Vyombo vya Habari vya Kimataifa vinapata faida gani kuzusha uongo kuihusu Tanzania na Rais Magufuli ?!. Angalia uongo/uzushi wa The Guardian la UK!

Na wewe unaweza kuthibitisha kwamba korona imekwisha?

View attachment 1461767


View attachment 1461768

View attachment 1461772
Siwezi kukuthibitisha kwa sababu moja kubwa : Corona bado ipo nchini...serikali imesema hivyo kwamba Corona bado ipo ingawa maambukizi yamepungua...Rais amesema tuendelee kuchukua tahadhari na kwamba Corona bado ipo...Waziri Mkuu naye amesema hivyo hivyo...wewe mwenzetu utuambie hapa. Je umesikia wapi kuwa Corona imekwisha TZ...ni Nani alisema hivyo?
 
Mkuu hii ni karne ya 21....Vita za karne hii nyingi Syo za mtutu.....
Vita za Sasa hivi n Vita za propaganda,Vita za upotoshaji,biological warfare mfano:korona....Vita za media,cyber war ,Vita za kisiasa na nyinginezo nyingi unazozijua czizohusika kutumia mabomu,wala bunduki.....

Katika Vita zote hizi taaifa moja linaweza kupgana na jingine kwa madhumuni Yale Yale...Kama ya Vita ya mtutu.....


Mfano:Vita ya propaganda ambayo inafanywa na Western media....
Lengo n kudhoofisha serikali ya nchi fulan kwa kuptia propaganda za uongo hivo kuathiri uchumi,siasa,n.k

Kumuweka kiongoz wanaomtaka wao kwa kutumia kuwalisha wananchi uongo juu ya chama au kiongoz mwingine .....so ukiangalia madhara na malengo n Yale Yale tu ya vita za mabomu na mtutu
 
Mimi nimehasabu tu "Hii ni kweli " Zimezidi "Huu ni uongo " Imetosha kunipa picha kamili

Hivyo za kuambiwa changanya na zako
 
This is sarcasm, right??
Mkuu P, hii ni fasihi, wachache tumeelewa.

Everyday is Saturday........................ 😎
 
kufurahisha katika hili ni TE="Pascal Mayalla, post: 35511665, member: 17813"]
Wanabodi,

Wanabodi, kila nipatapo fursa huwa ninawaletea makala ndefu za Kwa Maslahi ya Taifa, hivyo leo nimepata fursa tena naendelea na zile makala zangu za kuhamasisha uzalendo kwa jina la "Kwa Maslahi ya Taifa" ambazo zinaendeshwa kwa mfumo wa maswali, leo nazungumzia media za kimataifa zinafaidika nini kwa kuzusha uongo kuihusu Tanzania?, na hawa sources wao ambao ni Watanzania wenzetu, wanafaidika na nini kwa kuwa feed info za uongo, uzushi au kubuni?, what do they stand to gain?. Kuzusha uongo dhidi ya taifa lako na viongozi wake kwenye media za mabeberu ni uzalendo?!.

Ni muda mrefu baadhi ya vyombo vya habari vya kimataifa zikiwemo TV, Majarida na Online contents zao kutunga maurongo kuihusu Tanzania kumkashifu au kukashifu hatua mbalimbali zinazochukuliwa na rais Magufuli, katika maendeleo ya Taifa letu Tanzania, wao watabeza, watakashifu na sometimes hata kumtukana rais wetu, swali la kujiuliza ni vyombo hivi, vinapata faida gani kwa kututungia uongo au kutuzushia na kumzushia rais wetu Magufuli tuhuma za uongo?. What do they get or what do they wish to achieve?.

Katika janga hili la Corona, rais wetu Magufuli anasifiwa duniani kote kwa hatua alizochukua kupambana na Corona, ikiwemo kugomea lockdown, sasa hebu soma makala hii ya gazeti la The Guardian la Uingereza, jinsi ilivyo shehenezwa mauongo na mauzushi kuihusu Tanzania na rais wetu Magufuli!.
Tanzanian president accused of covering up Covid-19 outbreak

Wakati serikali yetu imetoa idadi ya vifo ni kwa huku Tanzania bara ni vifo 16 tuu, na walioambukizwa ni watu 489, hawa jamaa kupitia source wao, wanadai eti Tanzania inaficha idadi ya vifo na maambukizi ya Corona, wandai kuwa wao wameambiwa na source wao kuwa watu waliokufa kwa ugonjwa wa Corona kwa Dar es Salaam tuu pekee ni zaidi ya watu 400!, huku watu zaidi ya 20,000 wameambukizwa nchi nzima!. Huu ni uongo kabisa!, kama serikali yetu imesema waliokufa ni watu 16, then ukweli wa waliokufa ni 16, sasa hiyo idadi ya uongo na uzushi wanaipata wapi na kwa uongo kama huu una malengo gani?, wanapata faida gani kwa kuzusha uongo mkubwa kama huu?!.

Kwa faida ya wale wavivu kufuata links, nakuwekea makala yote, nikiainisha nini ni kweli, nini ni uongo na nini ni uzushi,
Coronavirus outbreak
Tanzanian president accused of covering up Covid-19 outbreak
John Magufuli has repeatedly played down the threat from the pandemic
Jason Burke Africa correspondent
Wed 27 May 2020 17.43 BSTLast modified on Wed 27 May 2020 19.45 BST




My Take
Hawa jamaa wanapata nini kwa kutuzushia uongo?. What do they stand to gain?. Na nyinyi Watanzania wenzetu mmafaidika na nini kwa kuwa vibaraka wa mabeberu na kutunga uongo kuhusu nchi yenu?!.
Uzalendo wenu uko wapi?.

Nawatakia Alhamisi Njema


Cha kufurahisha katika hili ni kwamba hata serikali yetu inapewa misaada na hao hao mabeberu. Nafikiri ukinzani wa mawazo ndio hufanya nchi ipige hatua. Ila kama tunao watu wasio na uchungu na taifa letu hawafai hata chembe ndogo ya haradali
 
Tuonyeshe hayo makaburi ya watu 400 wanaosemekana wamekufa Dar es Salaam...pia tuthibitishie hayo maambukizi ya watu 20,000
Tukubaliane mimi na wewe jambo moja nitaenda kukuonyesha hizo nyumba za Milele na wewe unionyeshe na unithibitishie wagonjwa wa korona wapungua sitaki takwimu za uongo za kina jiwe.Here we have an accord.
 
Tukubaliane mimi na wewe jambo moja nitaenda kukuonyesha hizo nyumba za Milele na wewe unionyeshe na unithibitishie wagonjwa wa korona wapungua sitaki takwimu za uongo za kina jiwe.Here we have an accord.
Mimi kuthibitisha Hilo ni Jambo rahisi kabisa....watu wanachapa kazi Kama kawaida...tikienda hospitali hatuoni wagonjwa wa Corona..mtaani kwetu hakuna aliyekufa kwa Corona....Sasa weee tuthibitishie hao watu 400 mnaosema wamekufa kwa Corona hapa TZ.
.tupatieni mchanganuo kuhusu vifo hivyo na hospitali walikokuwa na Kama baadhi wamefia majumbani tutajieni mitaa vijiji wilaya na mkoa...halafu ikibidi myuonyedhe makaburi hayo...na kuhusu maambukizi ya watu hao 29,000 tupatieni pia m hanganuo wake Dar es salaam wangapi na walioko huko Kila mkoa...
 
1)Wagonjwa wa korona hawawekwi alama mpaka utambue hawa ni wagonjwa wa korona.

2)watu kuchapa kazi haimaanishi kuwa korona hamna.

3)kutokufa kwa mtu mtaani kwenu hakumaanishi korona haipo.

4)umetembelea hospitali ngapi mpaka uhitimishe mahospitalini hakuna wagonjwa wa korona,kwa kifupi uthibitisho wako umeegamia kwenye hotuba ya jiwe umekopi mpaka hata maneno ya jiwe(kuchapakazi) bila hata kuyahariri.

5)- itakuja baadae baada ya iftar

Kwa kuwa uthibitisho wako ni wenye mashaka na usio na mashiko,siwezi kuandamana na wewe kwenda kukuonyesha hizo nyumba z milele walimopumzika hao waliopumzishwa na COVID 19
 
You people you are just contradicting yourselves.....Sasa Kama wagonjwa wa Corona hawana alama hizo takwimu za mambukizi kwa watu 20,000 na vifo 400 zimekujaje?
Hakuna kiongozi yeyote wa serikali aliyesema Corona haipo...Rais amesema Corona ipo Ila imepungua na tuendelee kuchukua tahadhari...
Nyie pamona na mabeberu mmekazana Corona ipo kwa wingi na watu wanakufa kwa mamia...Sasa sisi tunasema tuthibitishieni idadi au takwimu zenu..mmebaki mnazungumsha macho tu..Mtu ukiwa mtumwa kwa mabeberu ni taabu Sana...Sijui mnataka Nini...ok...tuseme wamekufa watu 400 na mambukizi ni watu 20,000 kwa hiyo nyie ndugu zetu na mabeberu wenu mnasemaje? Yaani tuseme hizo takwimu za vifo na maambukizi zilizopikwa zinawafurahisha kwa kuwa zinaonyesha vifo vingi na maambukizi makubwa?




..
 
Wanabodi, mimi ni miongoni mwa wana jf, tuliandika mengi kumhusu rais wetu, Dr. John Pombe Joseph Magufuli, hivyo kipindi hiki cha maombolezo, napitia baadhi ya mabandiko kwa ajili ya kumuaga rasmi.

Japo umetangulia, lakini kauli zako, maono yako na kile ulichokiamini, kitabaki na sisi Milele.
Sisi tulikupenda, lakini Mungu amekupenda zaidi.
Bwana Alitoa, Bwana Ametwaa, Jina Lake Lihimidiwe!.
Raha ya Milele Umpe Ee Bwana, na Mwanga wa Milele, Umuangazie, Apumzike kwa Amani...Amina x3.
RIP Dr. John Pombe Joseph Magufuli
Buriani ya kuonana...
Paskali
 
Amina.
 
Kuna wanasiasa wawili wanafahamika hasa zitto ndio wanawashwa kuichafua Nchi ila hawatafanikiwa
wafanikiwe mara ngapi ndo uamini kuwa wamefanikiwa???...jiwe kwishneeeee mpaka legacy yake inakufa..Rais wa kwanza kufa ajili ya ubishi kwa afya yake!
 
wafanikiwe mara ngapi ndo uamini kuwa wamefanikiwa???...jiwe kwishneeeee mpaka legacy yake inakufa..Rais wa kwanza kufa ajili ya ubishi kwa afya yake!
Jiwe bado anazungumziwa kama vile bado yupo hai, hatuoni Mkapa au Maalim seif kuzungumziwa zungumziwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…