Vyama vya Upinzani, kubalini kwamba sio udikteta wote ni mbaya

Vyama vya Upinzani, kubalini kwamba sio udikteta wote ni mbaya

DaudiAiko

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2012
Posts
372
Reaction score
310
Wanabodi,

Inabidi tusome nyaraka za wakati katika kipindi ambacho wapinzani wanaishiwa nguvu. Labda kupungua kwa ushawishi wa vyama vya upinzani umesababishwa na chama tawala. Vile vile labda sera zao zimepitwa na wakati. Maoni mbali mbali kuhusu harakati za vyama vya upinzani yametolewa lakini takwimu muhimu ni kwamba chama kikuu cha upinzani (CHADEMA) kilipata mbunge mmoja tu wakuchaguliwa kwenye uchaguzi wa 2020.

Sidhani kama vyama vya upinzani vitafanya vizuri kwenye uchaguzi wa 2025 na kwasababu hiyo, nimeanza kujiandaa kisaikolojia kwa ajili ya serikali yenye wawakilishi wa chama kimoja tu. Hii ni ishara ya kuelekea kwenye udikteta lakini sio udikteta wote ni mbaya.

"Benevolent dictatorship" ni aina ya udikteta ambao viongozi hufanya maamuzi sahihi na yenye manufaa kwa wananchi bila kuminya haki na uhuru wa wananchi wao. Hii hupunguza sana urasimu na michezo ya kisiasa iliyopo kwenye demokrasia.

Serikali iliyopo madarakani itakuwa imejihakikishia ushindi kwenye kila chaguzi na mamlaka ya kufanya maamuzi yoyote bila kuwashirikisha wengi. Kwasababu hiyo, ni muhimu kwa mfumo huu kuhakikisha uwepo wa nidhamu, na umakini katika kuhakikisha kwamba serikali haikosei.
 
Haya ni matamanio ya kila mwanaccm kuwa CHADEMA ipoteze nguvu, ila CHADEMA wakifanya movement hata moja na kujaza watu, utaona CCM inaanza tena kujishikisha na vyombo vya dola

Iko hivi, CCM sio chama cha kizazi hiki, na haitakaa tena ivute hisia za watu hasa vijana wa kizazi hiki. CCM haina uwezo tena wa kushinda uchaguzi wowote kihalali, na haitakaa iwe tena na uwezo huo.

Ni kweli kuwa inaweza kuendelea kukaa madarakani, ila sio kwa ushawishi tena wa kisiasa, bali ni mashirikiano yao ya kihalifu na vyombo vya dola. Mfano mrahisi ni sasa, CCM iko zaidi ya 97% kwenye sehemu zote za uwakilishi, lakini isiyo na mvuto kabisa, huku wananchi wakipuuza box la kura.

Matokeo haya ya wananchi kulipuuza box la kura ni ishara ya wazi ya kuichoka CCM, na hii itapelekea machafuko huko mbeleni ili kuitoa CCM madarakani. Tuombe machafuko hayo yasiwe makubwa, maana yataliharibu Taifa letu.
 
Lini nchi hii middle class wetu wataanza kuwa wakweli? Why middle class wetu wana huluka ya uongo,pretending?hivi hamuelewi kuwa tabia hii inatuletea generations za ajabu ambazo hazijiamini?

Mtoa hoja ur out of touch au ni mnafiki uliyelelewa kwenye familia ya kinafiki na UONGO mwingi,waambie chama dola waitishe UCHAGUZI mkuu even next week na playing field sawa na watanzania waamue kwa haki.
 
CDM wala haipo tena. Haina ushawishi popote zaidi ya Kilimanjaro na Arusha kidogo. Chama cha wahuni nani anataka?
 
Umeandika vyema maoni yako ila watafsiri watafakari hoja ndio wenye matatizo!
 
Wanabodi,

Inabidi tusome nyaraka za wakati katika kipindi ambacho wapinzani wanaishiwa nguvu. Labda kupungua kwa ushawishi wa vyama vya upinzani umesababishwa na chama tawala...
Wafariji TU waachukua chako mapema, kuwa Wana nguvu, Hulu wakiishi kwa kubambiki na kwa mbelelo ya policcm
 
Haya ni matamanio ya kila mwanaccm kuwa CDM ipoteze nguvu, ila CDM wakifanya movement hata moja na kujaza watu, utaona CCM inaanza tena kujishikisha na vyombo vya dola...
Hicho kizazi kipya cha kujivunia Tanzania [emoji1241] unachokiongelea ni kipi kwa mfano?

Hiki kizazi cha wala chips na wacheza Bongo fleva?

Hawa wanaojua ratiba za Fiesta nchi nzima kuliko historia fupi ya nchi yao,ilipotoka,ilipopitia na inakoelekea?

Hawa hawa wanaotembea wakiwaza ku-bet,kuliko kuwaza kufanya kazi yoyote ili kujipatia kipato cha jasho halali?

Kizazi cha wasomi wasootaka kuitumia akili yao ili kuigeuza elimu yao kuwa pesa?

Msomi anayewaza siasa akiwa anaota ubunge wakati bado yuko darasani?

Bado nchi hii hatuna wanasiasa wa vyama vya upinzani unaowaita wa kizazi kipya,zaidi ya kuwaona wamekariri mistari ya wasomi wa kizungu.

Imekuwa hulka siku hizi kukaona ka mwanasiasa kako jukwaani halafu kila baada ya dakika mbili unasikia.....ndugu wananchi nikimnukuu ......katika kitabu chake.......alisema.......

Hao ndio unawaandaa kupewa nchi??

Hoja sio ujana au uzee wa chama au wanasiasa bali uzalendo,maono,uadilifu,uthubutu na muelekeo wa taifa letu kwa vizazi vijavyo.
 
Hicho kizazi kipya cha kujivunia Tanzania [emoji1241] unachokiongelea ni kipi kwa mfano?

Hiki kizazi cha wala chips na wacheza Bongo fleva?

Hawa wanaojua ratiba za Fiesta nchi nzima kuliko historia fupi ya nchi yao,ilipotoka,ilipopitia na inakoelekea?

Hawa hawa wanaotembea wakiwaza ku-bet,kuliko kuwaza kufanya kazi yoyote ili kujipatia kipato cha jasho halali?

Kizazi cha wasomi wasootaka kuitumia akili yao ili kuigeuza elimu yao kuwa pesa?

Msomi anayewaza siasa akiwa anaota ubunge wakati bado yuko darasani?

Bado nchi hii hatuna wanasiasa wa vyama vya upinzani unaowaita wa kizazi kipya,zaidi ya kuwaona wamekariri mistari ya wasomi wa kizungu.

Imekuwa hulka siku hizi kukaona ka mwanasiasa kako jukwaani halafu kila baada ya dakika mbili unasikia.....ndugu wananchi nikimnukuu ......katika kitabu chake.......alisema.......

Hao ndio unawaandaa kupewa nchi??

Hoja sio ujana au uzee wa chama au wanasiasa bali uzalendo,maono,uadilifu,uthubutu na muelekeo wa taifa letu kwa vizazi vijavyo.

Kwa hiyo CCM ya wazalendo ni akina Mwinyi na Ridhiwani? Hawa vijana unawaona waoga ndio hao wanaoendesha mauji kwa sasa nchini, na wengine hadi kuua wazazi wao. Kama unaamini hicho chama cha wazee kitaendelea kupeta maana kina mbeleko ya vyombo vya dola, endelea kuamini hivyo hivyo.
 
Haya ni matamanio ya kila mwanaccm kuwa CHADEMA ipoteze nguvu, ila CHADEMA wakifanya movement hata moja na kujaza watu, utaona CCM inaanza tena kujishikisha na vyombo vya dola

Iko hivi, CCM sio chama cha kizazi hiki, na haitakaa tena ivute hisia za watu hasa vijana wa kizazi hiki. CCM haina uwezo tena wa kushinda uchaguzi wowote kihalali, na haitakaa iwe tena na uwezo huo.

Ni kweli kuwa inaweza kuendelea kukaa madarakani, ila sio kwa ushawishi tena wa kisiasa, bali ni mashirikiano yao ya kihalifu na vyombo vya dola. Mfano mrahisi ni sasa, CCM iko zaidi ya 97% kwenye sehemu zote za uwakilishi, lakini isiyo na mvuto kabisa, huku wananchi wakipuuza box la kura.

Matokeo haya ya wananchi kulipuuza box la kura ni ishara ya wazi ya kuichoka CCM, na hii itapelekea machafuko huko mbeleni ili kuitoa CCM madarakani. Tuombe machafuko hayo yasiwe makubwa, maana yataliharibu Taifa letu.
AMEN
 
Wanabodi,

Inabidi tusome nyaraka za wakati katika kipindi ambacho wapinzani wanaishiwa nguvu. Labda kupungua kwa ushawishi wa vyama vya upinzani umesababishwa na chama tawala. Vile vile labda sera zao zimepitwa na wakati. Maoni mbali mbali kuhusu harakati za vyama vya upinzani yametolewa lakini takwimu muhimu ni kwamba chama kikuu cha upinzani (CHADEMA) kilipata mbunge mmoja tu wakuchaguliwa kwenye uchaguzi wa 2020.

Sidhani kama vyama vya upinzani vitafanya vizuri kwenye uchaguzi wa 2025 na kwasababu hiyo, nimeanza kujiandaa kisaikolojia kwa ajili ya serikali yenye wawakilishi wa chama kimoja tu. Hii ni ishara ya kuelekea kwenye udikteta lakini sio udikteta wote ni mbaya.

"Benevolent dictatorship" ni aina ya udikteta ambao viongozi hufanya maamuzi sahihi na yenye manufaa kwa wananchi bila kuminya haki na uhuru wa wananchi wao. Hii hupunguza sana urasimu na michezo ya kisiasa iliyopo kwenye demokrasia.

Serikali iliyopo madarakani itakuwa imejihakikishia ushindi kwenye kila chaguzi na mamlaka ya kufanya maamuzi yoyote bila kuwashirikisha wengi. Kwasababu hiyo, ni muhimu kwa mfumo huu kuhakikisha uwepo wa nidhamu, na umakini katika kuhakikisha kwamba serikali haikosei.
Ndugu,
Hizo ni hadithi za watu ambao pamoja maguvu yote na pia kujipa umungumtu, walishindwa kabisa kuwa na mvuto wa kweli. Na ni za watu wale wanaoogopa maoni na maamuzi HALISI ya wananchi kupitia uchaguzi HURU na wa haki, lakini wamejawa UROHO wa kutawala.
Udikteta ni udikteta TU hata uupakeje rangi. Katika historia PIA pamekuwapo na waimba mapambio wengi wa aina yako wanaotetea udhalimu na ukandamizaji bila aibu kwa kuongozwa na tamaa na njaa zao. Akina Propesa Kabundi.
 
ALIEMFANANISHA MWAFRIKA NA NYANI ALIONA NINI? KWA MAONO YAKO UNAIVIONGOZIONA CCM BORA KAMA YALIVYO MAONI YAKO. TUTAFUTE KWANZA MACHO KISHA ZIFUATE AKILI MAANA HATA MAARIFA TUMEKOSA PIA. SISI NI KAMA VIPOFU. VIONGOZI WA KIAFRIKA NI TAKATAKA.
 
Tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...
 
Back
Top Bottom