Waarabu waliapa kurudi Zanzibar, Je yanaoendelea ni mapinduzi ya Afrabia?

Waarabu waliapa kurudi Zanzibar, Je yanaoendelea ni mapinduzi ya Afrabia?

Munaendelea kijidhihirisha, Kumbe tatizo ni Uarabu. Wabaguzi wakubwa
 
Je mnakumbuka kitabu cha Dr. Harith Ghassany aliyeandika kitabu chake cha Kwaheri Ukoloni kwaheri Uhuru, ambacho Mzee wetu Mohamed Said(Yumo humu) alikuwa ni research assistant wa kitabu hicho. Mzee wangu Mohamed Said najua una mengi ya kuzungumzia kitabu kile ambacho kwa kiasi kikubwa kilinifahamisha mengi kuhusu mapinduzi ya Zanzibar.

Hata hivyo, mada yangu ya leo sio kuhusu mapinduzi ya Zanzibar wala Muungano maana kitabu kile kina sentensi nzuri niliyoihifadhi tangu nipate kukisoma "Muungano umeficha siri za mapinduzi" kama nitakuwa nakumbuka vyema. Mapinduzi ya Afrabia yameelezewa vizuri sana katika kitabu kile cha Daktari nguli wa falsafa (PhD)

Katika Chapter ya 18, Dr. Harith ametuwekea Mahojiano yalisajiliwa Cairo mwaka 1975 na hayakufanywa na mwandishi wa kitabu. Mahojiano yalikuwa ya Marehemu Sheikh Ali Muhsin wa mwaka 1975 ambapo
ndio kwanza alipotoka jela ni tafauti na Sheikh Ali Muhsin wa siasa za baadae za Zanzibar katika kipindi cha siasa za vyama vingi.

Ali Muhsin alikuwa waziri wa mambo ya nje ya Zanzibar kabla ya mapinzudi, ambapo baadae alishikiliwa jela Tanganyika kabla ya kuachiwa mwaka 1974.

Katika mahojiano hayo, zaidi ya mara moja Ali Muhsin amezungumza zaidi ya mara moja kuwa "Inna aaidun! Tutarudi" Soma uk 239 & 241
View attachment 2664353
View attachment 2664354

Sijui kuhusu harakati za Afrabia zimefikia wapi, kwa wasiojua, Afrabia ni muungano wa Africa na Arabia, ambao kwenye kitabu wameandika

"Kwa ajili ya Wazanzibari na Watanganyika kwa ujumla wao ili kitabu hichi
kiwawezeshe kuzibadilisha nafsi zao. Waweze kuona fursa za mapenzi na neema zilizopo kwao wao na kwa ndugu na majirani zao wa jadi, na kisha wafanye kazi kwa pamoja katika kujenga Muungano Mpya na uhusiano mkongwe baina ya Waafrika na Waarabu—Afrabia—utakaosimama juu ya ukweli na hivyo kuimaliza kabisa mitikisiko na misukosuko ya muda mrefu." Uk Viii
View attachment 2664357

Je, yanayoendelea ni harakati za mapinduzi ya Afrabia?


Sign OLS
Raha ya kusoma ni kwamba kila mtu anafahamu kivyake, yaani huwa hatufanani. Nimemfahamu Ali Muhsin kwamba watarudi kwao Zanzibar kwani wakati huo walikuwa wakimbizi. Ila swala la Afrabia likitokea kwa muktadha alouelezea Dr. Ghassan sio mbaya.
 
Wageni wote tangu enzi nchi zao zilikuwa vizuri, ila walivamia, kwani unadhani wajerumani, waingereza, wareno, waarabu walivyokuja Afrika ilikuwa ni kwasababu ya maendeleo ya Afrika ukilinganisha na nchi zao au ni kutokana na umuhimu wa Afrika kwa maendeleo yao?
Wanakuja ki Biashara, au ulifikiri wanakuja kuwekeza kwenye Bandari kwaajili ya uzuri wa sura zenu?
 
Wakati mkiendeleza mawazo ya vitabu vya historia huko DRC na Rwanda wameshaingia mkataba na DPW tayari.
Rwanda na Kongo ni Machaka ya Wahalifu Wa Kimagharibi Kama ilivyo Falme za Kiarabu.

Dubai ni jiji la raha na starehe za Kila namna . Jiji la kishetani Karika nchi ya Kiislam.
Hata Ulaya ilianza ilipofanikiwa sana ndipo ilipokuja na wazo la kutafuta rasilimali Afrika kupitia mikataba ya kilaghai Kama waliyotuwekea CCM na Serikali yake Kwa DPW
 
Kumbe mkataba hauna shida yoyote,shida ipo kwe anaetaka kupewa mkataba!!!
Sasa mmewaponza watoto wa watu wasiojitambua kuandama mkiwadanganya shida ni mkataba,kumbe sivyo.
Ndio maana hata Kadinali Mwanya nae alisimama kidete
 
Mama ameweka mkataba Wa Vita Miaka 60 ijayo. Waarabu watakua wanachinjwa Barabarani kama kuku. Watoto Wa Wamasai,Wakurya,Wasukuma,Wagogo,Wairak, Wahazabe, Warangi, Wamanyema una Atakua hawana nafasi katika uchumi Wa nchi ya baba zao. Watakua hawana Ardhi ya kulima Wala kufuga katika Ardhi ya Baba zao. Watakua hawana anaona adha ya utumwa kama waliyoiona Babu zetu Karne Moja iliyopita.
Historia itakljirudia.
Vijana Wa Kiafrika watachoka kuishi kama watumwa kwenye nchi Yao.

Nchi itagawanyika vipande vipande, Baba Wa Taifa hili la Tanzania MWALIMU Nyerere na Mzee Karume waliona mbali sana. Aliunganisha taifa hili Kwa gharama kubwa sana. Kwa Afrika ,Taifa kubwa lenye rasilimali nyingi Kama Tanzania kulinganisha na kulifanya taifa moja lenye amani ni jambo kubwa sana. Tukiwadharau Waasisi Wa Taifa hili tutapata tabú sana.
Walishuhudia Kwa vitendo adha ya Kutawaliwa na wageni(Wakoloni) ambao walikuja kama wawekezaji wakati huo.
 
Mungu isaidie Tanzania tupate viongozi mashujaa kama Mwendazake ila mwenye busara kama Wa msoga na democracy kama Samia shida inakuja akipewa hichi hichi hana afu inakua dosari kubwa ama kweli Mungu akupi yote

Sahizi mikataba ya ulaghai kila kona mamaq
 
IMG_20230625_111702.png

Facts from emirates academia
 
Munaendelea kijidhihirisha, Kumbe tatizo ni Uarabu. Wabaguzi wakubwa
Tatizo ni Wageni kupewa Nchi yetu .
Haiwezekani . Tutawarithisha wajukuu zetu Vita na umwagaji Mkubwa Wa damu.

Nyerere na Karume walionja adha ya Kutawaliwa . Wangeweza kuungana nao na kuwaacha Ili kulinda maslahi Yao na familia zao.

Kama tuna uchungu Wa kubinafsisha basi tuanze na Serikali. Imeshindwa vibaya . Tubinafsishe Bunge limeshindwa Hata kutunga sheria zinazodumu Hata miaka 20 Kila mwaka wanabadili Sheria na kutunga sheria mbovu zaidi.
Tubinafsishe mahakama imeshindwa kuisimamia Haki na rushwa imetawala.
Tubinafsishe Jeshi Ili tupate Teknolojia kubwa . Tubinafsishe Police kuondoa rushwa , tubinafsishe Bima ya Afya wameshindwa. Tubinafsishe TTCL imeshindwa, Tubinafsishe Tanroad na Tarura,tubinafsishe Latra imeshindwa. Tubinafsishe CCM mana imeshindwa kuja na será nzuri ya kuwaletea wananchi maendeleo . Tubinafsishe wizara ya Kilimo mana imeshindwa Kutumia kilimo Cha kisasa kwenye nchi yetu.
Tubinafsishe Kila Kitu Kwa sababu tu hatutaki kuumiza vichwa vyetu juu ya matatizo ya watanzania kijacho . Babu zetu walipigania uhuru Wengine wakaooteza maisha Yao Kwa sababu walijitoa kupigania vizazi vijavyo . Sisi tunatekwa na akili zinazowaza starehe na Mali na Sio utaifa Wetu. Waandishi wamepoteza uwezo Wao Kwa sababu wanawaza pesa na Sio taifa lao na vizazi vya watanzania na utaifa wao.
 
Siku zote nilisema shida sio mkataba chuki zipo Kwa waarabu tu nikatukanwa.Ila wangepewa Wazungu kusingekuwa na kelele.
Hukuona Mali za Wazungu zikitaifishwa miaka ya sitini baada ya uhuru. ? Hukuona watu wakiandamana kupinga Wazungu kupewa gesi kule Mtwara?. Hukuona Mrema akipinga Wazungu kule Bulyankulu.Huoni migogoro ya Kule kwenye migodi ya wazungu Mara?

Huoni migogoro ya WAKULIMA na Wafugaji lila kukicha?
Hata Magaidi waliopo Uarabuni kuanzia wale wa Alkaida Wanapinga uchumi Wa nchi Zao kukaliwa na Wazungu.
Hata wajerumani walipinga uchumi Wa nchi yao kukaliwa na Wazungu. Warusi wanapigana na nchi za magaharibi tatizo ni mikataba iliyowekwa miaka iliyopita ambayo inawaumiza miongoni mwao.

Hili ni bara la Afrika Kwa ni nini waafrika wauze utu wao Kwa manufaa ya watawala . Nini Maana ya Demokrasia Kama tunalazimishwa kuuzwa Ili tu Serikali ipate pesa za watawala kula Bata na familia Zao ? Kama wameshindwa wakae pembeni. Wanang'ang'ania nini madaraka wakati wameshindwa kuja na Timu yenye uwezo Wa kujenga uchumi?

Unampaje MTU bandari uliyoijenga kwa gharama kubwa ambayo Mwekezaji atakaa miaka 10 bila kuirudisha Ile tuliyoiweka Kwa miaka 5.?
Tunawawekea Wageni mazingira mazuri ya kuja kuchukua pesa zetu kirahisi wakati huo huo watanzania Wenzetu tunawawekea mazingira magumu huku tukitengeneza mitandao ya Wizi na kupewa na ulaji !

Hiví huyo Mwekezaji angeweza kukusanya mapato wakati ule jiji la Dsm likiwa na miundo mbinu Duni? Malori yanakaa Barabarani kwenye Foleni kutwa Nzima . Mtandao Wa Malipo ya internet ni changamoto?
Tunadanganyana KUWA majirani watawakaribisha Hao wawekezaji. Upumbavu mtupu. Nani asiyejua KUWA wanakimbilia Tanzania Kwa sababu ya Amani na rasilimali watu iliyopo? Wawekezaji wanaoendelea sana nchi zenye Amani lakini zenye watawala wapenda rushwa na madili Ili waimbe wimbo mmoja .
 
Rwanda na Kongo ni Machaka ya Wahalifu Wa Kimagharibi Kama ilivyo Falme za Kiarabu.

Dubai ni jiji la raha na starehe za Kila namna . Jiji la kishetani Karika nchi ya Kiislam.
Hata Ulaya ilianza ilipofanikiwa sana ndipo ilipokuja na wazo la kutafuta rasilimali Afrika kupitia mikataba ya kilaghai Kama waliyotuwekea CCM na Serikali yake Kwa DPW
Hizi hekaya hazitusaidii zinatuacha na ulofa wetu wa miaka yote. Tunajifanya matajiri wa maadili wakati ni makapuku wa masuala mengine yote ya kimaisha.
 
watanganyika bana, munatesa sana na Zanzibar
Kama ambavyo Zanzibar ya Raisi Mwinyi inaitesa sana Tanganyika kupitia Raisi Samia......
Wanasema "What's good for the goose, is also good for the gander"
 
Kama ambavyo Zanzibar ya Raisi Mwinyi inaitesa sana Tanganyika kupitia Raisi Samia......
Wanasema "What's good for the goose, is also good for the gander"

wakati Jiwe anachagua baraza la mawaziri ambalo hata mzenj mmoja hakuwemo muliona ni sawa tu, sasa hivi munalia kwa kuwa na wao wamepata ulaji. Tatizo lenu ni kuwa hamutaki usawa, bali munataka always muwe munawanyonya wao. na ndio mana malalamiko yamekuwa mengi.
 
wakati Jiwe anachagua baraza la mawaziri ambalo hata mzenj mmoja hakuwemo muliona ni sawa tu, sasa hivi munalia kwa kuwa na wao wamepata ulaji. Tatizo lenu ni kuwa hamutaki usawa, bali munataka always muwe munawanyonya wao. na ndio mana malalamiko yamekuwa mengi.
Tungekuwa hatutaki usawa kama unavyodai hapa, sidhani wazanzibari kama Bakhresa, Mwinyi, Dr Salim na wengine wangeruhusiwa hata kumiliki ardhi huku Tanganyika. Ardhi siyo suala la muungano lakini bado wapemba wengi wanamiliki maelfu ya hekta za ardhi ila sisi watanganyika huwezi kutusikia tunalalamika hata siku moja au kuwafanyia vurugu.

Ardhi ndiyo utajiri mkuu wa Tanganyika, ila tunawapa wazanzibari ruhusu kuja kuishi kwetu....
 
Tungekuwa hatutaki usawa kama unavyodai hapa, sidhani wazanzibari kama Bakhresa, Mwinyi, Dr Salim na wengine wangeruhusiwa hata kumiliki ardhi huku Tanganyika. Ardhi siyo suala la muungano lakini bado wapemba wengi wanamiliki maelfu ya hekta za ardhi ila sisi watanganyika huwezi kutusikia tunalalamika hata siku moja au kuwafanyia vurugu.

Ardhi ndiyo utajiri mkuu wa Tanganyika, ila tunawapa wazanzibari ruhusu kuja kuishi kwetu....

Kama ndio utajiri mkuu, msengeuziana Ekari kwa elfu 50.

Na HIlo tatizo la ardhi mumelitengeneza nyinyi, serikali mbili zinaondoa moja kwa moja uwepo wa Tanganyika kwahiyo wazanzibar wana haki zote za utanzania kama mulivyo nyinyi. Mumekuwa mkiambiwa kuhusu serekali tatu kwa miaka mingi sana lakini hamkuwa mkishuhulika kabisa, cha ajabu hao munaosema wanufaikaji wa huu muungano wao ndio wamekua wakiupinga. huku nyinyi mkiwakebehi kuwa wanapenda kulalamika.
Watanganyika uelewa wao kuhusu Zanzibar ni mdogo sana na ndio mana wanajirop[okea tu mitandaoni
 
Back
Top Bottom