Waafrika wanalazimisha mafanikio ya Morocco yawe ya Waafrika wote

Waafrika wanalazimisha mafanikio ya Morocco yawe ya Waafrika wote

Kumbe kinachokusumbua ni chuki ya udini? basi endelea tu kuteseka ila tambua kua huna impact yeyote wala huwezi kubadili chochote.

Kinachokusumbua ni ushabiki wa dini ya watu, haya ndio hao wamesema ushindi ni wa waarabu, nyie mnashoboka tu.
 
Wapo barani Africa lakini hawapigani kwa ajili ya Afrika bali ni kwa ajiri ya nchi yao.

Mbona hamtaki kuelewa?

Mbona hayo mambo ya kupambania mabara huwa hatuyasikii kwenye mabara mengine zaidi ya Africa?

Wenyewe wameshasema wanapigana kwa ajili ya nchi yao na nchi za uarabuni na waislamu wao, basi tumekubali.
 
Morocco anaiwakilisha Arab emirates
maana wao walishalambwa vichwa asubuhi na mapema,angalau huyu anaiondolea aibu
 
Kuhusu kuishangalia Morocco huwezi kumpangia mtu aonyesheje furaha yake
Hujamuelewa. Soma upya. Hajasema usishangalie Morocco. Anachopinga kudandia mafanikio kwa kigezo cha uafrika. Kama unaishabikia ishabikie kwa kigezo cha mafanikio yao. Tuache kudandia mafanikio ya watu.
Ndio yaleyale eneo la mtu likipatikana madini serikali inataka yawe ya umma/serikali, mwenye eneo anaishia kupewa fidia na kuhamishwa. Ila eneo hilohilo likiwa halina rutuba unaachwa upambanie kivyako, likiwa na rutuba serikali/jamii hii hapa.
 
  • Thanks
Reactions: ITR
habari ndo hiyo,kila mtu abebe msalaba wake.afanikiwe mwingine kwa juhudi zake alafu mafanikio mnataka mshee wote eti kisa mmetoka kijiji kimoja,kha,,!
 
Sijui ni tumerogwa au haya yote ni sababu ya elimu duni au Mungu ndo alivyo tuumba yaani sijui jamii yetu ya kiafrika ina matatizo gani.

Waafrika ndio jamii pekee ambayo utapambana kwa nguvu zako kusoma kwa shida lakini ukipata kazi wanataka mshahara unao upokea uwe wa ukoo mzima.

Waafrika ndo jamii pekee ambayo utapambana peke yako kutafuta mafanikio kwenye maisha yako saa nyingine kuhatarisha mpaka maisha yako ili ufikie hayo mafanikio , lakini baada ya kupata huo utajiri wana razimisha uwe wa ukoo mzima.

Mfano angalia waafrika wanavyo razimisha mafanikio ya Morocco yawe ya waafrika wote.
Tena unakuta jitu zima ambalo kwa kuliangalia utasema ni jitu lenye akili ,lakini unakuta eti lina lalamika kuhusu kauli iliyo tolewa na naodha wa Morocco aliye sema ushindi wa Morocco ni wa na waarabu eti waafrika wamebaguliwa.

Jamaa aliongea ukweli kwa sababu timu yao imeandaliwa na mpaka sasa inahudumiwa kwa pesa za walipa kodi wa Morocco na si za waafrika ,sema tu waafrika ni jamii iliyo zoea kulalamika hata kwenye mambo ya kijinga

Ww unaye razimisha ushindi wa Morocco uwe wa waafrika wote kwa mchango upi ulio wapa mpaka kufikia hayo mafanikio yao?

Morocco inatumia mamilion ya $ ya kodi za wamoroco kuwekeza kwenye kwenye soka kuanzia kujenga viwanja vya kisasa na akademi ,wakati ss huku Tz viwanja vyote CCM imevingangania wakati hata kuviendeleza imeshindwa.

Kama unaishabikia Morocco ishangilie kwa sababu unapenda inavyo cheza au kuna wachezaji unawahusudi lakini sio kwa sababu uchwara eti ni wawa kilishi wa Afrika, ishabikie kama mnavyo shabikia uhispania, Ujerumani,Ubeligiji ambazo hazina uhusiano wowote na waafrika.

Waafirika ni watu tunao penda kupata matokeo hata kama hatujafanya mtihani.

Unakuta mtu hataki uwepo wa single mother mitaani lakini kwenye uzi wa kula tunda kimasihara ana simulia jinsi ambavyo ameshala kula mabinti zaidi ya 7 kimasihara tena bila kondomu.

Waafrika tuache unonko tufanye mambo yetu sisi kama sisi tuache tabia ya kijishikiza nyuma ya jamii nyingine kwa vigezo uchwara.
Kwanza uweze kwanaza kutofautisha "r" na "l" ndio urudi kuandika upya. Huu ni upoyoyo. Hata waarabu wala waislamu duniani hawakuchangia maandalizi ya morocco. Watu hawakulalamika walioongelea mantiki maana morocco ni mwakilishi kutoka bara la Africa. Ni suala la jiografia tu.
 
Mechi ya final AFCON kati ya Senegal vs Misri,wengi walishangilia Senegal na kuwabeza Misri kua ni waarabu sio waafrika!
Sasa inakuaje tena tunajipendekeza kwa Morocco? leo hii nina uhakika ikicheza Morocco vs Ghana,nyie wote mnaolalamika kubaguliwa mtaishangilia Ghana na mtaona Morocco sio waafrika! halafu acha kuchanganya Uarabu na uislamu,hakuna mchezaji wa Morocco aliyetaja uislamu,kama hujui wapo waarabu ila sio waislamu bali ni wakristo,

Tuache unafiki kwanza,ubaguzi tunao sana ila sisi kubagua hua tunaona ni sawa ila tukibaguliwa ndio tuna anza kulia lia.
we ndio hakuna unachoandika, yule nahodha ali-dedicate ushindi wao kwa waislam, unasemaje waislamu hawakutajwa? Au unachangia usichokijua
 
we ndio hakuna unachoandika, yule nahodha ali-dedicate ushindi wao kwa waislam, unasemaje waislamu hawakutajwa? Au unachangia usichokijua
Sasa wewe huna hata akili ya uelewa wa unachokisoma,unategemea usaidiwaje? Kua kiakili kwanza kisha njoo tena.
 
Kinachokusumbua ni ushabiki wa dini ya watu, haya ndio hao wamesema ushindi ni wa waarabu, nyie mnashoboka tu.
Ulivyokua hamnazo unafikiri waarabu wote ni waislamu! Misri kuna waarabu wengi ambao ni wakristo,Lebanon,Syria...huko wakristo wamejaa,acha kukariri,tumia simu yako kujifundisha mambo ili usiendelee kua kituko,

Kati ya Mimi na Wewe ni nani aliyeanza kuongelea dini? Wewe unajulikana humu kua Islamophobia inakutesa sana,comments zako na thd zako hapa JF zinathibitisha hilo,tafuta maembe mabichi utafune labda yatakupunguzia maumivu.
 
Kwanza uweze kwanaza kutofautisha "r" na "l" ndio urudi kuandika upya. Huu ni upoyoyo. Hata waarabu wala waislamu duniani hawakuchangia maandalizi ya morocco. Watu hawakulalamika walioongelea mantiki maana morocco ni mwakilishi kutoka bara la Africa. Ni suala la jiografia tu.
Acha uzuzu wao wameenda kucheza kwa ajiri ya taifa lao na si kwa ajiri ya waafrika.

Kama waliwataja waarabu na waislam wao ndo wanajua mchango wao kwao na ndio maana waliwataja na si nyinyi muwarazimishe wawatambue na nyinyi.

Aya mambo ya kupigania sijui bara zima utayakuta Afrika tu lakini kwenye mabara mengine hauwezi kukuta upuuzi huu.

Tuache kujifariji hakuna nchi inayo enda kupambana kwa ajiri ya nchi nyingine kila taifa lipambane na hali yake.
 
Ulivyokua hamnazo unafikiri waarabu wote ni waislamu! Misri kuna waarabu wengi ambao ni wakristo,Lebanon,Syria...huko wakristo wamejaa,acha kukariri,tumia simu yako kujifundisha mambo ili usiendelee kua kituko,

Kati ya Mimi na Wewe ni nani aliyeanza kuongelea dini? Wewe unajulikana humu kua Islamophobia inakutesa sana,comments zako na thd zako hapa JF zinathibitisha hilo,tafuta maembe mabichi utafune labda yatakupunguzia maumivu.

Waarabu huchukia sana nyeusi mnaoshobokea dini yao hiyo, huwaona matakataka, wana roho mbaya sana wale, sijui mliingiaje huo mkenge.
 
Moroco wamefanikiwa kwa sababu hawanywi Pombe na sio wazinzi
wapo na hofu ya Mungu that all hii ndo Siri Yao ya Mafanikio
Kwa hiyo siku zote ambapo walikuwa hawajafikia hii hatua walikuwa wanakunywa pombe na pia walikuwa ni wazinzi?

Na hayo mataifa manane yaliyowahi kulitwaa taji la dunia na wenyewe hawanywi pombe wala hawafanyi uzinzi.

Hili jukwaa linafanya tuwafahamu watu werevu na wapumbavu vilevile kutokana na wanayoandika humu.
 
Wapo barani Africa lakini hawapigani kwa ajili ya Afrika bali ni kwa ajiri ya nchi yao.

Mbona hamtaki kuelewa?

Mbona hayo mambo ya kupambania mabara huwa hatuyasikii kwenye mabara mengine zaidi ya Africa?
Nani amesema wanapigania Africa?

Wewe ndio huelewi ushabiki wa mashabiki na mitazamo yao ikoje.Mtu kusema Morroco ni Africa hama anishi wanapigana Africa ila wana wakilisha Africa maana kijiografia Morocco ipo barani Afrika na si Uarabuni

Kuingia waarabu kwa Morocco ni Mihemko na itikadi za kidini
 
habari ndo hiyo,kila mtu abebe msalaba wake.afanikiwe mwingine kwa juhudi zake alafu mafanikio mnataka mshee wote eti kisa mmetoka kijiji kimoja,kha,,!
Unaposhabikia let say ushindi wa Man city utakuwa umetoka nao kijiji kimoja?

Shida yenu hamu elewi ushabiki ni nini!
 
Unaposhabikia let say ushindi wa Man city utakuwa umetoka nao kijiji kimoja?

Shida yenu hamu elewi ushabiki.
je'Man city wakisema ushindi huu ni kwaajili ya wazungu na waingereza wewe mweusi sabiki wa Man city utakua na msimamo upi?
alafu mfano wako auendani Man city ni club Moroco ni timu ya taifa!
 
Kiasili waafrika ni wajamaa. Zamani kidogo hapa kwetu uliweza kwenda kijiji chochote ukajitambulisha kuwa unasafiri na unahitaji malazi na ukapewa na chakula na maji ya kuoga. Uzungu ndo unatutoa kwenye ujamaa ila bado upo katika viwango kama hivi vya mpira wa miguu. Ghana inashinda Tanzania tunashangilia. Huenda itafika wakati itapotea na kila mtu atafata mambo yake.
Tanzania ikishinda Ghana au Morocco haiwezi shangilia kumbuka
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Wengine wanakwambia team za Africa ziko mbili France na MORROCO kisa tu kuna watu weusi wakati waliwakataa wale wachezaji walipokuwa wadogo wazungu wakawatengeneza leo hii wanakwambia ni waafrika wenzetu yaani sisi ni vilaza wakujengewa sanamu kabisa tukumbukwe kila kizazi kwa ujinga wetu.
 
Back
Top Bottom