Nakupa 10/10.
Kumzindua Mwafrika ni Ibada.
Ni ibada kubwa sana maana Unamtatetea Kiumbe kilichoumbwa na Mwenyezi Mungu. Viumbe vinavyodharaulika. Viumbe vinavyonyanyasika.
Hii ndio lugha zinazotakiwa kuzungumzwa katika mitandao ya jamii katika karne moja inayokuja.
Mwenyezi Mungu hakufanya makosa kumuumba Mwafrika. Na Mwafrika hakuja duniani kupata shida.
Historia inaonyesha "Civilization" imeanzia Afrika. Kusema Mwafrika hawezi ni makosa.
Wazungu ndio wametuigiza Utamaduni wetu. Elimu waliokuwa nayo historia imetokea Afrika. Hizi sio simulizi.
Angalieni Timbaktu, kulikuwa na elimu na maendeleo kabla hata Ulaya hajajulikana. Ndio maana Rais Mstaafu wa Afrika Kusini Bwana Thabo Mbeki katika Utawala wake na harakati zake za kufufua hadhi na utu wa Mwafrika ali "adopt" rasmi Timbaktu na kuahidi kufufua historia yake.
Mifumo inayotawala imetengenezwa kumkadamiza Mwafrika. Fikra zetu zimepigwa mnada na tumewekwa kwenye giza na hawa hawa viongozi wetu wa sasa
Nini maana ya "Mapinduzi", kwanini Mwalim Nyerere alitumia neno hili? Ni neno zito sana. From "Oppression to Liberation", does this word or this theory "Revolution" applies anywhere in Tanzania?? Come back to us with a correct answer and stimulate this debate on a political matured lever and humble African traditional and respected manner.
Mwafrika hana damu ya manjano. Ni Binaadamu kama mtu mwingine.
Mwaka jana, Waafrika wakiwa kwenye mfuko wa bahari huko Afrika Kusini wakati wakisheherekea sikukuu yao ya Krismas. Mama mmoja wa Kizungu ambae yuko katika chama cha Upinzani Afrika Kusini, aliandika kupitia mtandao wake wa "Twiter" kuwa Waafrika waliojazana ufuko wa Bahari ni kama Manyani.
Wazazi wa Kiafrika na watoto wao wanatukanwa.
Atakomboleka tuu Mwafrika.