Unakimbia nini?
Utakuja kupima wakati ni too late.
Majibu yote yana faida.
Ukikutwa na VVU unachukua hatua sahihi ( kuepuka maambukizi mapya, kuepuka kuambukiza wengine, na kuzuia usiende kwenye hatua ya UKIMWI).
Ni kama unavyokutwa na kisukari au shinikizo LA damu, hayana tiba ila unazuia complications zake kwa kuyadhibiti.
Ukikutwa huna then unaendeleza mapambano ya kuhakikisha hupati.
Unaogopa kupima Leo kwa kujihisi, unaacha kuchukua tahadhali then unakuja kupata maambukizi many years after ulipojihisi.
Kutokupima ni kujidanganya, utakuja kupimwa ukiwa hata huna nguvu ya kusema sitaki kupimwa.
Wakati ni huu, tukomae kufikia 90, 90, 90 hatimaye VVU/ukimwi vidhibitiwe kama Ukoma.