DOKEZO Waandishi wa Habari Azam wanataabika Mikoani, wanahitaji msaada kulipwa stahiki zao

DOKEZO Waandishi wa Habari Azam wanataabika Mikoani, wanahitaji msaada kulipwa stahiki zao

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Hao wanajiita sijui Kina Balile akina Kibanda wapo bisy kuisifia serikali na kumkosoa waziri Slaaa ,
Niwape Taarifa Slaa hataki shobo ,wala hatakagi sifa huyo ,anatosha kujisifu mwenywe

teteeni hwa waandishi wa habari wa AZAM kama kweli mnaipenda tasnia na nyinyi sio wabnafsii
Sauti ipazwe haswa, na wao wanahitaji maisha mazuri kama wengine
 
Hao wanajiita sijui Kina Balile akina Kibanda wapo bisy kuisifia serikali na kumkosoa waziri Slaaa ,
Niwape Taarifa Slaa hataki shobo ,wala hatakagi sifa huyo ,anatosha kujisifu mwenywe

teteeni hwa waandishi wa habari wa AZAM kama kweli mnaipenda tasnia na nyinyi sio wabnafsii
Mjadala wa kitaifa unatakiwa
 
Hii kitu kaitumia Classmate wangu katoboa mapema ingali wengine tunataabika na masomo ya Chuo[emoji23][emoji23]

Anazunguka tu kqenye ziara za Mawaziri, Mjengoni5kazoeleka kama kijiwe cha kahawa.

Yote tisa kumi jamaa kaweza kupambana hadi kafikia hatua ya ku Donated mambo ya maendeleo huko kijijini kwao
😆😆
 
Na hao ndio tunaaminishwa wana unafuu kuliko wengine.
Niliwahi kufanya field kwenye chombo cha habari (radio) miaka kumi iliyopita, wakati mwingine sisi wa field ndio tulikuwa tunaokoa jahazi ya kuwanunulia vocha na chai tuliowakuta kazini maana hali ngumu.

Baadaye nikafanyaga kwenye gazeti kitengo tofauti na habari, hapo palikuwa na unafuu maana tulikuwa tunakunywa na chai ya bure + 5000 ya nauli.
Baadaye nikaacha kabisa hiyo sekta nikakimbilia kwingine.
 
Kuna hii ishu inayowahusu ripota wa Azam TV mikoani, wapo walioanza na kampuni wapo waliojiunga na Azam baadaye. Kwa mujibu wa mikataba yao ambayo ni renewable Kila baada ya Mwaka Mmoja au miaka miwili inatagemeana na maamuzi ya Viongozi, hawa watu ndiyo injini ya habari ya Azam News na baadhi ya vipindi lakini kwa miaka yote hiyo waajiri wamekuwa wakiwafanyia ujanja ujanja kwenye mikataba yao bila kuwapa kile wanachostahili kupata.

Wakati wanaanza kazi Azam Media LTD, taarifa zinadai ya kwamba walikuwa wanalipwa retainer (Mtu anayeajiriwa ili kusaidia au kuhudumia kwa muda mrefu) kiasi cha Tsh. laki tano na elfu hamsini kwa mwezi, na Kila Habari inayoruka kwenye Taarifa za Habari za Azam TV ripota alilipwa kiasi cha Tsh 10 Elfu, na Makala moja ya Dakika 30 Mwandishi Renainer alilipwa kiasi cha Tsh elfu hamsini.

Lakini wakati wa Uongozi wa Tido Muhando akiwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media LTD, walishushiwa viwango vya malipo ambapo Retainer ilishushwa kutoka Malipo ya laki Tano na nusu kwa mwezi Hadi Laki tatu na nusu huku story wakiongeza TSH.elfu 5 na kufikia kiasi cha Tsh elfu 15 na Makala zikishushwa Bei Hadi kufikia kiasi cha Tsh elfu 30 tu.

Lakini Habari zinazoenda kwenye platform nyingine kama Redio ya UFM na Mitandao ya kijamii wakiiipwa kias cha Tsh. elfu tatu tu.

Cha kusikitisha na kuwaumiza zaidi ni kwamba Ili waweze kulipwa stahiki zao kwa mwezi husika kwa maana ya retainer na story zilizoruka, ripota atalazimika kufikisha habari 15 kwa mwezi mmoja huu ni unyonyaji kwa sababu hawa watu hawana likizo, wanafanya Kazi siku zote 365 za mwaka.

Inapotokea ripota akiugua mfano akalala kitandani kwa wiki tatu bila kufanya kazi na kushindwa kufikisha habari 15 hawezi kulipwa stahiki zake, yaani si retainer wala hizo story chache alizozifanyia kazi. Kitu ambacho kwa chombo kikubwa kama Azam ni kuidhalilisha tasnia, na ni Ulukatili na kinyume cha haki za mfanyakazi.

Kama nilivyoeleza hapo awali, baadhi yao wamejiunga na Azam TV kati ya Mwaka 2013 na kuendelea wamekuwa wakipitia manyanyaso makubwa, lakini wale waliopo Ofisini Makao Makuu wanalipwa mishahara minono huku hawa Maripota wakinyonywa mpaka tone la damu licha ya kufanya kazi bila kuchoka kwa muda wote.

Hoja nyingine ni kwamba hao wote kwa miaka yote hiyo inayofikia 10 na zaidi wamefanya bila kuwa na bima za afya wala NSSF ingawa kwa taarifa nilizonazo ni kwamba mwaka jana AZAM Media LTD iliwaunganisha kwenye mfuko wa hifadhi ya jamii na huduma za bima za afya kwa maana ya NSSF na NHIF ambapo wameanza kuchangia mwezi Julai mwaka huu.

Kampuni inapaswa ione aibu kwa walioanza kuitumikia na kuikuza kwa kuwaingizia michango yao ya NSSF tangu walipoanza kazi. Kuanza kuwalipa ni jambo jema lakini kuanza kuwaingizia NSSF kuanzia mwaka jana baada ya miaka kumi na zaidi ni kutowatendea haki.

Huku ni kuwaonea na kuwapunja haki zao za msingi kwa Maisha yao ya kesho. Fikiria mtu kafanya kazi zaidi ya miaka 10 anaanza kulipwa NSSF mwaka wa 9 yaani miaka yote 9 iliyopita ameambulia patupu hii siyo haki, siyo utu, siyo ubinadamu.

Mzee wetu Said Salim Bakhersa na vijana wake akina Abubakar ni watu wa Imani na wenye hofu ya Mungu tunaamini hawalifahamu hili na hawawezi kukubali kuwapunja vijana waliosaidia kuikuza kampuni yeke kwa kuruhusu mikataba ya kinyonyaji.

Mwisho, hao waandishi hawawezi kusema kwa hofu ya kupoteza vibarua vyao lakini iangalieni upya mikataba ya reporter wenu. Waziri husika wasaidie hawa vijana wapate haki yao, maana kutoingiziwa kitu NSSF kwa miaka zaidi ya 10 ni unyonyaji ambao haujawahi kutokea. Naamini wengi wetu tunaipenda Azam TV kutokana na ubora na umahiri wa waandishi wenu.

Boresheni Maisha yao waendane na hadhi ya Azam TV. Kuna waandishi wenu huku mikoani tunawaona wamechoka mbaya, wengine tunagombaniana nao daladala yaani ni aibu. Unakutana naye kwanza kachoka, nguo mpauko, kavuja jasho wee hadi huruma, kumbe ananyonywa.

Hata akikaa kwenye TV tunaacha kuconcetrate kwenye habari yake anayoichambua tunakumbuka alivyokuwa anagombania chenji na konda ni aibu kwa Kampuni kwakweli.

Vile mnavyopandisha bei za vifurushi wazingatieni na wao kwenye maslahi maana Habari za Azam TV bila wao hakuna kitu. Ikikupendeza Mh. Rais wasemee hawa watu wapate stahiki zao, walipo hawawezi kusema ila wanachopitia wanakijua wenyewe. Mimi nimefanya tu kuleta taarifa.
Pahala popote kazini ama katika taasisi shida inakua sio mmiliki bali ni yule anayepewa mamlaka ya uendeshaji taasisi.
Waswahili tuna roho za korosho sana na ubinafsi uliopitiliza.
Sio tu Azam media,hata upande wa viwanda vya ngano katika usafirishaji/madereva mie nimeshuhudia wakilalamika.
Ila unakuta masikini Bakhresa hajui wala wakuu wa juu hawajui.
Waswahili tuna shida sana kwa kuhujumiana wenyewe kwa wenyewe.
 
Pahala popote kazini ama katika taasisi shida inakua sio mmiliki bali ni yule anayepewa mamlaka ya uendeshaji taasisi.
Waswahili tuna roho za korosho sana na ubinafsi uliopitiliza.
Sio tu Azam media,hata upande wa viwanda vya ngano katika usafirishaji/madereva mie nimeshuhudia wakilalamika.
Ila unakuta masikini Bakhresa hajui wala wakuu wa juu hawajui.
Waswahili tuna shida sana kwa kuhujumiana wenyewe kwa wenyewe.
Inataka Moyo
 
Nionyeshe media yoyote ambayo haina matatizo kama haya (Labda TBC ambayo ni Serikali) in short this is a dying industry kwahio inabidi hao wadau wawe wajanja watumie kuwa kwao AZAM na kuvuta kilichopo kila kinapopatikana na hapo hapo kutokusita kufanya freelancer, kuna ma MC kibao sikuhizi wanatumia kuwa kwao kwenye Kampuni fulani kupata tenda za harusi na wengine kufanya vijiblogu vyao kuwa angalau na authenticity kuliko ingekuwa vinginevyo....

That said sekta zote zinapumulia mashine unless una mbinu zako kinachopatikana hakikidhi mahitaji
 
Pahala popote kazini ama katika taasisi shida inakua sio mmiliki bali ni yule anayepewa mamlaka ya uendeshaji taasisi.
Waswahili tuna roho za korosho sana na ubinafsi uliopitiliza.
Sio tu Azam media,hata upande wa viwanda vya ngano katika usafirishaji/madereva mie nimeshuhudia wakilalamika.
Ila unakuta masikini Bakhresa hajui wala wakuu wa juu hawajui.
Waswahili tuna shida sana kwa kuhujumiana wenyewe kwa wenyewe.
Kwamba wanapewa kidogo kuliko kilichopo kwenye Mkataba ? Sababu akiamua kutoa kingi kwenye kusafirisha hizo ngano, atashindana vipi bei na Mo ambaye yeye labda hatoi kingi kama hicho ? Siongelei Azam per se ila hizi kampuni wateja wao ni shareholders ambao wao wanachojali ni as much profit as possible na sio wametoa welfare kiasi gani (ukiona wanatoa welfare hio ni Publicity Stunt)...

That is the nature of the Beast..,

1731395345561.png
 
Kwamba wanapewa kidogo kuliko kilichopo kwenye Mkataba ? Sababu akiamua kutoa kingi kwenye kusafirisha hizo ngano che atashindana vipi bei na Mo ambaye yeye labda hatoi kidogo kama hicho ? Siongelei Azam per se ila hizi kampuni wateja wao ni shareholders ambao kwao wanachojali ni as much profit as possible na sio wametoa welfare kiasi gani (ukiona wanatoa welfare hio ni Publicity Stunt) That is the nature of the Beast..,

View attachment 3150045
Mkuu nina ndugu amefanya kazi kama dereva hapo Bakhresa group.
Msimamizi wao alikua akiwapunja pesa za posho za kupakua ngano.
Kila trip moja kuna posho inawekwa.
Mathalan kila trip mfano elfu 6.
Msimamizi anakata anaweka kila trip elfu 3.
Ndio maana nikakwambia shida sio mmiliki ni mtu anayepewa kazi ya uendeshaji taasisi.
Embu rudi usome kwa uelewa nilichoandika kaka.
Na nikazidi kuongeza kuwa sisi wenyewe waswahili tunahujumiana.
 
Mkuu nina ndugu amefanya kazi kama dereva hapo Bakhresa group.
Msimamizi wao alikua akiwapunja pesa za posho za kupakua ngano.
Kila trip moja kuna posho inawekwa.
Mathalan kila trip mfano elfu 6.
Msimamizi anakata anaweka kila trip elfu 3.
Ndio maana nikakwambia shida sio mmiliki ni mtu anayepewa kazi ya uendeshaji taasisi.
Embu rudi usome kwa uelewa nilichoandika kaka.
Na nikazidi kuongeza kuwa sisi wenyewe waswahili tunahujumiana.
Je hata wakipewa hio Posho ya elfu sita inakidhi hayo mahitaji ? Na mimi rudi kunisoma ndio maana kuanzia mwanzo kwenye media sijazungumzia AZAM pekee bali Industry kwa ujumla na kwenye hili la Kampuni nimezungumzia kampuni zote kwa ujumla in the capitalists environment..., yaani hata hio tatu anayowapa hata kama akitoa mbili kuna watu bado watakuja kuomba kazi..., hivyo huyo msimamizi anakula kwa urefu wa kamba yake kama wanavyofanya wengine..., Au kama mataifa ya Ulaya yanavyo-marginalize mataifa yanayoendelea...

Matsya Nyaya; (Sanskrit: मात्स्यन्याय; IAST: mātsyanyāya) is an ancient Indian philosophy which refers to the principle of the Law of Fish.

1731396056188.png
 
Pahala popote kazini ama katika taasisi shida inakua sio mmiliki bali ni yule anayepewa mamlaka ya uendeshaji taasisi.
Waswahili tuna roho za korosho sana na ubinafsi uliopitiliza.
Sio tu Azam media,hata upande wa viwanda vya ngano katika usafirishaji/madereva mie nimeshuhudia wakilalamika.
Ila unakuta masikini Bakhresa hajui wala wakuu wa juu hawajui.
Waswahili tuna shida sana kwa kuhujumiana wenyewe kwa wenyewe.
Nakataa kuamini kwamba bakhresa hajui.

Hajui kivipi?

Tatizo ni kwamba wabongo tunaabudu matajiri.
 
Kuna hii ishu inayowahusu ripota wa Azam TV mikoani, wapo walioanza na kampuni wapo waliojiunga na Azam baadaye. Kwa mujibu wa mikataba yao ambayo ni renewable Kila baada ya Mwaka Mmoja au miaka miwili inatagemeana na maamuzi ya Viongozi, hawa watu ndiyo injini ya habari ya Azam News na baadhi ya vipindi lakini kwa miaka yote hiyo waajiri wamekuwa wakiwafanyia ujanja ujanja kwenye mikataba yao bila kuwapa kile wanachostahili kupata.

Wakati wanaanza kazi Azam Media LTD, taarifa zinadai ya kwamba walikuwa wanalipwa retainer (Mtu anayeajiriwa ili kusaidia au kuhudumia kwa muda mrefu) kiasi cha Tsh. laki tano na elfu hamsini kwa mwezi, na Kila Habari inayoruka kwenye Taarifa za Habari za Azam TV ripota alilipwa kiasi cha Tsh 10 Elfu, na Makala moja ya Dakika 30 Mwandishi Renainer alilipwa kiasi cha Tsh elfu hamsini.

Lakini wakati wa Uongozi wa Tido Muhando akiwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media LTD, walishushiwa viwango vya malipo ambapo Retainer ilishushwa kutoka Malipo ya laki Tano na nusu kwa mwezi Hadi Laki tatu na nusu huku story wakiongeza TSH.elfu 5 na kufikia kiasi cha Tsh elfu 15 na Makala zikishushwa Bei Hadi kufikia kiasi cha Tsh elfu 30 tu.

Lakini Habari zinazoenda kwenye platform nyingine kama Redio ya UFM na Mitandao ya kijamii wakiiipwa kias cha Tsh. elfu tatu tu.

Cha kusikitisha na kuwaumiza zaidi ni kwamba Ili waweze kulipwa stahiki zao kwa mwezi husika kwa maana ya retainer na story zilizoruka, ripota atalazimika kufikisha habari 15 kwa mwezi mmoja huu ni unyonyaji kwa sababu hawa watu hawana likizo, wanafanya Kazi siku zote 365 za mwaka.

Inapotokea ripota akiugua mfano akalala kitandani kwa wiki tatu bila kufanya kazi na kushindwa kufikisha habari 15 hawezi kulipwa stahiki zake, yaani si retainer wala hizo story chache alizozifanyia kazi. Kitu ambacho kwa chombo kikubwa kama Azam ni kuidhalilisha tasnia, na ni Ulukatili na kinyume cha haki za mfanyakazi.

Kama nilivyoeleza hapo awali, baadhi yao wamejiunga na Azam TV kati ya Mwaka 2013 na kuendelea wamekuwa wakipitia manyanyaso makubwa, lakini wale waliopo Ofisini Makao Makuu wanalipwa mishahara minono huku hawa Maripota wakinyonywa mpaka tone la damu licha ya kufanya kazi bila kuchoka kwa muda wote.

Hoja nyingine ni kwamba hao wote kwa miaka yote hiyo inayofikia 10 na zaidi wamefanya bila kuwa na bima za afya wala NSSF ingawa kwa taarifa nilizonazo ni kwamba mwaka jana AZAM Media LTD iliwaunganisha kwenye mfuko wa hifadhi ya jamii na huduma za bima za afya kwa maana ya NSSF na NHIF ambapo wameanza kuchangia mwezi Julai mwaka huu.

Kampuni inapaswa ione aibu kwa walioanza kuitumikia na kuikuza kwa kuwaingizia michango yao ya NSSF tangu walipoanza kazi. Kuanza kuwalipa ni jambo jema lakini kuanza kuwaingizia NSSF kuanzia mwaka jana baada ya miaka kumi na zaidi ni kutowatendea haki.

Huku ni kuwaonea na kuwapunja haki zao za msingi kwa Maisha yao ya kesho. Fikiria mtu kafanya kazi zaidi ya miaka 10 anaanza kulipwa NSSF mwaka wa 9 yaani miaka yote 9 iliyopita ameambulia patupu hii siyo haki, siyo utu, siyo ubinadamu.

Mzee wetu Said Salim Bakhersa na vijana wake akina Abubakar ni watu wa Imani na wenye hofu ya Mungu tunaamini hawalifahamu hili na hawawezi kukubali kuwapunja vijana waliosaidia kuikuza kampuni yeke kwa kuruhusu mikataba ya kinyonyaji.

Mwisho, hao waandishi hawawezi kusema kwa hofu ya kupoteza vibarua vyao lakini iangalieni upya mikataba ya reporter wenu. Waziri husika wasaidie hawa vijana wapate haki yao, maana kutoingiziwa kitu NSSF kwa miaka zaidi ya 10 ni unyonyaji ambao haujawahi kutokea. Naamini wengi wetu tunaipenda Azam TV kutokana na ubora na umahiri wa waandishi wenu.

Boresheni Maisha yao waendane na hadhi ya Azam TV. Kuna waandishi wenu huku mikoani tunawaona wamechoka mbaya, wengine tunagombaniana nao daladala yaani ni aibu. Unakutana naye kwanza kachoka, nguo mpauko, kavuja jasho wee hadi huruma, kumbe ananyonywa.

Hata akikaa kwenye TV tunaacha kuconcetrate kwenye habari yake anayoichambua tunakumbuka alivyokuwa anagombania chenji na konda ni aibu kwa Kampuni kwakweli.

Vile mnavyopandisha bei za vifurushi wazingatieni na wao kwenye maslahi maana Habari za Azam TV bila wao hakuna kitu. Ikikupendeza Mh. Rais wasemee hawa watu wapate stahiki zao, walipo hawawezi kusema ila wanachopitia wanakijua wenyewe. Mimi nimefanya tu kuleta taarifa.
Burudani kwa wote
 
Kila mtu atabeba mzigo wake mwenyewe

Wanaleta malalamiko jf kwan akuna vyombo vya kuwatetea na kupeleka malalamiko yao
Kwan akuna sheria za kaz kwan akuna mahakama ya kaz na km sio mahaka ya kaz kwan akuna sheria zinazoeza waruhusu wao kufungua kesi

Ttzo waandishi wengi ni Ccm na akili zao na mawazo yamekaa ki ccm
 
Pahala popote kazini ama katika taasisi shida inakua sio mmiliki bali ni yule anayepewa mamlaka ya uendeshaji taasisi.
Waswahili tuna roho za korosho sana na ubinafsi uliopitiliza.
Sio tu Azam media,hata upande wa viwanda vya ngano katika usafirishaji/madereva mie nimeshuhudia wakilalamika.
Ila unakuta masikini Bakhresa hajui wala wakuu wa juu hawajui.
Waswahili tuna shida sana kwa kuhujumiana wenyewe kwa wenyewe.
Mchawi wa mswahili ni mswahili mwenzake.
 
Back
Top Bottom