DOKEZO Vyoo kama hivi kwenye Mabasi ya Luxury ni kinyaa na hujuma kubwa

DOKEZO Vyoo kama hivi kwenye Mabasi ya Luxury ni kinyaa na hujuma kubwa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2021
Posts
590
Reaction score
1,648
Wakuu,

Mtu analipia basi luxury kupata huduma extra, nzuri na bora, asafiri akiwa anajisikia huru. Inakuaje unalipia kusafiri basi luxury halafu unakutana na choo kama hiki? Choo hiki ni kwa huduma ya haja ndogo pekee na hauruhusiwi kuingiza tishu/toilet paper na haiwekwi kabisa chooni lakini unaruhusiwa Kwenda na yako, ukitakiwa kuiweka kwenye chombo cha taka chooni humo.

Choo hakina maji, koki haifanyi kazi kama mnavyoona kwenye picha, mlango ni wa kujiegesha; yaani inabidi uushikilie muda wote ambao unatumia choo hiko la sivyo unaweza kufunguka muda wowote wakati unafanya mada zako ukaaibika. Na kutokana na Malalamiko ya watu huduma hii iko hivi muda mrefu, sasa abiria wanalipia pesa ya luxury ya nini kama huduma haziboreshwi?

Mmewafikiria wanawake kwenye huduma hii? Wanawake hasa wakiwa katika vipindi vyao mwezi wanahitaji sana kuwa na maji kwenye huduma ya choo. Sasa ndio yuko kwenye kipindi chake akaenda kutumia hiko choo kuna usalama hapo?

Ni uchafu wa hali ya juu, unaingia mzima unaondoka na U.T.I sugu

Choo katika Basi la Kidia One Express wanakutoza Tsh. 45,000/- kwa huduma ya luxury

kid3.jpg
kid2.jpg
kid1.jpg
kid.jpg

Kwa wenye uzoefu na mabasi Luxury/V.I.P kutoka kampuni nyingine hali ikoje?
 
Kila jambo linaweza kuwa geni mwanzoni, ila kadri siku zinavyosonga wanaweza kupata namna ya kuboresha.

Muhimu wazingatie usafi kadri mtu anavyotoka msalani basi mtu wa usafi aende kuweka sawa mazingira ikiwemo kutumia kemikali za kuua vijidudu kama ilivyo kwenye Vyoo vya kwenye ndege.

All in all tuwapongeze hayo makampuni ya mabasi yanatoa huduma za Choo ndani ya basi kwani yanasaidia kutunza muda lakini pia afya za wasafiri hasa wenye matatizo ya kibofu cha mkojo. Kuna watu hawawezi kuhimili kukaa masaa 3 bila kwenda haja ndogo.

Kuna mwaka tulisafiri na basi la kampuni fulani, sasa bahati mbaya kuna Dada alishikwa na Tumbo la kuhara siku hiyo

Bila kujali usalama wake pale Mikumi National Park aliomba ashuke kwaajili ya kuweza kujisaidia.

Hata maji ya kuweza kujisafisha alikosa, ikalazimika Wamama na Wadada wenye tissue wamsaidie.

Kwahiyo taratibu tutafika huko unapotamani kufika, ila hii ni hatua kubwa ya kupongeza kuweza kupata huduma za Choo ndani ya Basi
 
Kila jambo linaweza kuwa geni mwanzoni, ila kadri siku zinavyosonga wanaweza kupata namna ya kuboresha.

Muhimu wazingatie usafi kadri mtu anavyotoka msalani basi mtu wa usafi aende kuweka sawa mazingira ikiwemo kutumia kemikali za kuua vijidudu kama ilivyo kwenye Vyoo vya kwenye ndege.

All in all tuwapongeze hayo makampuni ya mabasi yanatoa huduma za Choo ndani ya basi kwani yanasaidia kutunza muda lakini pia afya za wasafiri hasa wenye matatizo ya kibofu cha mkojo. Kuna watu hawawezi kuhimili kukaa masaa 3 bila kwenda haja ndogo.

Kuna mwaka tulisafiri na basi la kampuni fulani, sasa bahati mbaya kuna Dada alishikwa na Tumbo la kuhara siku hiyo

Bila kujali usalama wake pale Mikumi National Park aliomba ashuke kwaajili ya kuweza kujisaidia.

Hata maji ya kuweza kujisafisha alikosa, ikalazimika Wamama na Wadada wenye tissue wamsaidie.

Kwahiyo taratibu tutafika huko unapotamani kufika, ila hii ni hatua kubwa ya kupongeza kuweza kupata huduma za Choo ndani ya Basi
Havina tofaoti na vioo via kwenye treni
 
Hivi kule ndani kuna mkanda wa kuvaa ukiwa unajisaidia?maana nawaza kama basi likiingia kwenye shimo au road bump shughuli yake si itakuwa ni hatari sana.Tena kuna mtu aliwahi kuniambia ukikaa karibu na hicho choo harufu inayotoka huko ndani ni kali sana,hii naona inasababishwa na kukosa maji...
 
Hata mabus ya BM ya Dar-Dodoma yale yenye namba zile series za DRL yana vyoo vichafu havifai. Unaweza kuingia ukakuta vimefurika yaani mikojo imejaa hata kukojoa unaona kinyaa, mara nyingi vinanuka havifanyiwi usafi mara kwa mara. Nadhani ndiyo maana Shabiby hizi bus zake mpya ECH ameamua kuondoa vyoo ndani ya bus maana utunzaji ni changamoto kwetu sisi rangi nyeusi.
 
Karibu Gari za Tilisho. Vyoo vyake ni Visafi na Wahudumu wanakaa Jirani na vyoo kukuelekeza. Ila hawatumii Dabuni ya Dettol maybe kuzuia Ile harufu yake kusambaa Garini
 
wewe
Wakuu,

Mtu analipia basi luxury kupata huduma extra, nzuri na bora, asafiri akiwa anajisikia huru. Inakuaje unalipia kusafiri basi luxury halafu unakutana na choo kama hiki? Choo hiki ni kwa huduma ya haja ndogo pekee na hauruhusiwi kuingiza tishu/toilet paper na haiwekwi kabisa chooni lakini unaruhusiwa Kwenda na yako, ukitakiwa kuiweka kwenye chombo cha taka chooni humo.

Choo hakina maji, koki haifanyi kazi kama mnavyoona kwenye picha, mlango ni wa kujiegesha; yaani inabidi uushikilie muda wote ambao unatumia choo hiko la sivyo unaweza kufunguka muda wowote wakati unafanya mada zako ukaaibika. Na kutokana na Malalamiko ya watu huduma hii iko hivi muda mrefu, sasa abiria wanalipia pesa ya luxury ya nini kama huduma haziboreshwi?

Mmewafikiria wanawake kwenye huduma hii? Wanawake hasa wakiwa katika vipindi vyao mwezi wanahitaji sana kuwa na maji kwenye huduma ya choo. Sasa ndio yuko kwenye kipindi chake akaenda kutumia hiko choo kuna usalama hapo?

Ni uchafu wa hali ya juu, unaingia mzima unaondoka na U.T.I sugu

Choo katika Basi la Kidia One Express wanakutoza Tsh. 45,000/- kwa huduma ya luxury


Kwa wenye uzoefu na mabasi Luxury/V.I.P kutoka kampuni nyingine hali ikoje?
wewe kunya halafu usepe
 
Back
Top Bottom