Vyombo vya Habari vinacheza Mdumange wa CCM, vyapigwa marufuku kuripoti mapokezi ya Lissu Jimboni

Vyombo vya Habari vinacheza Mdumange wa CCM, vyapigwa marufuku kuripoti mapokezi ya Lissu Jimboni

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2016
Posts
15,835
Reaction score
23,776
MALISA GJ

Baada ya Lissu kunusurika risasi 37 na waliompiga, ama kutojulikna , na baadaye kupokwa ubunge wake, na pia kunyimwa matibabu na mafao yake, na watu ambao wana majina ya watakatifu , "Yoana Nduguwai" na "Yohana Alcohol Padlock" huku wakimtakia kifo, Mungu kamtende miujiza kaibuka mzima na majereaha mwilini.

Wauaji hao ambao hawajulikani "Mungu anawajua" wapo tu wanavuta pumzi huku roho zikiwauma kutokumuua Lissu.

Vyombo vya Habari vya ndani haviripoti habari zake, ITV hawakuweka habari za Lissu alipowasili SINGIDA na kupokelewa na umati wa watu zaidi elfu ishirini.

Nimekuwa nikisoma kwenye vitabu na sasa nashuhudia kwa macho. Uhuru wa habari unakanyagwa na watu hawathubutu kukemea kwa sababu ya HOFU. Vyombo vya habari vilivyoalikwa kuripoti tukio la Lissu kuchukua fomu havijatokea kwa sababu ya HOFU.

Azam wakavuka kiunzi cha HOFU na kwenda kuripoti. Lakini ghafla wakakatisha matangazo na kufuta post zote zinazohusu Lissu kuchukua fomu. Nimeshangaa sana.

Kuna watu wanashangilia kuona uhuru wa habari ukiminywa ili wafurahishe mamlaka. Na wengine wanaogopa kukemea ili nao wasiingie kwenye makucha ya mamlaka. Tukifika hapa hakuna aliye salama.

Jana @advocate_jebra alieleza kisa cha Simba na Kondoo. Simba alifungiwa kwenye kizimba kwa siku kadhaa. Akawa anatafuta msaada wa kufunguliwa kwa nje. Kondoo akapita. Simba akamwambia nifungulie naahidi sitakula. Kondoo akamwambia Simba apa, akaapa. Kondoo akamfungulia.

Alipotoka akamrarua kondoo na kutaka kumla maana alikua na njaa ya siku kadhaa alizofungiwa kwenye kizimba. Wanyama wengine wakapita wakakuta Simba na Kondoo wakizozana. Kondoo akajielezea, Simba nae akajielezea. Simba akakiri ni kweli aliahidi hatamla kondoo lakini ana njaa ya siku 3 afanyeje?

Wanyama wote kwa sababu ya HOFU wakaunga mkono maelezo ya Simba kuwa amle tu kondoo, maana alikua na njaa.

Kobe akasema hajaelewa mkasa huo vizuri. Akamuuliza Simba unasema ulifungiwa kwenye kizimba? Simba akajibu ndio. Akamuuliza kipi? Akamwambia kile pale? Akamuuliza mbona kidogo sana? Uliwezaje kukaa humo? Simba akasema nilikuwemo. Kobe akamwambia hebu ingia tuone kama kweli uliweza kuenea humo. Simba akaingia, kobe akafunga komeo kwa nje na kuondoka.

Kobe akawaambia wanyama wenzie. Leo Simba angemla kondoo mngejiona mko salama kwa sababu si nyie mmeliwa. Lakini kesho angepata njaa tena, na hatujui ingekua zamu ya nani.

Ukiogopa kukemea uonevu haimaanishi kwamba upo salama. Inamaanisha umejiweka kwenye hatari zaidi. Leo vyombo vyote vimeungana na mamlaka kuzuia habari za Lissu. Nilipoona Azam wamerusha matangazo nikasema angalau tumempata Kobe wa kuokoa wenzie.

Mara ghafla kobe huyo naye akaungana na wenzie kumtetea Simba amle kondoo. Bila kujua kesho Simba atapata njaa tena na hawajui itakua zamu ya nani.

#Picha kwa hisani ya CHADEMA



a.jpeg
aa.jpeg
aaaa.jpeg
 
Hivi nikweli vimepigwa marufuku au ni wasiwasi wao tu!
Vimepigwa marufuku, unafikiri ilikuwaje Azam wakarusha alafu ghafla wakaanza kufuta posts zote?

ITV hawaripoti kabisa, yaani tuendako huko ni kuangalia BBC na mitandao ya kijamii lakini lazma kuanza kampeni ya kumu-unfollow millard Ayo
 
Jihadharini na Chachu ya Mafarisayo na waandishi.

Hivi yule Mlevi mwenye Chama huku akiwaita wenzake wote kuwa ni wasaliti naye vipi kule Machame hawakumpokea alipotoka Gerezani??
Au hata walipotaka kumvunja mguu ??

Kuonyesha mafuriko ya Lisu ni khari sana kwa CCM.

Ogopa sana Rushwa ya fedha na madaraka.
Mwandishi anaona mwenzake kapata uteuzi naye anaahidiwa kuteuliwa ,kamwe hawezi kuripoti habari tofauti na ya mwenye nguvu ya ulaji.

Katiba inasababisha mtu mmoja anaweza hata kusujudiwa na kutolewa sadaka za kuteketeza kama Mungu mana anashika riziki za mtu yeyeote anayemtaka. Ni katiba ya kimungu ; jambo ambalo hua halimpendezi Mungu kamwe .Ndio maana nchi zote zinazowatukuza watawala kwa kiwango cha miungu hazidumu katika amani zaidi ya kutumia nguvu kubwa.
 
Waandishi wa habari nao ni watu.

Chama kiache ubahili wa kiMbowe wa kubana hela kwa ajili ya chenji ya konyagi.

Chama kiweke fungu la waandishi wa habari.

Wanasiasa wanatafuta maisha na waandishi pia wanatafuta.

Hakuna mtu atajitoa mhanga kuandika habari zinazoweza kumharibia kazi bila kupata angalau posho ya malazi, nauli, hela za chakula za kuachia familia ili hata kama atawekwa ndani familia ipate hata mihogo.

Tusidanganyane CCM na Mwenyekiti wake wamewashika waandishi tangu miaka ya uwaziri. Waandishi ndani ya CCM Uhakika wa kula upo. Vyombo binafsi vibajiendesha kwa fedha wanazopata wanapopata matamasha au matangazo. Hakuna mtu anayekataa hela hata kwenye mazingira kama ya yuda kumsaliti Mfalme wa Mbingu na nchi, Masihi wa Mungu.
 
Lissu atatoa upinzani mkali kwa Bwana Pombe ila kwa hofu hii iliyotamalaki, sina uhakika kama NEC nao hawatafuata nyayo na kufanya MAGAZIJUTO kwenye kura za urais. Mzee Pombe anataka na kaagiza ushindi mkubwa kuliko ule wa 2015
 
Vimepigwa marufuku, unafikiri ilikuwaje Azam wakarusha alafu ghafla wakaanza kufuta posts zote?

ITV hawaripoti kabisa, yaani tuendako huko ni kuangalia BBC na mitandao ya kijamii lakini lazma kuanza kampeni ya kumu-unfollow millard Ayo
Acha roho mbaya..Millard Ayo unataka afungiwe??..Hivi unadhani ni rahisi tu hivyo,hapa tunatumia fake ID,unadhani tungekuwa na real ID mambo yangekuwa hivi?

Hivi vyombo sio kuwa hawataki kucover habari za wapinzani,ishu ni kuwa maisha yao baada ya kucover yatakuwaje
 
Vimepigwa marufuku, unafikiri ilikuwaje Azam wakarusha alafu ghafla wakaanza kufuta posts zote?

ITV hawaripoti kabisa, yaani tuendako huko ni kuangalia BBC na mitandao ya kijamii lakini lazma kuanza kampeni ya kumu-unfollow millard Ayo

ITV na milliard inabidi wawe hivyo,hawana namna...wasipojikomba watapotezwa

Ni hapa jf pekee tunanena...huku kitaa ni kimya kimya...ni kula na kipofu
 
Waandishi wa habari nao ni watu.
Chama kiache ubahili wa kiMbowe wa kubana hela kwa ajili ya chenji ya konyagi.
Chama kiweke fungu la waandishi wa habari.
Wanasiasa wanatafuta maisha na waandishi pia wanatafuta.
Hakuna mtu atajitoa mhanga kuandika habari zinazoweza kumharibia kazi bila kupata angalau posho ya malazi, nauli, hela za chakula za kuachia familia ili hata kama atawekwa ndani familia ipate hata mihogo.
Tusidanganyane CCM na Mwenyekiti wake wamewashika waandishi tangu miaka ya uwaziri. Waandishi ndani ya CCM Uhakika wa kula upo. Vyombo binafsi vibajiendesha kwa fedha wanazopata wanapopata matamasha au matangazo. Hakuna mtu anayekataa hela hata kwenye mazingira kama ya yuda kumsaliti Mfalme wa Mbingu na nchi, Masihi wa Mungu.
Kaka habari zinauzwa, hazinunuliwi! Habari ikiwa na coverage kubwa inapata matangazo mengi na kwa rate ya juu sana. Hapa anaekosa zaidi ni Media za Tanzania na kuwanufaisha BBC. Ndio maana hata uzalishaji wa magazeti umepungua!
 
itv na milliard inabidi wawe hivyo,hawana namna...wasipojikomba watapotezwa

ni hapa jf pekee tunanena...huku kitaa ni kimya kimya...ni kula na kipofu
Umeeleweka ila Nyerere angekaaa kimya leo ungekuwa unawachamba makalio wakoloni kule Masaki.
 
Acha roho mbaya..Millard Ayo unataka afungiwe??..Hivi unadhani ni rahisi tu hivyo,hapa tunatumia fake ID,unadhani tungekuwa na real ID mambo yangekuwa hivi?

Hivi vyombo sio kuwa hawataki kucover habari za wapinzani,ishu ni kuwa maisha yao baada ya kucover yatakuwaje
Mimi natumia cheo changu na siyo feki kama unavyoita, lakini Nyerere angefanya utakavyo leo tungekuwa na uhuru?

Shule ya kata uliyosoma, hukusoma kitabu kinaitwa "GRAIN OF WHEAT"? mbegu lazma ife ili ichepue, utakufa wewe wanao wataishi!

Martin Luther aliuawa wamarekani weusi wakapata ukombozi kidogo.
Flyofd ameuawa ukombozi unazidi, nyie wazaramo mnatuangusha sana hapa nchi
 
Kaka habari zinauzwa, hazinunuliwi! Habari ikiwa na coverage kubwa inapata matangazo mengi na kwa rate ya juu sana. Hapa anaekosa zaidi ni Media za Tanzania na kuwanufaisha BBC. Ndio maana hata uzalishaji wa magazeti umepungua!
well said, Habari inataftwa kwa gharama zozote ila huyo MATAGA hajielewi kabisa, BBC na jf ndio vyombo namba moja kwa sasa hapa nchini kutupatia habatoi za kweli na uhakika
 
Back
Top Bottom