Waandishi wa Habari na Bahasha: Sio Kila Bahasha ni Rushwa

Waandishi wa Habari na Bahasha: Sio Kila Bahasha ni Rushwa

Chante,

Hauna haja ya ku "reply with quote" unapojibu hoja ndefu, inakuwa umeibandika hoja ndefu na unayoijibu ndefu, haileti raha. Wewe bandika hoja yako kwa kuandika unajibu post # ipi, inatisha kabisa, hii yote ni katika raha za kufanya mjadala uwe mzuri, naomba rudi na u edit kwa kuyapunguza hayo mabandiko kwa kuondoa post ya mwanzo ya mada, kwani tayari ipo juu kila page haina haja ya kuirudia tena.

Ahsante.
 
Dada yangu FaizaFoxy, hebu muulize Maalim wako Mohammed Said, aliwezaje kuyaandika hayo aliyoaandika na atawezaje kuya print na kuyasambnaza maandishgi yake bila kuwezeshwa?. Ili media zifanye kazi zake vyema ni lazima ziwezeshwe!. Huu uwezeshaji wa media zetu masikini ili zitimize wajibu wake nazo ni bahasha!.

Hivi unajua kwa nini shule la Islamic Seminaries zinafanya vibaya na ndizo shule zinazovuta mkia zikifuatiwa na shule za Wazazi?!. Jee unadhani watoto wa Kiislamu wanazaliwa na akili pungufu ya Wakikrito?!. Hapana!, wote wanazaliwa na akili zawa na wengine hata kuwazidi Wakristu, kwa nini sasa ndio wana end up failures?!. Tena tuna bahati hatujafanya sense walioko magerezani wengi ni wa dini gani, au idadi ya masikini wanaioshi katika umasikini uliotopea wengi ni wa dini gani?!, utashang'aa!. Sababu ni nini?, ni kiwango cha uwezeshaji!. Wenzenu Wakristu wanafanya uwezeshaji kwa taasisi zake huku wakisaidiwa na ile MOU ambayo nayo ni bahasha!.

Media zetu ni masikini za kutupwa bila kuwezeshwa, haziwezi!. Sasa kama uwezeshaji huu unaiuta rushwa!, hebu muulize Rais Kikwete huwa anawapa nini wale waandishi wa habari anao safiri nao?!. Kama kweli kila anaetoa bahasha kwa waandishi lazima aende jela, naomba tuanzie na Ikulu, nami jela nitajipeleka mwenyewe bila hata kusubiri kutafutwa!

Lengo la hii mada ni kuonyesha kuwa kweli bahasha zipo lakini sio kila bahasha ni rushwa!. Ziko bahasha safi za facilitation ambazo lengo lake ni uwezeshaji wa media, hizi sio rushwa!
.

Hilo povu linalokutoka hapo kuhusu Waislam, linaonesha kuwa unapokea vibahasha kuuandika vibaya Uislam. Pole sana, umedhihirisha tunayoyajuwa.
 
Mkuu Pasco, kwanza hongera kwa maelezo yako mazuri. Mimi naomba unisaidie kitu kimoja. Wapo waandi wa habari za uchunguzi ambao nao hulazimika kutoa bahasha kutoka mifukoni mwao ili wapate habari. Hiyo nayo ni rushwa? Ama sawa kufanya hivyo.
Mkuu Jumakidogo, kwanza asante kunipa hongera, na asante kuibua hii issue ya 'rushwa halali', justified corruption!. Katika sekta zote za uandishi wa habari, uandishi wa habari za uchunguzi ndio mgumu kuliko fani zote, sisi waandishi tunaitana 'wapiganaji', na wale wakongwe au wahariri tunawaida 'makamanda' hivyo waandishi wanaondika habari hizi za uchunguzi wanapaswa kuitwa "makomandoo" ndio maana waandishi kama Jerry Muro wanamiliki bastola na pingu kihalali!.

Undishi wa habari za uchunguzi kwanza unahitaji kipaji maalum, mwandishi husika lazima awe na 'sharp nose for news' kuweza kutambua habari zaidi ya habari ili afanya investigative journalism. Lazima awe na "curiosity" ya ziada kubaini some hidden agendas, lazima awe jasiri na uwezo wa subra ya hali ya juu pamoja na uvumilivu na ustahimilivu ili kupata anachokitaka!.

Mashirika yote ya kijasusi hata TISS yetu inatoa rushwa kwa watu wanaitwa ma "informer" wake wenye jukumu la kutafuta taarifa zozote nyeti. Hawa ma informer ili wapate taarifa hivyo most of the times, wanatoa rushwa ili kuzipata taarifa hizo, hizi ni rushwa halali!. Sasa mwandishi wa habari za uchunguzi, sio tuu ana risk maisha yake, bali pia sometimes hulazimika kutoa chochote ili kupata unachokitaka, hiyo rushwa sometimes ofisi itakurudishia ukiweza ku account for au sometime inakula kwako!.

Wakati wa yale mauaji ya Zanzibar ya January 200I, nilikwenda kucover kwa media fulani, polisi ikatangaza kuwa walitumia risasi za moto baada ya kutumia rubber bullets kutozaa matunda!, ikanibidi nimpe kidogodogo polisi fulani incharge wa amoural ya polisi Zanzibar kumuomba anionyeshe rubber bullet inafafanaje! Huyo polisi akanithibitishia Zanzibar hawana rubber bullets!. Wakati wa press conference ya polisi Zanzibar, nikaomba nionyeshwe hiyo rubber bullets inafafanaje, au tuonyeshwe vishina vya hizo risasi bandia zilizotumika, polisi wakang'aka sio jukumu la polisi kuwaonyesha raia silaha, hizo ni siri za jeshi!.

Jioni ile nikaripoti kuwa japo polisi Zanzibar wamedai kutumia risasi bandia, wameshindwa kuonyesha uthibitisho wowote wa uwepo wa risasi hizo, hivyo story ika conclude kuwa polisi wa Zanzibar wamewamiminia risasi za moto waandamanaji Zanzibar na kuua 22!.
Kesho yake nilishikwa na kutiwa ndani Mwembemadema for two good days!.

Kwenye bahasha za uwezeshaji, nimeitaja TMF kutoa fungu kwa waandishi ili waandike habari za uchunguzi na habari za vijijini na nikasisitiza bahasha hizi sio rushwa!.

Vyombo vya habari vya Tanzania vinakabiliwa na ukata wa kufa mtu, baada ya Mzee wa vijisenti kuthibitika ana vile vinjisent, ingekuwa ni nchi za wenzetu vijana wa kazi wangeibuka na investigative story yenye inside out!. Huku tunabiri tuu press conference, semina, warsha na makongamano only!
 
  • Thanks
Reactions: ral
Pasco,
  1. Hustahili kusema hivyo tena wewe ni mwanasheria
  2. Bashasha yoyote ni haramu
  3. Unachozungumza ni mazoea, mazoea hayafanyi haramu kuwa halali. Ukata sio excuse ya kufanya maovu
  4. Wewe mwenyewe umekosa ''moral authority'' debe unalompigia mtu mmoja humu sio bure lazima kuna nguvu ya pesa
  5. Tatizo hatuna watu waliobobea kwenye habari. Watu kama Ulimwengu, Kajubi, Nizar, Ryoba, Kuhenga, kwa viwango vya uandishi wa BBC (English), CNN au Al Jazeera walitakiwa kuwa kwenye fani bado kama reporters au waandishi. Lakini huku wameshatundika madaluga eti wao ni ma columnists na maveteran matokeo yake kina Nzowa, Bashir Mwenda, Orest & CO ndo wako news room wao wanawaza bahasha tu
  6. Pasco waulizeni akina Uli Mwambulukutu, Nizar Visram, Mbaraka Islam au Rajab Ahmed wakueleze uharamu wa bahasha
Mkuu Kintiku
Mimi sio mwanasheria, bali ni mwanahabari niliosomea sheria!. Kuwa mwanasheria sio kusoma sheria bali kupractise sheria!. Hivyo LL.B ninayo, naweza kupractise wakati wowote, bali nimebaki kwenye habari just for the love of it, I'm comming of age hivyo soon nita wind off journalisim with a bang na kuanza kupractise sheria kama wakili wa kujitegemea na kesi zangu zitakuwa` zile za kutetea wanyonge on pro bono!.
Sio kila bahasha ni rushwa!.
Wote uliowataja nawajua na wengine nimefanya nao kazi na wengine nawajua zaidi ya uwajuavyo wewe!.
 
Chante,
Hauna haja ya ku "reply with quote" unapojibu hoja ndefu, inakuwa umeibandika hoja ndefu na unayoijibu ndefu, haileti raha. Wewe bandika hoja yako kwa kuandika unajibu post # ipi, inatisha kabisa, hii yote ni katika raha za kufanya mjadala uwe mzuri, naomba rudi na u edit kwa kuyapunguza hayo mabandiko kwa kuondoa post ya mwanzo ya mada, kwani tayari ipo juu kila page haina haja ya kuirudia tena.
Ahsante.
FaizaFoxy, kwa hili asante, punguza religious sentiments wala usituletee vifungu vya dini kupinga rushwa!.
Dada yangu nasisitiza rushwa ni malengo sio kila bahasha ni rushwa kama fedha mnazopewa nyie wanawake na sisi wanaume sio zote ni hongo!. Fedha ikitolewa kuchumbia inaitwa posa, wakati fedha hiyo hiyo ikitolewa kutongozea inaitwa hongo!
Malengo ya posa na hongo ni yale yale, posa ni kupata mke na kuhalalisha lile tendo na hongo ni zinaa!.
Mke akipewa fedha kwenye ajili ya matumizi yake nayo ni hongo?, malaya akilipwa ujira kwa kazi yake ndio hongo!. Kote ni fedha zimetolewa kwa tendo lili like, kihalali sio hongo, kizinaa ndio hongo!

Vivyo hivyo kuna bahasha zinatolewa kwa media kihalali na kuna bahasha haramu, bahasha halali sio rushwa bali zile haramu!.
 
Pasco,'
" Bahasha" za Grants na fellowship si rushwa. Hizi hazitolewi ili mwandishi aandike mazuri tu ya yule anayetoa hiyo pesa. (emphasis is mine).
Wale wote mnaosisitiza kila bahasha ni rushwa, tafuta post #131 mumsome Jasusi!
 
FaizaFoxy, kwa hili asante, punguza religious sentiments wala usituletee vifungu vya dini kupinga rushwa!.
Dada yangu nasisitiza rushwa ni malengo sio kila bahasha ni rushwa kama fedha mnazopewa nyie wanawake na sisi wanaume sio zote ni hongo!. Fedha ikitolewa kuchumbia inaitwa posa, wakati fedha hiyo hiyo ikitolewa kutongozea inaitwa hongo!
Malengo ya posa na hongo ni yale yale, posa ni kupata mke na kuhalalisha lile tendo na hongo ni zinaa!.
Mke akipewa fedha kwenye ajili ya matumizi yake nayo ni hongo?, malaya akilipwa ujira kwa kazi yake ndio hongo!. Kote ni fedha zimetolewa kwa tendo lili like, kihalali sio hongo, kizinaa ndio hongo!

Vivyo hivyo kuna bahasha zinatolewa kwa media kihalali na kuna bahasha haramu, bahasha halali sio rushwa bali zile haramu!.

Vifungu vya dini tazama ni nani alivianzisha au hujajiona? au mtu akitaja dini yangu kwa vibaya mimi nikae kimya? na wewe wewe tu uwe na ruksa? lakini nnapotaja mimi, wewe uninyamazishe? wacha kuwa biased. Huwa sijibu kwa kukisia na sintokaa kimya utapoanza, au udini kwako ni Uislam tu? ulipotaka darsa ulifikiri ntakutolea wapi? Mnayaanzisha wenyewe tukijibu mnakurupuka, macho mnayo lakini hayaoni. Ndio maana hata unapoipokea rushwa unataka kuihalisha kuwa si rushwa kwa kuwa tu macho yako hayaoni, moyo wako haukusuti, na dhamira yako haiko sawa.

Hata umalaya unatumika kuwa rushwa au hujasikia rushwa ya ngono? na huo nao uhalalishe.
 
wacha nitoe judgement.
after having heard all the parties to this dispute and with the consideration of the evidences given by both parties
the forum (hereby reffered to as JF) rulled that the complainant has failed to satisfy the forum on the legality of the bahasha
received and there is no proper justification of his act.The forum is hereby ordering Pasco and other journalists with the
same habit to return all the bahashas to JF founder with due effect within 24 hours.The bahasha shall be kept and or be used by JF for its daily expenses.
So ordered.
No right to appeal granted.

lokissa
JF senior judge.
 
Vifungu vya dini tazama ni nani alivianzisha au hujajiona? au mtu akitaja dini yangu kwa vibaya mimi nikae kimya? na wewe wewe tu uwe na ruksa? lakini nnapotaja mimi, wewe uninyamazishe? wacha kuwa biased. Huwa sijibu kwa kukisia na sintokaa kimya utapoanza, au udini kwako ni Uislam tu? ulipotaka darsa ulifikiri ntakutolea wapi? Mnayaanzisha wenyewe tukijibu mnakurupuka, macho mnayo lakini hayaoni.
Usianzishe Jihad vs Crusade, walioanzisha tangu enzi za Continapole wameshindwa itakuwa wewe?. Si unaona jinsi Mazayuni wanavyowatesa ndugu zenu kule Mashariki ya Kati?, si umeona ana wanaopigania Uislamu wanafanywa nini?, amekiona kilichompata Saadam, Osama na juzi juzi Ghadafi?!, bado unataka kutangaza vita?.

Naomba tutafungua thread nyingine tufanye vita kati ya Uislamu na Ukristu, ipi ni dini ya kweli ya Mwenye Enzi Mungu tuone nani atashinda, au hata tuwashindanishe Mtume Mohammed (SAW) na Nabii Issa Bin Maryam (AS) tuone nani ndio mwenye darja ya juu kwa Mwenyenzi Mungu, (Allah subhana wa ta'ala). kwa sasa hebu tujadili hizi bahasha bila kuingiza udini!.
 
wacha nitoe judgement.
after having heard all the parties to this dispute and with the consideration of the evidences given by both parties
the forum (hereby reffered to as JF) rulled that the complainant has failed to satisfy the forum on the legality of the bahasha
received and there is no proper justification of his act.The forum is hereby ordering Pasco and other journalists with the
same habit to return all the bahashas to JF founder with due effect within 24 hours.The bahasha shall be kept and or be used by JF for its daily expenses.
So ordered.
No right to appeal granted.

lokissa
JF senior judge.
Lokisa nimecheka!, infact JF inaendeshwa kwa bahasha!. Jee sisi wote tunaotoa michango kwa jf, tunatoa rushwa ili jf iendelee kubaki hewani?. Hata ile bahasha ya mchango wa juzi kwa marehemu ni rushwa ili familia ituone sisi jf tumemlilia?, jamani bahasha za rushwa zipo ila sio kila bahasha ni rushwa!.
 
Chante,

Hauna haja ya ku "reply with quote" unapojibu hoja ndefu, inakuwa umeibandika hoja ndefu na unayoijibu ndefu, haileti raha. Wewe bandika hoja yako kwa kuandika unajibu post # ipi, inatisha kabisa, hii yote ni katika raha za kufanya mjadala uwe mzuri, naomba rudi na u edit kwa kuyapunguza hayo mabandiko kwa kuondoa post ya mwanzo ya mada, kwani tayari ipo juu kila page haina haja ya kuirudia tena.

Ahsante.
Thanks alot,
nimekuelewa na nimetekeleza..
 
Bahasha ya Kushinikiza Positive Covarage.
Hii ndio bahasha ya kwanza ya rushwa, hutolewa na source ili kuwa entice waandishi wawafanyie favourable covarage. Kwa kawaida bahasha hii inakuwa nene fulani, bahasha hii huandamana na obligation kuwa lazima story itoke. Bahasha hizi za shinikizo la story kutoka hazitolewi kwa waandishi wote, bali to only few selected, na kwa vile bahasha hizi ni rushwa, hutolewa kwa kificho!. Zile bahasha za halali kama za usafiri husainiwa wazi wazi na hukawiwa kila mtu akiona kwa sababu there is nothing to hide, lakini hizi hutolewa kwa kificho, no one will know nani amepokea bahasha na nani hajapokea kutokana mazingira ya usiri. Watoaji wa bahasha hizi wanajua ni rushwa na wapokeaji wanajua ni rushwa!. (to avoid conflict of interest, nawaombeni msiniulize zaidi kuhusu hizi!).
Bahasha za Kuzuia Habari Kutoka-Hii ni Rushwa!.
Kuna bahasha za kuzuia story fulani isitoke!, hizi ni bahasha zinazotembezwa kwa waandishi ili kuzuia story fulani isitoke ili kulinda maslahi fulani au jina la mtu fulani lisichafuke!. Hii inahusisha kuitwa kwenye tukia na kutake a good care ya waandishi ili wasiripoti kabisa kuhusu tukio fulani!. Hii mara nyingi huusisha ama scandals au black mail. Mfano kigogo mmoja mheshimiwa sana, ameshitakiwa kwa kosa la kufumwa akifanya mapenzi na Changudoa ufukweni. Story hiyo ikitoka itamvunjia heshima sana mzee, hivyo anakata fungu fulani la kutakata la kuwatake care waandishi wote wanaoripoti toka mahakamani ili kesi ya kigogo ikitajwa waipotezee. Au Wafanyakazi wa kiwanda fulani wamegoma, wewe ni mwandishi unakwenda kucoiver story, unaanza na mgomo, ili kubance story, lazima uwatafute na management, ile kufika management, unakuwa well taken care off, uamuzi ni wako, ulinde heshima ya taaluma yako na ulale njaa, ama uuze utu wako jioni ukakae viti virefu, uamuzi huwa ni individual!.


Vipi waandishi wanaoongozana na misafara ya kampeni wakati wa uchaguzi, hizo bahasha zinachukuliwaje?

Kwa mfano, katika kampeni ya CCM mwaka 2005 katika mkutano wa kampeni wa Karagwe kuna mpiga kura alimuuliza mgombea wa ccm swali la kuudhi akashindwa kujibu, baada ya mkutanao wakati wa kugawa bahasha, Muhingo; aliyekuwa mratibu wa eneo hilo, akawaomba waandishi wasiripoti hilo tukio lakini mwandishi wa Mwananchi akaripoti na kesho yake akakosa bahasha. Mfano kama huo ulitokea tena wakati wa kampeni za 2010.
 
Mkuu Jumakidogo, kwanza asante kunipa hongera, na asante kuibua hii issue ya 'rushwa halali', justified corruption!. Katika sekta zote za uandishi wa habari, uandishi wa habari za uchunguzi ndio mgumu kuliko fani zote, sisi waandishi tunaitana 'wapiganaji', na wale wakongwe au wahariri tunawaida 'makamanda' hivyo waandishi wanaondika habari hizi za uchunguzi wanapaswa kuitwa "makomandoo" ndio maana waandishi kama Jerry Muro wanamiliki bastola na pingu kihalali!.

Undishi wa habari za uchunguzi kwanza unahitaji kipaji maalum, mwandishi husika lazima awe na 'sharp nose for news' kuweza kutambua habari zaidi ya habari ili afanya investigative journalism. Lazima awe na "curiosity" ya ziada kubaini some hidden agendas, lazima awe jasiri na uwezo wa subra ya hali ya juu pamoja na uvumilivu na ustahimilivu ili kupata anachokitaka!.

Mashirika yote ya kijasusi hata TISS yetu inatoa rushwa kwa watu wanaitwa ma "informer" wake wenye jukumu la kutafuta taarifa zozote nyeti. Hawa ma informer ili wapate taarifa hivyo most of the times, wanatoa rushwa ili kuzipata taarifa hizo, hizi ni rushwa halali!. Sasa mwandishi wa habari za uchunguzi, sio tuu ana risk maisha yake, bali pia sometimes hulazimika kutoa chochote ili kupata unachokitaka, hiyo rushwa sometimes ofisi itakurudishia ukiweza ku account for au sometime inakula kwako!.

Wakati wa yale mauaji ya Zanzibar ya January 200I, nilikwenda kucover kwa media fulani, polisi ikatangaza kuwa walitumia risasi za moto baada ya kutumia rubber bullets kutozaa matunda!, ikanibidi nimpe kidogodogo polisi fulani incharge wa amoural ya polisi Zanzibar kumuomba anionyeshe rubber bullet inafafanaje! Huyo polisi akanithibitishia Zanzibar hawana rubber bullets!. Wakati wa press conference ya polisi Zanzibar, nikaomba nionyeshwe hiyo rubber bullets inafafanaje, au tuonyeshwe vishina vya hizo risasi bandia zilizotumika, polisi wakang'aka sio jukumu la polisi kuwaonyesha raia silaha, hizo ni siri za jeshi!.

Jioni ile nikaripoti kuwa japo polisi Zanzibar wamedai kutumia risasi bandia, wameshindwa kuonyesha uthibitisho wowote wa uwepo wa risasi hizo, hivyo story ika conclude kuwa polisi wa Zanzibar wamewamiminia risasi za moto waandamanaji Zanzibar na kuua 22!.
Kesho yake nilishikwa na kutiwa ndani Mwembemadema for two good days!.

Kwenye bahasha za uwezeshaji, nimeitaja TMF kutoa fungu kwa waandishi ili waandike habari za uchunguzi na habari za vijijini na nikasisitiza bahasha hizi sio rushwa!. Maridadi sana, hapa napata somo kuwa pengine rushwa japo ni kosa kwa sheria za nchi. Lakini kwa upande mmoja wa shilingi inaweza kuwa na faida pia. Hapa tunaona waandishi wa habari za uchunguzi wanaweza kuhatarisha maisha yao kwa ajili ya kusaka habari nyeti na mara nyingine hulazimika kutoa bahasha ili wapate habari kwa wepesi. Lakini pia hapa kuna jambo dogo nitahitaji msaada kidogo kuhusu matokeo ya faida ya rushwa atoayo mwandishi wa habari za uchunguzi . Kwa mfano: "Ikiwa mimi ni mwandishi wa habari za uchunguzi, nimepata fununu kuhusu taarifa ambazo pengine zinahusu njama zinazotishia usalama wa Taifa. Lakini kwa bahati mbaya yule mtoa taarifa anahitaji apewe bahasha kwanza ndipo anipe habari hiyo. Kwa bahati mbaya wakati nampa rushwa hiyo, jamaa wa Takukuru wananiweka kati na kunifungulia mashitaka ya kutoa rushwa. Mambo yatakuwaje hapo kwa upande wangu ikiwa nilikuwa natoa rushwa ili nipate habari kwa ajili ya maslahi ya Taifa? Je hii ni mfano wa rushwa halali? Samahani japo nimeuliza swali la kisheria, lakini naimani kwa uzoefu wako katika tasnia ya uandishi wa habari bila shaka umewahi kukumbana ama kushuhudia kesi ya aina hii. Nipe japo kwa ufupi.
Mkuu.
 
Mkuu Pasco frankly speaking
je maadili ya uandishi wa habari yanaruhusu haya unayotueleza humu janvini?
Tuanzia hapo kwanza
 
Vipi waandishi wanaoongozana na misafara ya kampeni wakati wa uchaguzi, hizo bahasha zinachukuliwaje?

Kwa mfano, katika kampeni ya CCM mwaka 2005 katika mkutano wa kampeni wa Karagwe kuna mpiga kura alimuuliza mgombea wa ccm swali la kuudhi akashindwa kujibu, baada ya mkutanao wakati wa kugawa bahasha, Muhingo; aliyekuwa mratibu wa eneo hilo, akawaomba waandishi wasiripoti hilo tukio lakini mwandishi wa Mwananchi akaripoti na kesho yake akakosa bahasha. Mfano kama huo ulitokea tena wakati wa kampeni za 2010.
Kakalende, wale waandishi wanaozunguka na wagombea ni rushwa at its best, ila rushwa hii ni legal rushwa!. Vyombo vya habari vya umma pia vilipewa bahasha nene na nchi wafadhili ili vitoe haki sawa ya covarage kwa vyama vyote na hii imemcost Tido.

Kusema ukweli hapa ndipo lazima tukubali, beggars can not be chooses, vyombo vya habari vilitakiwa kuwa na uwezo wake vyenyewe, nikiwa UK nimeona helkopta ya SKY News ikiranda. Huku kwenye kampeni Ufoo Saro wa ITV alizunguka na helcopter ya Mbowe na reporting yake ili reflect ile lift, sambamba na Gaston Msingwa alizunguka na helcopter ya JK na reportage ili reflect hiyo favuor!

Uchaguzi wa 2000 mimi ndio nihead political desk la media fulani na nilijitahidi kuwa very fair, baada ya uchaguzi, Karume aliponea tundu la Sindano!, mimi ikani cost eti nimetoa more millage kwa CUF!.
 
Mkuu Pasco frankly speaking
je maadili ya uandishi wa habari yanaruhusu haya unayotueleza humu janvini?
Tuanzia hapo kwanza
Mkuu paulss, news is free, na ndio maadili ya uandishi wa habari, kitu chochote kitakachoingilia uhuru wa habari ni kinyume cha maadili, hivyo haya ninayoyaeleza humu yale mazuri hayaendi kinyume cha maadili na yale mabaya ambayo ndio rushwa zenyewe ni kinyume cha maadili ila ndicho kitu kinachofanyika!.
 
Ila kwangu bahasha zote ni rushwa.maana si ulalipwa? Iyo bahasha haipo kwenye package yako
 
Mkuu paulss, news is free, na ndio maadili ya uandishi wa habari, kitu chochote kitakachoingilia uhuru wa habari ni kinyume cha maadili, hivyo haya ninayoyaeleza humu yale mazuri hayaendi kinyume cha maadili na yale mabaya ambayo ndio rushwa zenyewe ni kinyume cha maadili ila ndicho kitu kinachofanyika!.
Mkuu mimi si mwandishi wa habari lakini siamini kama kazi ya uandishi wa habari haina maadili yanayozuia kupoke chochote kutoa kwa mtu unayechukua taarifa toka kwake
Pamoja na sababu lukuki za uchovu wa vyombo vyetu vya habari ambapo nakubaliana na wewe lakini je maadili ya kazi yana ruhusu?
Naamini umesomea kazi hii na unajua naongelea nini
 
Back
Top Bottom