingi ( No More Rubber-Stamp)
 
Ni ukweli usiopingika,yule mama anayeongoza bunge/pamoja na yule bro. 'wameshindwa' kazi yao! Haki inapopotea ni rahisi amani kutoweka!
 
Walimfanyia fitna sitta, sasa kamasi inawatoka, sitta alikua anajitahidi sana ku-balance mijadala, na sheria na kanuni anazijua kwelikweli, haya mazezeta mawili yalipewa uspika for a reason, to serve their masters, hata mimi nisingekubali hoja muhimu kama ya mnyika kuhusu maji zezeta ndugai linakataa tu lenyewe, kazi yake kuibana serikali, anajisahau yeye anakua part ya serikali, kwanini wapinzani wasikasirike kwa usenge kama huo?

let them reap what they sow,

ningependa zichapike siku moja bungeni, tena waanze na makinda au ndugai
 
Ngoja niandike kwa kifupi tu, sote tunafahamu kuwa Bunge la JMT na vikao vyake, linaongozwa kwa kanunu na sheria kama ilivyo kwa mabunge mengine.
Kwa kuwa umeamua kuuweka huu mjadala kuwa baina ya Tundu Lissu na Anne Makinda, basi ni vyema tukajikita zaidi kwenye ufahamu wao binafsi juu ya utambuzi na uchanganuzi wa sheria.

Ikumbukwe kuwa kila mara Tundu Lissu anaposimama na kupinga hoja au kutokua na imani na jambo fulani bungeni, huwa ananukuu vifungu fulani vya kanuni na taratibu. Sasa hapa tujiulize, uwezo wa Anne Makinda kutafsiri sheria ni mkubwa kiasi gani? Taaluma yake ya Ualimu inamsaidia kupambana na wanazuoni wa sheria kama Lissu?

Sidhani kama ni kweli maana ni mara kadhaa tumekuwa tukimsikia Anne Makinda, akikiri kuwq bado kanuni na sheria za Bunge zinamtatiza haswa katika kuzitafsiri.

"Nashukuru kutambua kuwa kaka yangu Pasco nawe ni Mmenye mwenzangu"
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom