Vurugu za Bungeni: Tundu Lissu, Anastahili Adhabu Kali?!. Ni Mtundu Toka Shule!.

Vurugu za Bungeni: Tundu Lissu, Anastahili Adhabu Kali?!. Ni Mtundu Toka Shule!.

Hivi katika hao wote waliosoma "spesho" skulz kuna hata mmoja aliyevumbua chochote?

Na kwa chochote namaanisha kitu au kanuni yoyote ile katika jambo lolote lile?

Yes, kanuni ya kumpelekesha Makinda na Ndugai hadi wanapoteza mwelekeo kabisa na kuahirisha kikao cha bunge, siku mbili mfululizo! Seminal, 100% Tanzanian!
 
Nahisi kizungu zungu hapa, mwaka 1961 palikuwepo na mfumo wa elimu wa form one? khaaaaa! Nisaidieni muliokula chumvi nyingi mkuu Mag3

Kwahiyo unataka kutuambia kwamba miaka hiyo ya mkoloni hakukuwa na shule za sekondari siyo?? yani wewe hata hujiulizi mwalimu Nyerere pamoja na wasomi wengine wa enzi za ukoloni waliwezaje kufika vyuo vikuu kama hakukuwa na Sekondari??
 
Kwahiyo unataka kutuambia kwamba miaka hiyo ya mkoloni hakukuwa na shule za sekondari siyo?? yani wewe hata hujiulizi mwalimu Nyerere pamoja na wasomi wengine wa enzi za ukoloni waliwezaje kufika vyuo vikuu kama hakukuwa na Sekondari??

mkuu Mwita Maranya, naomba unifafanulie tu ndugu yangu nijue mfumo mzima wa elimu enzi hizo kabla ya uhuru/enzi za ukoloni kuanzia primary hadi chuo kikuu kusomea diploma/degree ! Najua wasomi walikuwepo na wataendelea kuwepo we nitoe tu kizungu zungu mkuu!
 
Last edited by a moderator:
405769_213221562155375_747636924_n.jpg

Tundu Lissu ni MTUNDU kweli kweli
 
Unatumia vigezo gani kufikia hilo hitimisho?

Naomba unisaidie ili nikuelewe vizuri!

Dark City hauamini kama karne hii bado watu wanahongwa tshirt,kanga,sh 5000,na kula pilau na soda wanacheza kwamba hakuna kama fulani simply amehongwa vitu ambavyo baada ya muda mfupi havitumiki tena lakini amempa mtu ulaji wa miaka 5,bado sana na inatakiwa kazi ya ziada Watanzania wengi ni short sighted hawaangalii keshp kitatokea nini wao wanaangalia saa hivi wana nini,poor TANZANIAN
 
Wanabodi,

Juzi katika kikao cha bunge, Spika wa Bunge, Mhe. Anne Maklnda, alimtaja Mbunge wa Singida, Mhe. Tundu kama ndie Mbunge anayeongoza kwa kuwa chanzo cha vurugu za bungeni, kwa kuongoza kwa utovu wa nidhamu, kuleta fujo na vurugu bungeni, hali ambayo sio tuu inahatarisha hali ya utulivu, amani na usalama wa bungeni, bali pia kumepelekea Spika kufuta baadhi ya ratiba za bunge ambazo zilikwisha ridhiwa na kuingizwa kwenye order paper ikiwemo kupokea hoja binafsi za wabunge, kwa kilichoelezwa kuepuka vurugu zaidi.

Jana kika cha kamati ya Uongozi kimekaa kujadili hali hiyo na matokeo yake, tutayapata kesho asubuhi baada ya kipindi cha maswali ya papo kwa papo na maswali na majibu! ni hakika rungu la kiti, lazima litamshukia Mhe. Tundu Lissu!.

Swali la kwanza la kwanza ambalo wengi mtapenda kujiuliza ni, ni jee ni kweli, Mhe. Tundu ni mtundu na ndie chanza cha utovu wote wa nidhamu wa bunge hili la kumi?, kama anavyoelezwa na Madam Speaker?, au huo utundu wa Mhe. Tundu, sio utundu bali uzingatiaji wa kanuni za Bunge, kufuatia Mhe. Spika, kuonyesha udhaifu mkubwa katika kuliendesha bunge kwa kutokuzingatia, sheria, taratibu na Kanuni?.

Kwa vile mimi ni mmoja wa watu tunaomfahamu Mhe. Tundu, Tangu akiwa Shuleni, Ilboru (sio darasa moja, Nikiwa A-level, yeye alikuwa O-Level) naomba kuchukua fursa hii kumfariji Mhe. Spika, kwa kumuomba asiumize sana kichwa chake kuendelea kubishana na Mheshimiwa Tundu Lissu kuhusu kanuni za bunge, wala wasipoteze muda kumuadhibu kwa jambo ambalo liko wazi kabisa na udhaifu unajulikana tangu chanzo chake, ulipo na labda utaendelea kuwepo, hata akiadhibiwa vipi, kwa sababu Mhe. huyu ni mbishi hakuna mfano!, haswa pale anapokuwa na uhakika kuwa yuko right!.

Nashauri Mhe. Spika, lazima ufike mahali, umkubali huyu jamaa kuwa lile jina lake la Tundu, sio jina tuu, huyu bwana analiishi jina lake kwa kuwa ni mtundu kweli pale kanuni zinapopindishwa ili kutoa mteremko kwa upande fulani!.

Nimebahatika kusoma na Mhe. Lissu shule moja kule Ilboru, (sio darasa moja) miaka hiyo enzi za Mkuu mmoja aitwae Bino!. Huyu Bino alikuwa ni mwalimu mkuu bingwa wa nidhamu, ila kwa Tundu, alinyanyua mikono juu na kwisha kuishusha juu baada ya kuthibitika kuwa japo Tundu alikuwa "toto tundu", ila pia ndie aliyekuwa kipanga wa darasa lake!, kwani pepa alikuwa akizifumua, utadhani mtihani katunga yeye!.

Tundu Lissu alijiunga shule ya vipanga ya Ilboru akitokea Singida, wakati huo akiitwa Antipasi Tundu, na alikuwa ni mtoto mtundu kweli!. Wakati huo, Ilboru ilichukua wanafunzi wenyeji wa Arusha, Singida na Shinyanga!. Sisi Wasukuma tukiitwa "Wasukusu", wenyeji wakiitwa "wamenye" huku jamaa wa Singida wakijiita watu wa "Singapore", uji ukiitwa "sumu", na nje kulikuwa na duka la kwa "Akwii".

Utundu wa Tundu Lissu ulkikuwa ni kwenye mishe mishe tuu hizi za zile, haijulikani alikuwa akisoma saa ngapi, ila pepa zikija, anafumua ile mbaya!. Moja ya maeneo ambayo jamaa alikuwa ni ni mtundu au tusema ni mbishi, ni kwenye school debate!. Jamaa akishakuwa na uhakika yuko on the right track, ni mbishi hakuna mfano!. Hata nami nilikuwa na matatizo yangu tangu shule, yale matatizo ya kawaida ya Chapa Ng'ombe, unapokutana na vibinti vya Vyeupe vya Kiarusha pale Mlimani Ilboru, ukijumlisha na lilke baridi la kule, tena wakati huo, "bwawa halijaingia luba!'...

Tundu lissu aliondoka na wani kali, akaenda Galanos hatimaye UDSM. Sisi vilaza wengine tukaishia vile vyuo vya mashenzini!. Tulipoteana kwa kipindi cha miaka 10!, tulikuja kukutana tena mjini Atlanta, yeye akiwa na yeke nami na yangu, ndipo akanieleza yuko LEAT, na huko aliichachafya serikali vivyo hivyo kama anavyo mchachafya Madame Spika, kwa kumsubu bila huruma!.

Pamoja na utundu wote huu wa Mhe. Tundu Lissu, wakati tukisubiria kusikia ni adhabu gani itamfika hapo kesho, kuna maswali matatu tujiulize!.
  1. Jee ni kweli Mhe. Tundu Lissu ni mtundu kihivyo na ndio anayeongoza kwa utovu wa nidhamu hadi kustahili adhabu kali?.
  2. Au ni Spika ndiye dhaifu hadi kushindwa kumdhibiti Tundu Lissu na utundu wake?.
  3. Baada ya kuthibitisha, Mhe. Tundu Lissu alikuwa ni mtundu toka shuleni, jee nani wa kubadilika kati ya Mhe Tundu Lissu na wabunge wa upinzani, wakae kimya wakati sheria, ?, hivyo kumpatia fursa Mhe. Spika kujiendeshea bunge anavyotaka, ili kudumisha utii, na nidhamu, bunge liwe la amani?.
  4. Hivyo Mhe Spika kuwathibitishia Watanzania kuwa hata yeye ambaye ni "ameweza" kuliendesha bunge vizuri tuu, ambalo ni mhimili mmoja wa dola, hivyo jee, 2015, tukamilishe majaribio ya "jinsia" kwa mihimili miwili iliyobakia?, ili nchi yetu iwe ni nchi ya usawa halisi wa kijinsia?.

Wasalaam

Pasco.
(Skulu Meti wa Toto T).

Mkuu PASCO naomba kunukuu baadhi ya maneno katika thread yako ambayo naona ndiyo chanzo cha matatizo yote haya:
  1. Spika ndiye dhaifu
  2. Spika kujiendeshea bunge anavyotaka
  3. Bunge lina "Spika wa majaribio ya jinsia"
  4. Taratibu na kanuni, zinakiukwa, na kupindishwa
 
Je Makinda naye ni Kinda bado katika uendeshaji wa shughuli za Bunge ?

siyo yeye tu ni makinda na makinda yake ya ccm bado ni makinda katika upeo wao hata wa kutambua kuwa watanzania siku hizi wamekuwa waelewa na wanajua nani mkweli na nani longolongo.
hoja zilizoletwa bungeni na ccm na upinzani ukizipima tu huhitaji elimu ya chuo kikuu kutambua ipi muhimu kwa maslahi ya taifa.
 
Tundu mbele ya Kinda nani zaidi? hakika kauli ya Jk inajidhihirisha waziwazi.
 
Ni kweli Tindu Lissu ana kipande cha lawama katika hili, lakini ukiangalia kwa undani, tatizo ni baadhi ya wabunge kuingia kwenye mob mentality na deindividuation kuchukua nafasi huku wakiamini hakuna adhabu itakayotolewa kwa sababu inavyoonekana wanaamini kila lile alifanyalo Mh. Tindu Lissu ni kweli.

Ukiangalia video ya bunge la siku tatu zilizopita, baada ya Tindu Lissu kuanza kugonga meza na kuimba, Mh. Msigwa naye papo hapo akaungana naye na wengine wakafuatia.

Cha kushangaza, Naibu spika (Mh. Ndugai) ambaye ndiye alishiriki katika uandishi na utengenezaji wa kanuni za bunge, inafikia sehemu anashindwa hata kujua ni kanuni ipi inasimamia lipi kama ilivyoonekana siku tatu zilizopita alipokuwa akihangaika kuuliza kanuni kwa wasaidizi wake pembeni. Hii nayo inajenga picha kwa wabunge kama spika na naibu kile wakifanyacho wala hakieleweki.

Nashindwa kuelewa, kwa nini watu wanalinganisha bunge la kipindi cha Mh. Sitta na la sasa na wanaona utendaji wa Mh. Sitta ulikuwa mzuri wakati tofauti zake ziko wazi kabisa ambazo ni nje ya utendaji mahiri wa spika bali ni idadi, aina ya wabunge na utendaji wa serikali bungeni. Kipindi cha Mh. Sitta, hakukuwepo na Mh. Lissu, Mh. msigwa, Mh. Nasari n.k

Kwa majumuisho, lawama ziko pande zote, ila mwanzilishi mara nyingi wa mabishano ya kanuni (Mh. Lissu) ndiyo anaonekana kwa macho ya Watanzania kama analeta vurugu kwa vile wananchi hawajawa na mazoea ya kuona bunge makini la vyama vingi ( No More Rubber-Stamp)


Ng'wanamapalala

Du, Watanzania gani tena hao pot? Madame Speaker ndiyo Watanzania?
 
Dhulma ya madame speaker na naibu wake ndiyo chanzo kikubwa cha vurugu bungeni, Leo hadi Shibuda amewaonya kwa jinsi walivyo chemsha! I wish wampe adhabu ili waonje ladha ghadhabu hasira za watanzania...
 
Ng'wanamapalala

Du, Watanzania gani tena hao pot? Madame Speaker ndiyo Watanzania?

Mkuu,
Nilichofanya hapa ni kuwa na balanced opinion. Tukubali kuwa pale mjadala unapohamia katika jamii basi lazima kutakuwepo na contradicting remarks.

Ninafikiri hata wewe unafahamu kama kuna watu ambao mtazamo wao utakuwa upande wa Mh. Makinda na huku wengine wakiwa upande wa Mh. Lissu.

Nashindwa kuelewa kwa nini unaona kama sikumtendea haki Mh. Lissu wakati hata mtendaji mkuu wa chama (Dr. Slaa)aligusia kwenye press conference na kusema yeye anapingana na mbinu iliyotumika kukabiliana na machafuko bungeni ambapo bunge liliahirishwa badala ya kuwa susppended kwa muda tu mpaka pale hali ya amani itakapo rejea ili kikao kiendelee.

Anyway, hili ni wazo langu tu na tukubali kutokubaliana.
 
I didn't ask you, did I?

Uko kwenye mjadala jamvini. Watu wsnajadili mambo mazito. katikati unauliza idadi ya wajukuu. just say what does it have to do with the discussion. stop trivializing serious deliberations.
 
Uko kwenye mjadala jamvini. Watu wsnajadili mambo mazito. katikati unauliza idadi ya wajukuu. just say what does it have to do with the discussion. stop trivializing serious deliberations.

You can't tell me what to do.
 
Makinda anaidhurumu nafsi yake na naamini inamsuta kwa kutetea mafisadi wakubwa, anapindisha sheria wazwaz hata mtoto wa shule ya msingi ataligundua hilo bila kuambiwa, LISSU ni jembe sana na anajua analofanya na hua yupo makini sana , wakimpa adhabu itawatokea puani, kwanza sakata hilo naamini lishawamaliza jijini dar es salaam sasa wakiendelea kurikoroga ndo wanajimaliza kabisaa, all in all lets wait nguvu ya umma inaelekea kushinda 2015 utakua mwanzo wa siasa mpya za tanzania!!
 
Unatumia vigezo gani kufikia hilo hitimisho?

Naomba unisaidie ili nikuelewe vizuri!
Mkuu Dark City,
nimeripoti chaguzi 4, hivyo ya 2015 itakuwa ni uchaguzi wa tano kuuripoti. CCM siku zote inashinda sio kwa sababu inapendwa sana, bali kwa mazoea tuu!, nimeisha andika makala zangu mbalimbali kwa nini 2015 ni CCM tena. Chadema itavuna wabunge wengi zaidi huku bara, CUF itapoteza baadhi ya majimbo. Mshindi wa jumla wa urais ataendela kuwa CCM!.

Chadema inayo nafasi ya kushinda kama itakubali "to do things right", kwa sasa kupitia M4C, Chadema, inafanya kazi nzuri, yaani "is doing the right thing!". Ili chapa kipya kiweze kuking'oa "chama kubwa", "chama kongwe", na kuingia Ikulu, "doing the right thing" peke yake hakutoshi!, it got to do "things right", kitu ambacho sikioni Chadema kufanya!, as a result watu wataendeleza mazoea!.

Zile umati za watu kwenye maandamano au kwenye mikutano, sio kura!, nimeisha waambia Chadema humu kwa nini hawatashinda urais 2015 na nini cha kufanya, lakini nimeishia kutukanwa tuu "wee gamba!", mimi nasisitiza kuendelea kusema ukweli no matter what. Let them call me what they may, ila ikifika 2015 mtayaono na baada ya hapo tutaanza kuelewana vizuri!.

Siasa ni kama barabara ndefu, mbovu na ya kona kona, milima, mabonde, mashimo na makorongo!, vyama ni kama magari, wanachama ndio abiria, na viongozi wa vyama ndio madereva!. Kuelekea 2015 ndio safari yenyewe. Kwa huku bara, mchuano ni kati ya CCM, (gari kongwe, injini kongwe chovu, lakini dereva mzoefu, aliyeisha izoea hiyo barabara, miaka nenda, miaka rudi, hivyo anajua aendesheje, wapi apunguze mwendo na wapi aende kasi, wapi kuna korongo wapi kuna bonde, wapi kuna konakali na wapi kuna mlima, etc,etc!) na Chadema (gari mpya na injini bomba ina nguvu kupita gari kongwe na inakwenda mbio kuliko ule mkweche ila ina dereva mpya ambaye hajui njia!, kazi ya dereva mpya ni kutimua mbio, na kuendesha kwa kasi ili awahi kufika!, kutokana na kutojua njia, japo anakwenda kasi zaidi, kwa kuipita gari kongwe kwa mbali, mara kibao hujikuta anapotea njia, hivyo kulazimika kurudi nyuma na kuendelea na safari!.

Kwenye hii scenario, huyu dereva mpya anayo nafasi ya kushinda, sio kwa kitimua mi mbio, bali endapo atakubali au kuwasikiliza baadhi ya abiria wake wazoefu ambao wameishaipita njio hiyo mara nyingi ndani ya ule mkweche, au kutusikiliza sisi watazamaji wa mchuono huo ambao sio abiria wa gari yoyote, ila tuko homo njiani kwa muda mrefu, tunapoona dereva mpya anakosea, huwa tunampungia ishara kuwa huko siko!, au kumpa ishara ya hatari ya mbele, lakini hasikilizi!. Yeye ni mwendo kasi wa mbio tuu huku akishangiliwa na umati wa abiria wake, kuwa aendeleze "mwendo mdundo!.

Safari ya kuelekea 2015 ndio hii inaendelea, sasa hivi tuko half way!, bado hakuna dalili za dereva mpya kujifunza, hebu tusubiri, nasikia kutafanyika zoezi la kubadilishana madereva baadae mwaka huu, hebu na tusubirie timu mpya tuone, hata ikirudi timu ile ile kama itaendelkeza uendeshaji ule ule, basi ni hakika bila mashaka yote, mshindi ataendelea kuwa yule yule, dereva bingwa mwenye ule mkweche!.

Pasco.
 
Back
Top Bottom