Vyombo vya habari vya kimataifa vyatahadharisha kuwa Tanzania yaweza kurudi kwenye uvunjifu wa haki na uhuru wa kujieleza

Vyombo vya habari vya kimataifa vyatahadharisha kuwa Tanzania yaweza kurudi kwenye uvunjifu wa haki na uhuru wa kujieleza

fazili

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2011
Posts
16,427
Reaction score
22,418
Vyombo vya habari vya kimataifa kutoka Africa na nje ya bara la Africa vimeonesha wasiwasi kuwa Tanzania inaweza kurudi nyuma katika masuala ya haki, uhuru wa kujieleza na demokrasia.

Hayo yamesemwa kufuatia hotuba ya rais Samia kwenye maadhimisho ya miaka 60 ya Jeshi la Polisi Tanzania yaliyofanyika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro mapema wiki hii.

Katika hotuba yake rais Samia alionesha kuchukizwa kwake na jinsi vyama vya siasa, vyama vya kutetea haki za binadamu na balozi za nchi za Ulaya na Marekani zilivyokuza habari za utekaji na mauaji ya baadhi ya watu nchini.

Katika hotuba yake rais alivitaka vyombo vya kimataifa viache Tanzania ijiamulie mambo yake kupitia katiba halali iliyopo.
 
Kwaambali EU na Nyundo kubwa ikumbukwe shilingi yetu inazidi kuporomoka ...exchange rates USD
 
Kule US wale waandamanaji waliokua wanapinga mauaji ya Gaza,mbona walikua wanapigwa na kukamatwa?
Huko hakuna uhuru wa kujieleza?
 
Kwaambali EU na Nyundo kubwa ikumbukwe shilingi yetu inazidi kuporomoka ...exchange rates USD
Jamani Chura kiziwi hana Cha kupoteza yeye tayari ni mzee wakati wowote anaaga ameshatengenezea wanawe n ndg zake utajiri mkubwa Sana
 
4Rs zinafanya kazi huko si rahisi labda waongo waendelee kumdanganya Rais Samia kwa kumjaza uongo na achelewe kuwagundua na njama zao za uongo.
 
Back
Top Bottom