Waafrika hadi sasa tunashindwa nini ku-document dini zetu kama waarabu, wahindu, wajapan, Wachina, wayahudi?

Sasa kwa nini Mungu asiwafungulie neema wamjue, badala yake anawaziba macho na masikio na kuifanya mioyo yao iwe mizito?

Kitendo cha Mungu kuingilia kikizidisha uwezekano wa hawa watu kutomjua Mungu lawama ni kwao au kwa Mungu?
 
Sasa kwa nini Mungu asiwafungulie neema wamjue, badala yake anawaziba macho na masikio na kuifanya mioyo yao iwe mizito?

Kitendo cha Mungu kuingilia kikizidisha uwezekano wa hawa watu kutomjua Mungu lawama ni kwao au kwa Mungu?
Ndiyo kama nilivyokujibu hapo awali kwamba walishapewa ujumbe wakumjua Mwenyezi Mungu wao lakini walichupa mipaka kutokana na viburi vyao. Walionyeshwa kila aina ya ishara lakini wao walikuwa wanaleta mzaha.
Bahati ya kumjua Mwenyezi Mungu walipata kutoka kwa mtume mwenyewe.
 
Dini sahihi ni dini ya Allah (SWT), dini ya kiisilamu, full stop.
Wewe mtu, amka hapo usingizini. Wengi tulikuwa kama wewe lakini tukapata muda wa kujitafakari na kugundua hizi imani ni mipango ya watu tu, ivi ushawahi jiuliza kwanini kila imani inavutia kamba kwake?
Yaani ukiyafatilia mafundisho ya imani zote ni mazuri tena yanakushawishi kuamini kuwa imani hiyo ndio yenyewe, lakini je! Mungu kaziweka hizo imani zote? Jibu litakuwa hapana kwamaana mungu anayesemekana kuwa na hekima asingeweza kuweka utitiri wa dini nyingi ambazo kila dini inapinga nyingine.
Katika hayo yote tutakubaliana kuwa dini zote ni uzinguaji tu, ni mawazo ya binadamu tu yaliyobuniwa kuwa kama njia ya kumtafuta mungu wa kufikirika.
AMKENI japo huo usingizi ni mtamu. Tafuteni muda wa kuzihoji hizo dini zenu sio kila unachoambiwa kuhusu dini yako unakubaliana nacho hata kama kinakupa ukakasi.
 
Dini zetu si ndio huu Uchawi tulionao wenzetu wa Afrika ya Magharibi wamejitahidi kuendelea na Voodo yao

Sisi huku Afrika ya Mashariki inatubidi nasi tuhalalishe
Kuna mda flan sku ya jana nlikua nafikiria kwamba " labda uchawi n kitu kzuri lakn wazungu walivokuja na dini zao wakaanza kusema mabaya juu ya uchawi". Mfano,katika biashara mtu akifankiwa utaskia et anatumia uchawi ina maana uchawi una nguvu zaid. Au kwenye siasa utaskia fulan karoga iili apate ubunge.

Nategemea kufanya research nijue n kwa nn wakoloni walitumia nguvu nyng sana kuuponda uchawi??? Kwa nn walitumia nguv nyng sana kusambaza dini zao?? Mda mwngne ukigoma kuamin wanakuua why??

Sometimes nafikiriaga huenda wazungu nao n wachaw (lakn kwa kuwa uchawi wao wameu document ndio mana tunaona ktu cha kawaida) mfano ndege inapaa ,whatsapp videocall, hv vtu vingefanywa na mwafrika tungeambiwa n uchawi lakn kwa kua kafanya mzungu bas tunaambiwa n technology.

In short hua nafikiria kwamba "wazungu wameficha uchawi wao kwny mwamvuli wa technolojia"
 
Hii imesababishwa na wazungu wame brainwash akiili zetu. Walituaminisha kua kitu chochote cha Africa n kibaya na dhaifu.
 
Huko Benin Serikali yao na Katiba yao zinaamini Uchawi lakini ndio Masikini sana katika Afrika
 

Kulazimishwa kuingia dini ya Mzungu huku kwetu ZANZIBAR haijakuwepo tafauti na bara lote la Afrika. Ila wazee walichukua tahadhari na ilikuwa hawapeleki watoto wao maskuli kwa kukimbia kile walichokuwa wakiita UKAFIRI, ndio hiyo dini ya Wazungu.

Na ilikuwa watoto wakipelekwa madrasa tu kusoma na kuijua dini yao hii ikiwa ni pamoja na Qur’an Takatifu.
 
mungu huyo unayemzungumzia ana ujuzi wote na uwezo wote?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…