Vyombo vya usafiri vinavyoongoza kwa vurugu barabarani

RRONDO

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2010
Posts
55,727
Reaction score
123,094
1.bodaboda-hawa bangi na viroba huenda vinawapeleka mbio
2.bajaj-hawa nao kama bodaboda tu
3.daladala-hawa nao bangi na viroba vinawakimbiza kusaka hesabu
4.Subaru,Altezza-wazee wa ligi na kelele
5.taxi zenye mistari
6.vigari vidogo ist,Passo etc hawa sijui shida ni nini
7.vyombo vyenye namba zinaanzia ST,PT,UT,DFP,SU, hawa wanahisi wako juu ya sheria wanasahau wakipiga mzinga maumivu hayajui wewe ni nani
 
Hii list imekamilika, no 6 wanavunja mno sheria hata wapate ajali hawatakaa wabadilike!
No 5. Udogo wao unawafanya wawe na fujo zaidi maana kanafasi kadogo tu kanamtosha hivyo inakuwa rahisi kuchomekea mara kwa mara.

No 3,2,1, huu ni ugonjwa nahisi tiba yake walipaswa wawe na line yao inayojitegemea pembeni huko ili wakaparuane wenyewe kwa wenyewe.😂🤣😂🤣
 
Inategemea. Kwa mjini hapa bodaboda na bajaji na PT ndio wenye fujo.

Ila kwenye highway za mikoani aisee ogopa sana ST SU. Hawa jamaa ni nini sijui kinawapataga wakishavuka mlandizi. DFP na CD aanakimbia yes but angalau wanajali watumiaji wengine wa barabara I guess kwasababu kuna mkono wa wazungu. Ila ST na SU wakianza kuovertake wanatoka wote kazi kwako unayekuja uwapishe.
 
Unawahau Malori ya mchanga....
Hawq wanakupigia mihoni puuuuuuuuu pooooio poooooo
Unawasahau watembea kwa miguu hawa nao wanakera hatari
Malori wastaarabu sana, wangekuwa kama bodaboda au bebi woka tungekufa sana
 
Unawahau Malori ya mchanga....
Hawq wanakupigia mihoni puuuuuuuuu pooooio poooooo
Unawasahau watembea kwa miguu hawa nao wanakera hatari

Hahaha yani mtembea kwa mguu anakutaka wewe ndio uwe makini yeye hajali gari iko speed anataka avuke, apite pembeni ya barabara kama konokono wewe ndio umkwepe doh! Ajabu ikiwa sehemu kuna kidimbwi cha maji wanakuwaga makini ili tu asimwagiwe maji!
 
CD kidogo wastaarabu
 
Hahaha yani mtembea kwa mguu anakutaka wewe ndio uwe makini yeye hajali gari iko speed anataka avuke, apite pembeni ya barabara kama konokono wewe ndio umkwepe doh! Ajabu ikiwa sehemu kuna kidimbwi cha maji wanakuwaga makini ili tu asimwagiwe maji!
Wavumilieni watembea kwa miguu
 
 
CD kidogo wastaarabu
Very much so hata wakiwa highways. Powerful cars ila wanaendesha vizuri.

Mimi nikisafirigi na pikipiki watu wananiulizaga kama siogopi mabasi na malori. Nawaambiaga hao hawana shida sana, nikija kubutuliwa probably itakuwa ni ST SU. Maana nikiwa upande wangu wao ni kama wanaona pako wazi tu, piga honi vipi piga pass vipi hawaelewi wala hawaombi, hawaangalii upana/ubovu wa barabara au kama ni daraja wao wanatoa gari mpaka mstari wa njano wa upande wangu kunilazimisha mimi nikimbie barabarani kuwaacha wamalize overtake yao.

Tena wakiwa wengi, akitoka wa mbele wa nyuma hawaangalii wanachomoka pia kama manyumbu.
 
Mungu anisamehe ila nikikuta bodaboda zimegongana sisikitiki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…