Waamuzi waliochezesha mchezo wa Simba vs KMC afungiwa na TFF

Waamuzi waliochezesha mchezo wa Simba vs KMC afungiwa na TFF

Kwa anayejua au aliyenazo sheria na kanuni za maamuzi na adhabu kwa timu na waamuzi uwanjani aziweke hapa please kuna kitu nakitafta hapa.
Hasa Mwl. Kashasha km yumo humu.
 
Fake news!
common sense, waamuzi wasaidizi wote wama kosa gani?
Wewe jamaa Ni bure kabisa aiseee
Soma hiyo
Screenshot_20190426-160031.jpeg
 
hiko kikao kimekaa saa ngapi badala ya kulipa wachezaji wenu waache mgomo mnahangaika kutengeneza habari za uongo kuhusu Simba
 
Kwani yule mchezaji hakushika? Na kwa nini azam hawana slow motion??
Ulisahau msimu wa Mwaka juzi kuna match ilileta utata Mikoani Azam akaambiwa alete recorded dvd akagoma akasema kuwa record haipo tena hii match ilikuwa inawahusu Mikia
 
Muda si mrefu hata kama imewekwa ktk accpunts zao tff ila itatolewa ma statement kamq "our accounts were hacked" zitafuata.
 
Na anayeamua kuwa ni pigo lA penalty ni Nani?? Ukishamjua utaishi maisha ya Raha mstarehe!
Mbona sio wote wanaouwa mtu wanahukumiwa kunyongwa. . Huu mchezo wa waingereza mgumu Sana kuuelewa
 
TFF iwashukuru Azam tv kuonesha hizi mechi na wao wamejikuta wanaangalia replay ya matukio, ila kwa mechi ya jana ilikuwa na maamuzi ya hovyo
Refa aliechezesha mechi ya Simba vs KMC abdalah Kambuzi amefungiwa na kuondolewa kuchezesha mechi za ligi kuu

Mechi hiyo iliyoisha kwa Simba kushinda kwa bao 2-1 , ilileta malalamiko mengi akituhumiwa kuipendelea Simba

TFFimetoa taarifa ya kuwafungia waamuzi wote 3

View attachment 1081726
 
-Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) limewaondoa kwenye orodha ya waamuzi. Waamuzi waliochezesha mchezo wa jana wa ligi kuu Tanzania Bara kati ya KMC dhidi ya Simba, Mwamuzi wa kati Abdalah Kambuzi, Mwamuzi msaidizi namba moja (Line 1) Godfrey Msakila, na mwamuzi msaidizi namba mbili (line 2) Consolata Lazaro kuchezesha ligi kuu Tanzania Bara msimu huu baada ya kuonesha kiwango kisichoridhisha cha maamuzi katika mchezo huo.
#Tpl
 
Cha msingi simba hawajaondolewa point 3,
Karma is a bitch , mwaka juzi kagera sugar walitufunga huku walimchezesha mchezaji mwenye kadi nyekundu ambaye hakustahili kuwepo,TFF wakatupokonya ubingwa .

Vumilieni hata kama chungu malipo hapa hapa Simba ndo bingwa mjadala closed!
 
Maamuzi sahihi, kama tunataka kupiga hatua katika soka hili halipaswi kujirudia
 
Ilipaswa sheria ya kufutwa matokeo pindi marefa kama hawa wajitokezapo... maana timu zinaumia kisa miamala ya tigopesa...
Kufungiwa hakubadilishi matokeo so na sheria ya kufuta matokeo iwekwe ili haki ipatikane..
REFA ANAIBEBA SIMBA KAMA HANA AKILI NZURI... AFU TUNATAKA KUFIKA FAINALI YA CAF CHAMPIONS LEAGUE HIVI..??
 
Back
Top Bottom