Waafrika na suala la ubaguzi na ukatili katika soka

Waafrika na suala la ubaguzi na ukatili katika soka

Hawa ndio wa kuwashangilia.👇
 

Attachments

  • Screenshot_2022-12-16-21-26-44-386_udaku.special.app.jpg
    Screenshot_2022-12-16-21-26-44-386_udaku.special.app.jpg
    219.7 KB · Views: 6
Wamekataa wenyewe tena kwa sauti kubwa.Mtuache na mizimu na machawi yetu halafu mfikirie na namna ya kuachana na maliasili zetu.wafirwaji ninyi.
 
Sijui umeielewa mada vizuri! Nani kaumia hapo! Siwezi kuumia ama kuteseka sababu sina chuki na mtu.
Sasa kama hujaumia ama kuteseka! Na huna chuki na mtu! Hiyo nguvu ya kupangia watu maisha unaitoa wapi?

Kwani lazima kila mtu ashabikie Morocco na Misri? Mimi nadhani kila mtu angeishi maisha yake. Kama kuna mtu amechagua kuishabikia Senegal, Ufaransa, nk. Muache!

Na wewe shabikia timu unayoipenda, na hakuna atakaye kulazimisha ushabikie timu nyingine.
 
Mleta mada sidhani kama unawafahamu vizuri Morocco; wanayo yasema raia wa nchi hiyo kuhusu Africa siyo kwa bahati mbaya. Soma historia ya mahusiano ya Morocco na the rest of Africa utaelewa. Huu ujunga wa Morroco huwezi kuukuta Algeria wala Egypt. Binafsi nilidhani Morocco wamejifunza madhara ya kujitenga na Africa kumbe bado. Ipo siku watazijutia sana kauli hizi
 
Afrika itabaki kuwa Afrika tu, hususani hapa Tanzania. Nimefuatilia katika social media's za bongo, aise ni kama vile walikua wanatafuta vijisababu kutoka kwa hawa ndugu zetu Waarabu (Morocco) ili wapatiamo cha kusema/kuwatukana na kulialia.

Unakuta mwanaume mzima anawakandia wanaume wa Morocco, huyo huyo anaejiita mwanaume anawashabikia ufaransa wanaopromoti ushoga, huyo huyo anaejiita mwanaume anashabikia timu sababu ina weusi.

Unaacha kushabikia Waafrika wenzio unashabikia Wazungu, eti kwa sababu ina mchanganyiko na wasaliti walio ukana uraia wao! Waafrika wengi wao wana tabu mno, ALEYOMBBA GEKKE waafrika wengi wao wana tabu, sio ubaguzi tu bali na ukatili pia tunao. Naomba nisieleweke vibaya👉watu weusi wengi wao ni wabaguzi, wakatili na wanaroho mbaya. Tujirekebishe.

Na nimekuja kuamini haya, that day walipokutana Egypt na Senegal asilimia kubwa ya mashabiki wa Kibantu walikua upande wa Senegal. Leo hii anakuja Mbantu kulialia ya Morocco lakini hakumbuki ya Egypt na Senegal n.k.

Kwani Morocco wana kosa gani? Si wanapigania nchi yao? Hapo kosa lipo wapi? Wao wapo kwa ajili ya nchi yao na watu wao, lakini kuna wabantu wanalialia. Tuacheni ubaguzi.

So, hapa nachoona, kinachoangaliwa ni rangi especially waarabu, watu ambao walibarikiwa, mtawachukia, mtawabagua na kuwasema vibaya lakini hakibadiliki chochote dhidi yao, watabaki kuwa watu wakarimu, wana imani, na wavumilivu kwa haya wanayopitia kutoka mataifa ya magharibi na kwa baadhi ya Wabantu tunaoishinao huku.

God bless Arabian countries, awaongoze, awalinde, na Allah aendelee kuwapa subira na haya wanayopitia. Wale wanaowachukia hawa ndugu zetu, na kuwasusa na kushabikia wazungu, Mungu atawaongoza.

ALEYOMBBA GEKKE, ipo siku mtawakubali tu waarabu.

Mungu awabariki sana hawa ndugu zetu Morocco, mmepigana vyakutosha mpaka semi final wakati wakina Ghana na wenzie walitolewa kwa aibu.

Hakika Morocco ni wanaume na wale wanaodai kuwa ni laana, hizo ni kasumba zenu, ndivyo mnavyokaririshana huko mitaana na vijiwe vya kahawa. Kwa sisi wenye imani zetu upumbavu kama huu haupo, eti hiyo ni laana! Hivi mnaijua laana ninyi!

Sasa tunasubiri hiyooJjumapili hao Wabantu wasaliti mchanganyiko na Wazungu tuwabonde kisawasawa. Sisi wana Argentina tutalipiza kisasi, siku hiyo mtalia sana.

Waabheja sana.
Tuchukulie mfano huu,
Bwana A mwenye rangi maji ya kunde ana wake wa5. Katika hao wake mmoja wao ni mweusi ambapo wengine ni weupe. Katika kuzaa watoto, mke mweusi akazaa watoto mchanganyiko na wengi wao wakiwa weusi na weupe wachache. Sasa swali ni kwamba je ni sawa kwako hawa watoto weupe wa mke mweusi wamkane mama yao kwakuwa wao ni weupe? Je wawakane na ndugu zao wa tumbo moja kuwa sio ndugu zao kwa kuwa wao ni weusi!? Je, hawa wabaguzi waitwe watoto wa mama yupi!? Je ni sahihi wao kumkana mama yao kuwa hawamtambui kama mama yao bali wanaishi kwake tu? Vip kama wewe ndo baba yao utawafanyaje?
 
Tuchukulie mfano huu,
Bwana A mwenye rangi maji ya kunde ana wake wa5. Katika hao wake mmoja wao ni mweusi ambapo wengine ni weupe. Katika kuzaa watoto, mke mweusi akazaa watoto mchanganyiko na wengi wao wakiwa weusi na weupe wachache. Sasa swali ni kwamba je ni sawa kwako hawa watoto weupe wa mke mweusi wamkane mama yao kwakuwa wao ni weupe? Je wawakane na ndugu zao wa tumbo moja kuwa sio ndugu zao kwa kuwa wao ni weusi!? Je, hawa wabaguzi waitwe watoto wa mama yupi!? Je ni sahihi wao kumkana mama yao kuwa hawamtambui kama mama yao bali wanaishi kwake tu? Vip kama wewe ndo baba yao utawafanyaje?
Manyanyaso ambayo waarabu huwa wanapata Ulaya ni ajabu Morocco kujifungamanisha nao kuliko Africa. Kwanza Mzungu anamkubali mtu mweusi kuliko mwarabu na wao Morocco hilo wanalijua kabisa.
 
ILA MOROCCO WAO NDO WALIANZA KUTUKANA SISI AFU KUHUSU KUBARIKIWA HUO NI UONGO WA VITABU TU MBNA TEKNOLOGIA NA SUPER POWER NI MAREKANI NA WAO WAPO TU KUTIA HURUMA?

Sent from my SM-G950U using JamiiForums mobile app
 
Kwahiyo unashabikia timu kwa sababu ina weusi sio, lakini hapo hapo ni kwa faida ya wafaransa na ulaya kwa ujumla sio! Ila waafrika wenzio ukawatosa haijalishi tukonao bara moja!! Sasa huu utasema sio ubaguzi!!

Tukubali tukatae waafrika wanaongoza kwa ubaguzi duniani japo sio wote, mwanzo nilifikiri wahindi ndio namba one, kumbe sivyo nilivyofikiri..


Olenimala nkoi? Au niongee kichina utanielewa!
Namba moja ni waarabu.
 
Morocco wametukana nini na wapi?

Argentina wamewanyamazisha hawa mahaters wa maorocco, jana itakua wengi mno wameumia Argentina kutwaa ubingwa

Asanteni sana Argentina kuwabomoa hao wahaini wa ufaransa.
 
Tuambie sababu ya wewe kuishabikia Morocco na kutokuishabikia Ufaransa, hili jibu litanipa pa kuanzia.

Morocco ni ndugu zetu, na wapo katika bara letu, hivyo lazima niwe upande wao.


Argentina tumemaliza kazi.

God bless Moroccans
 
Back
Top Bottom