Tetesi: Waajiriwa wapya wa afya na elimu hawapewi hela ya kujikimu

Tetesi: Waajiriwa wapya wa afya na elimu hawapewi hela ya kujikimu

Bro,

Kafanye kazi kwa MASLAHI MAPANA YA TAIFA, wewe Ni miongoni Kati ya laki uliebahatika kupata kazi.

Kafanye kazi
Posho ya kujikimu ni haki ya mtumishi. Acha kuwafanyia mzaha watu wengine. Ingekuwa wewe ungesema hivyo?
 
Tufundishwe mind set kujiajiri aseee huko mbele watoto wetu wasije dhalilika maana ajira zinazidi kuwa finyu.,...tujiajiri
Huyu keshaajiriwa. Haki zake ziheshimiwe.
 
Kuwa na subira mzee. Sometimes huwa inachelewa, ila utalipwa. Fanya kazi.
 
Labda pesa za kuwalipa hazipo, vinginevyo ongeeni na waajiri wenu huko halmashauri waone ni namna gani ya kuwawezesha kabla ya kupata hiyo pesa na mshahara wenu kuanza kulipwa...
 
Mwaka 2015 nina mwanangu alichaguliwa mkoani ualimu hakupata chochote hata mshahara wa mwezi wa kwanza hakupata kwa hiyo wajue hilo kwa tahadhari.
 
Halmashauri haiwezi kuandaa pesa ya kujikimu,ukaikuta unapoenda kuripoti kwani haifamu ni yupi ataripoti au hatoripoti....kuna siku 14 za kwenda kufunga mizigo ndio uende kuanza kazi ....nenda kaage familia ukirudi utaikuta ipo.......
You try to think correctly,thing again accurately.
 
Nilitaka kuanzisha uzi kuhusu hili pia!

juzi nikiwa halmashauri moja wapo nliwauliza hiki kitu! nkaambiwa hela ya kujikimu ni "LABDA" mpaka mwezi ujao! nkawauliza sasa katika hiki kipindi chote mtu unaishije!? wakasema hiyo hawajui ni kutafuta alternative! nikawaambia sasa kama ni hivo vipi kuhusu salary!? ntapata mwezi huu!? nayo wakasema LABDA mpka mwezi ujao nlichoka sana!

nkawaambia sasa nataka kuchukua 14 days ntafute pesa mwenyewe na kujiandaa maana huu mkoa sijawahi fika! wakakataaa kua mwisho ni seven days!

nkajiuliza ina maana wanaajiri watu ilihali hawajajiandaa kuwapa angalau hiyo posho ya kujikimu!? nakumbuka yule bwana shemdoe wakati anatangaza alisema watakaochukua ila wasiripoti watashughulikiwa kumbe ilikua siasa tu kuonesha inawahi kutoka ilhali hakuna!?

nimeamua nirudi kwenye biashara yangu na kwa heshima ya kizalendo nataka serikali itafute mtu wa kuni replace, nimerejista kila kitu siku ntakayoona wameweka hyo hela ndo ntaenda! wasipoweka watafute mtu mwingine!

japo nna shida ila nisigeuzwe punda!

asanteni!
Maigizo mengi mno hizi serikali zetu.
 
Back
Top Bottom