Vurugu za Bungeni: Tundu Lissu, Anastahili Adhabu Kali?!. Ni Mtundu Toka Shule!.

Vurugu za Bungeni: Tundu Lissu, Anastahili Adhabu Kali?!. Ni Mtundu Toka Shule!.

Makinda amepwaya sana tatizo lake hajitambui tu, Tundu yupo right kupigania haki
 
Wajaribu kumfungia kuhudhuria vikao vya bunge waone moto wake.
 
Mkuu Pasco, hongera kwa mchango wako uliofuata baada ya bandiko, sitaki kuwaza sana kwa nini mara nyingi unapigiaga chapuo watu fulani na kuonekana kama unanukia marashi ya ukanjanja, lakini kwa hili natamalaki kwa kujua kumbe na wewe huwa una moyo na maoni ya kizalendo na nchi hii na kuchukia upuuzi uliokithiri wa awamu hii japo sijajua kama ni another trick kama za wale jamaa wa new habari na CDMA!!!
 
walimfanyia fitna sitta, sasa kamasi inawatoka, sitta alikua anajitahidi sana ku-balance mijadala, na sheria na kanuni anazijua kwelikweli, haya mazezeta mawili yalipewa uspika for a reason, to serve their masters, hata mimi nisingekubali hoja muhimu kama ya mnyika kuhusu maji zezeta ndugai linakataa tu lenyewe, kazi yake kuibana serikali, anajisahau yeye anakua part ya serikali, kwanini wapinzani wasikasirike kwa usenge kama huo?

let them reap what they sow,

ningependa zichapike siku moja bungeni, tena waanze na makinda au ndugai

Huogopi Ban???? maneno makali yanayokubalika yapo....tumia kufikisha ujumbe.....si hlo lenye red
 
Mh. Tundu Lisu ananikumbusha mbali! Mwaka 1961 tukiingia Form 1, haikuchukua muda darasa letu, pamoja na kuwa vinyoya, likajulikana kama "siasa kali" (wakati huo hatujapata uhuru). Bahati mbaya wengi wa vipanga darasani walilazimika kuchukua masomo ya sayansi kwani huo uhuru wa kuchagua haukuwapo sana. Nina hakika mtu kama Tundu Lisu, angesoma wakati huo, labda siasa angeisikia tu kwa mbali...sana sana angeishia kuwa Injinia au dakitari! Linalosikitisha ni kuwa wengi wa viongozi wa baadaye kutoka kundi letu (Wabunge na Mawaziri) ni wale ambao somo la "additional & applied mathematics" walikaa nao mbali kama ukoma. Kweli mambo yalikuja kubadilika!

Mkuu umehamia digitali kweli?
 
Mkuu Pasco,kwa mujibu wa hoja yako mimi nahisi Tundu Lissu akili zake zimepitiliza ndio maana anasumbua.
 
Haya unamjuwa, kama alikuwa ana fujo Ilboru, pale si Ilboru, kuna wenye fujo zaidi yake na kuna vichwa zaidi yake.
 
Spika na Naibu wake waondolewe au vinginevyo wafuate kanuni za Bunge pasipo kupindisha kanuni hizo na kuleta upendeleo kwa wabunge wa CCM. Wasipofanya hivyo tutegemee zaidi kukosolewa na wabunge wa upinzani, hasa Mh. Tundu Lissu.
 
Pasco.
Ilboru sekondari kama ilivyo Mzumbe Sekondari haikuwahi kuwa special school maisha yake yote ni kwa kipindi fulani.... hivyo basi umedanganya kusema wakati wenu ilikuwa special school, nadhani hapa ni sifa za bure mnakata... aliyesoma ilboru... naomba aangalie hiyo miaka ya Tundu Lisu kulikuwa na u-special school kati ya 1983 hadi 1986? O,'level?
 
Ni kweli Tindu Lissu ana kipande cha lawama katika hili, lakini ukiangalia kwa undani, tatizo ni baadhi ya wabunge kuingia kwenye mob mentality na deindividuation kuchukua nafasi huku wakiamini hakuna adhabu itakayotolewa kwa sababu inavyoonekana wanaamini kila lile alifanyalo Mh. Tindu Lissu ni kweli.

Ukiangalia video ya bunge la siku tatu zilizopita, baada ya Tindu Lissu kuanza kugonga meza na kuimba, Mh. Msigwa naye papo hapo akaungana naye na wengine wakafuatia.

Cha kushangaza, Naibu spika (Mh. Ndugai) ambaye ndiye alishiriki katika uandishi na utengenezaji wa kanuni za bunge, inafikia sehemu anashindwa hata kujua ni kanuni ipi inasimamia lipi kama ilivyoonekana siku tatu zilizopita alipokuwa akihangaika kuuliza kanuni kwa wasaidizi wake pembeni. Hii nayo inajenga picha kwa wabunge kama spika na naibu kile wakifanyacho wala hakieleweki.

Nashindwa kuelewa, kwa nini watu wanalinganisha bunge la kipindi cha Mh. Sitta na la sasa na wanaona utendaji wa Mh. Sitta ulikuwa mzuri wakati tofauti zake ziko wazi kabisa ambazo ni nje ya utendaji mahiri wa spika bali ni idadi, aina ya wabunge na utendaji wa serikali bungeni. Kipindi cha Mh. Sitta, hakukuwepo na Mh. Lissu, Mh. msigwa, Mh. Nasari n.k

Kwa majumuisho, lawama ziko pande zote, ila mwanzilishi mara nyingi wa mabishano ya kanuni (Mh. Lissu) ndiyo anaonekana kwa macho ya Watanzania kama analeta vurugu kwa vile wananchi hawajawa na mazoea ya kuona bunge makini la vyama vingi ( No More Rubber-Stamp)

Hapo kwenye bluu nimeshakukataza tokea jana husikii,kipindi cha sitta mijadala mizito kama epa na richmond aliruhusu ijadiliwe na ccm wenzake wakasulubiwa vya kutosha!!!idadi sio ishu we msukuma,slaa peke yake alikuwa analiyumbisha bunge zima,sitta hakuwa mbabaishaji,kanuni zote zilikuwa kichwani,..yani kumlinganisha sitta na makinda ni matusi makubwa kwa mzee sitta
 
Lissu ni kichwa/kipaji maalumu......tatizo Bunge limejaa vilaza wengi ukianzia kwa spika na naibu wake na 75% ya wabunge wa CCM ni vilaza baadhi yao ni mafisadi wa Elimu! mfano Lukuvi ni mwalimu wa UPE
 
JK alishawahi kusema kuwa "Ni afadhali Slaa awe Rais lakini sio Tundu Lissu awe Mbunge(sio Rais)"
Kumbe alishasoma alama za nyakati kitaambo.

Kitambo sana mbona?
Lissu anafahamika sana kwenye anga za sheria za haki za binadamu. Rufaa ya Godbless Lema ni ushahidi mwingine.
wa kazi yake.
 
Back
Top Bottom