Vyombo vya habari Tanzania ubaguzi wenu utawaponza. Hii siyo haki

Vyombo vya habari Tanzania ubaguzi wenu utawaponza. Hii siyo haki

MAHANJU

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2014
Posts
5,252
Reaction score
8,003
Nianze na kuvisikitikia vyombo vya habari hasa baadhi ya TV stations kubwa kubwa hapa nchini na baadhi ya magazeti. Mnafanya ubaguzi kwa kuonesha live coverage kwa matukio ya CCM pekee. Endeleeni na ubaguzi huu iko siku mtasema ukweli.

Tundu Lissu anazunguka mikoani kutafuta wadhamini na matukio yake anahudhuria na maelfu ya watu ambao wanasimamisha hata kazi zao kwa masaa, hizi ni habari na matukio yanayoaswa kusomwa kwenye taarifa zenu na kuandikwa pia kwenye magazeti.

Eti mnatishwa, kwanini anayewatisha msimwambie aende mahakamani au aliwafungia mkamshtaki ili haki itendeke?

Kama tukio la Lissu kutafuta wadhamini ni haramu si mngeshaona amepelekwa mahakamani?
Endeleeni kulinda ugali wenu kwa kuogopa kuwapa watanzania ukweli. Andikeni habari zenu kwa kuchagua lakini hamtafanikiwa.

Sijajua udhaifu wenu kwenye sheria ya nchi uko sehemu gani? Hivi hamna wanasheria wa kusimamia vyombo vyenu mnasubiri kutishwa tu?

Siasa hazitabiriki, huyu mnayeogopa kumuonyesha siku akiwa Rais wenu mtafanyaje?
 
Hata wao hawapendi hii hali, sema ndio hawana lakufanya. Wanajua fika habari za Lissu wakati huu ndio zingewafaa kwenye kuuza magazeti yao, na kuvipa umaarufu vituo vyao vya radio na televisheni.

Lakini wanaona ni bora wapate hicho kidogo wanachopata sasa hivi kwa kuwapa wasikilizaji wao na watazamaji wao wasichokipenda, kuliko walazimishe kutaka kingi, halafu ndio vyombo vyao vifungiwe kabisa.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Kwa lugha rahisi ni kila mfanyabiashara anajua sio tu JPM atashinda bali atashinda kwa margin kubwa, yafaa nini kupoteza resources zao kwa failure Lissu.
tusisahau vita ya goliati na daudi ..mambo yanabadilikaga tu gafla..huwezi jua lini ni lini na wapi
 
kwa ukawaida tu ni kwamba watu wanaangalia na maisha baada ya uchaguzi unaweza ukawapa promo wapinzani baada ya hapo uchaguzi ukiisha ukajutia maamuzi ..hata kama ulikuwa unalipa kodi utaambiwa hulipi..kumbuka ishu ya star tv aisee
 
Kwa lugha rahisi ni kila mfanyabiashara anajua sio tu JPM atashinda bali atashinda kwa margin kubwa, yafaa nini kupoteza resources zao kwa failure Lissu.

Kwa sababu mwenyekiti na mkurugenzi wa tume ya uchaguzi anawateua yeye, wakurugenzi wa halmashauri na ambao ni wasimamizi wa huo uchaguzi ni makada wenzake na mafuta ya magari yao, anawajazia yeye, polisi ni mali yake!

Kwa nini asishinde! All in all, hakuna lenye mwanzo likakosa mwisho. Mwisho wenu utakapofika, mtaondoka tu. Ila Tanzania itabakia daima.
 
Mkuu usihangaike na hawa wala hawana impact. Wenye tv ni wa kuhesabika ila kila mtu ana simu na mambo yote ya Lissu tunayapata kiganjani. Hawa wala hawatoi msaada wowote hata kwa ccm wenyewe zaidi ya kulinda biashara zao.
 
Nyie si mna social media? Sasa vilio via nini? BTW msisahau kuwaambia social media wawapigie kura pia, ...
 
Aandikwe kwenye magazeti yote na television zote zimwonyeshe mguu Kwa mguu, bado haitasaidia, kwani yupo anayesubiri kuapishwa

Wewe mwenyewe unalo jibu
Hii ni safi sana, unaenda kumuangalia Mgonjwa anayesubiri operesheni kubwa ya kichwa alafu anakwambia "waambie wanaodhani nitakufa kuwa nitapona ndani ya wiki moja na nitarudi kwenye shughuli zangu kama kawaida" ni maneno yaliyojaa ujasiri mkubwa, na si busara kama utaanza kuangusha machozi mbele yake.
 
Wajiuluze kiwa Makonda aliyewatisha yuko wapi sasa?
 
Hivi chadema mpaka leo hamna TV yenu ?,mtalalamika mpaka lini?,washenzi nyie wategemea cha ndugu
 
Boss hawa mbona dawa yao ndogo saana ni kuacha kununua magazeti yao nakuangalia TV zao...Sie mbona wengi wetu siku hizi tumeacha ukitaka taarifa za siasa wewe nunua bando lak la 2500 kwa siku badala ya kununua magazeti matatu ya 3,000 kwanza unakuwa umesave 500/= kuhusu TV kwa hivi sasa hatulipii vin'gamuzi vya azam mpaka hapo mpira utakapoanza kwani ule hauna ccm wala chadema..tutawanyoosha taratibu
 
Back
Top Bottom