Vyeti visivyo na nguvu mbele ya five experience na umekaa shule miaka 17

Vyeti visivyo na nguvu mbele ya five experience na umekaa shule miaka 17

sangaone98

Member
Joined
Apr 16, 2024
Posts
77
Reaction score
107
Hiki ni kipindi kigumu sana kwa upande wa vijana hasa kwa watoto wa kiume.

Mambo yamegeuka kabisa

Zamani jamii ilikuwa inaamini mtu alie soma ndie mkombozi wa jamii hasa kwenye swala la uchumi lakini mambo yamekuwa sio kwa miaka ya 2000 to date.

Kila mmoja anashuudia maajabu yanayo fanywa na watu ambao hawakupata nafasi ya kwenda shule hasa elimu za juu( chuo).

Ndio watu ambao leo vijana walio soma wanawategemea hasa kwenye swala la uchumi,

Wakati wew upo shule unapiga kitabu ili sikumoja upate kuishi vizuri mwenzio yupo mtaani anatafta connection za maisha na michongo kwa sababu hajasoma na hana kitu kingine cha kujivunia kwenye swala la kupata pesa zaidi ya afya, akili na nguvu alizo nazo,

Baadae ukimaliza shule unakuta wale ambao waliishia form 4 wakat ww unaenda chuo au Alevel wamesha weka maisha yao kwenye mstali mzuri wakati ww unajikuta unakosa pa kuanzia kuyakabili maisha na hapo ndipo unaanza kujutia kwanni ulienda shule ukapoteza mda wa utaftaji kwa cheti ambacho leo kinakosa thamani mbele ya uzoefu wa miaka mitano plus( experience 5yrs×).

Ahsanten.
 
Back
Top Bottom