VVU na UKIMWI: Historia yeke, chanzo cha maambukizi, dalili, kinga na juhudi za kupambana na ugonjwa huu

VVU na UKIMWI: Historia yeke, chanzo cha maambukizi, dalili, kinga na juhudi za kupambana na ugonjwa huu

Hivi ni kweli kwamba "kuna dawa ambayo ukimeza kabla/muda mfupi baada ya kujamiana inazuia maambukizi ya VVU"???
Ni kweli dawa hizo. Zinatolewa kwa watu walioko katika mazingira hatarishi ya kupata maambukizi ya VVU mfano Madaktari Baada ya kujichoma sindano, iwapo umekutana na mtu ambaye ana maambukizi
 
Virusi wa UKIMWI wana uwezo wa moja kwa moja wa kushambulia mfumo wa fahamu hasa ubongo. Hivyo wakati mwingine mtu anaweza kuumwa matatizo ya akili kutokana na virus hawa. Mara nyingi wakianza kutumia dawa na kinga kupanda Ile ugonjwa wa akili unapona
Umeshamuona huyo HIV?
 
Discordant couples kwa lugha rahisi ni kwamba mwanandoa mmoja ameathirika na mwingine hajaatharika. Kitu gani kinachosababisha hali hii kutokea hakijulikani. Hata hivyo watafiti wanafikiria juu ya mambo mengi mfano jinsia, genitiki, afya ya wanandoa, matumizi ya kondom nk nk.

Hasara kubwa ni kwamba hali hii inachangia kuenea sana kwa maambukizi
Faida ni kuwa hawa wanandoa wanaweza kuwa sampuli nzuri katika majaribio kinga na tiba ya UKIMWI
Majibu ya kitaalamu sana haya!!!
 
Bakteria wengi wanaonekana kwa microscope za kawaida. Virus wa HIV waneonekana kuanzia zamani. Na sasa hivi wanaonekana kwa kutumia 3D electronic microscope. Pitia hii article kutoka PubMed
Catching HIV ‘in the act’ with 3D electron microscopy
3D ni teknolojia ya juu sana ktk maswala maswala ya picha na michoro. Kifupi hutoa/huonesha picha/mchoro kwa uharisia wake. Ahsante Mkuu, kifupi wewe ni mbobezi ktk maswala ya HIV/AIDS kama siyo afya kwa ujumla wake.
 
Inawezekana umekuwa na maswali ambayo yamekuwa yakikutatiza juu ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI na ugonjwa wa UKIMWI.

Leo nakupa nafasi ya kuuliza swali lolote juu ya mada hii. Twende kazi!


Mteja /Mtu anapogundulika ni HIV+... Ni vipimo gani kwa sasa ambavyo huwa anatakiwa kufanya na kwa interval ipi kama vile kwa ajili ya Monitoring ya CD4, kucheki wingi wa virusi, athari za dawa kwa mgonjwa kwenye figo na ini..... Nawaza tuu...
 
Ni kweli dawa hizo. Zinatolewa kwa watu walioko katika mazingira hatarishi ya kupata maambukizi ya VVU mfano Madaktari Baada ya kujichoma sindano, iwapo umekutana na mtu ambaye ana maambukizi
Mkuu Vipi Upatikanaji Wa Hizi Dawa Upoje!, namaanisha zinapatikana hadi kwenye maduka ya dawa ya kawaida au Hadi Hospital?.
 
Tafiti nyingi zimeonyesha dalili zifuatazo hujitokeza kwa watu wengi waliopata maambikizi ya VVU kwa mara ya kwanza. •Homa •Uchovu •Maumivu ya viungo na misuli •Kuvimba mitoki sehemu mbalimbali ya mwili •Kupata vidonda kwenye koo •Upele mchanganyiko kwenye kiwiliwili •Vidonda sehemu mbali mbali mwili •Kuharisha •Kichefuchefu na Kutapika •Kupungua uzito •Kutoka jasho hasa wakati wa usiku •Maumivu ya kichwa. •Homa ya uti wa mgongo (baadhi ya wagonjwa. Dalili hizi za awali hufanana na dalili za mtu anayeumwa mafua. Dalili hizi hujitokeza katika kipindi cha wiki mbili mpaka 6 toka kupata maambukizi ya VVU.
Ni lazima hizi dalili zijitokeze zote kwa the same time ?
 
Back
Top Bottom