Waarabuni hutumia Islam to colonize countries kama vile wazungu walivotumia Ukristo

Waarabuni hutumia Islam to colonize countries kama vile wazungu walivotumia Ukristo

beatiful thing about islam vs christianity debates ni kwamba imani zote zilihusisha ukandamizaji huko awali, kwa hilo hakuna wa kujifanya mbora kuliko mwengine

ndio maana wenye busara zao wakasema kuamini na kutoamini ni haki ya binadamu kila mtu afuate imani zake kivyake
 
halafu pia si ni lengo la wakristo kufanya dunia nzima iwe wakristo pia, au we mwezetu wakristo gani gani hao uwajuao wasio na ajenda ya kuusambaza ukristo kama tu waislamu watakavyo uislamu usambae
Yes, lakini sio kwa upanga na kutishia watu kuwaua wanapotaka kuhama dini.
 
kwanza kabisa hapo kwenye maeneo matakatifu ya kiislamu yote yapo uarabuni sio kweli, kuna maeneo yapo israel, mengine ya uajemi, mengine yapo hata hapa Tanzania unaweza kudhuru misikiti ya zamani, ni vile tu yale maeneo ya uarabuni yametajwa tangu mwanzo katika Quran na kama Makka ni lazima kwenda kwa muislamu mwenye uwezo ila si kweli hakuna maeneo mengine matakatifu kwa waislamu.

halafu kuhusu kiarabu kuonekana ndio lugha rasmi ya ibada, unapaswa ujue dini zote zilikuwa hivyo huko mwanzo,

na kwamba hadi leo hii wayahudi lugha yao takatifu ni kiebrania hata wakisali husali kwa lugha hiyo, wakatoliki walizungumza na kusali kilatino hadi pale Papa wao aliposema inaruhusiwa kusali lugha ingine, ila ukienda vatican hadi kesho wanatumia kilatini ijapokuwa kuna lugha ya kiitaliani ambayo ndio lugha izungumzwayo maeneo kuzunguka vatican yote,

wahindu hadi kesho kutwa wakisali hawasali kihindi wanasali kwa kutumia lugha ya kale iitwayo sanskrit

na uonapo waislamu wasio waarabu wamevaa hijab ama makanzu jua tu ni kutokana na aya za Quran, ukisoma mafundisho yake utapata kuona vazi la hijab limeelekezwa liwe kama lilivyo, wakati kanzu halina maelekezo ya moja kwa moja, ila linaonekana linaendana sana na maelezo ya stara anayopaswa mtu wa kiislamu wa kiume awe nayo, kama vile kuvaa nguo kuvuka magoti, na kuvaa nguo kufunika kifua , halafu haibani

kuhusu waislamu wote kuwa eti wanalazimika kuwa na utamaduni mmoja sio kweli, waislamu tupo wa aija nyingi, muislamu wa saudi arabia na waafrika wana mitazamo tofauti, muislamu wa malaysia ana mtazamo tofauti na muislamu wa india.

ndio maana hata hapa Tanzania waislamu wa asilo tofauti huwa hawachangamani sana kwasababu wana tofauti kubwa za kitanaduni na kimtazamo wa dunia na dini pia
Apologist excuses.
 
Yes, lakini sio kwa upanga na kutishia watu kuwaua wanapotaka kuhama dini.
hayo ya kutishia watu wakihama dini sijui upanga, hayo yote yanatokana na tafsiri za kibinadamu, ila Quran yenyewe ipo very clear kuwa dini ni kitu cha hiyari, kwa maana hata uislamu ulipoanza waislamu walipigwa vita na kuuwawa na waarabu waliokuwa na dini nyenginezo za asili, ila waislamu kwa hiyari walibaki na uislamu wao, hadi pale kwa rehema za mwenyezi Mungu akawasaidia wao waislamu wakashika mamlaka ya maeneo yote ya makabila ya kairabu.

kwahiyo waislamu walipigana kupinga udhalimu wa makabila ya kiarabu kupinga waislamu kuabudu Mungu kwa imani yao

same way kama warumi walivyopinga wakristo wa mwanzo na baadae wakristo wakafanikiwa kuiweka Roma chini ya ukristo.

sasa hayo ya upanga kusambaza dini huko baadae hayo yapo kwenye ubinadamu sasa, na jinsi watu wanavyotafsiri vifungu vya Quran, ambavyo kwanza vingi vilishuka kwa muktadha maalum, inabidi mtu aelewe kwanini viliandikwa kama vilivyoandikwa katika Quran, sio kuvitafsiri tu vyenyewe bila kujua stori yake yote katika hiyo Qurani,

ni kama biblia ilivyojaa aya za kuagiza waisraeli wapigane kikatili kabisa na wafilisti, ambapo ilikuwa kwasababu, wale walifanya imani za kukufuru na dhambi na huku wakipinga waisraeli, sasa pata picha mtu atumie aya hizo hizo aseme ukristo umeruhusu kuua, si kweli, kwa maana vile vifungu bipo kwa sababu ya yaliyoteka wakati huo, same na Quran aya za kisapoti Jihad zilishushwa kulingana na hali waliyopitia waislamu wakati huo dhidi ya waarabu waliofuata dini za makabila yao badala ya uislamu

pia kwenye harakati za kusimamisha dola zao na dini zao watawala wengi, hufikia hatua ya kutumia huo upanga, ila si kwamba dini hasa ilisema tumia upanga kusambaza dini, bali sasa ni utashi wao, na wanatumia hizo aya za Quran kujustify matendo yao, same hata watawala wa kikristo wengi katika historia walitumia biblia kujustify maovi yao
 
Apologist excuses.
thats your view, but as a muslim, i have my own perspective as how i see things, thats why i am still a mislim, and you have your own perspective of things thats why you are still a christian and not muslim

ndio maana suala la imani suala binafsi, kila mtu ana mtazamo wake na jinsi aonavyo upande wake ni sahihi

dini ni hoja, waislamu tuna hoja zetu, na nyinyi mna zenu, na sisi tunajua tuko sahihi kama mjionavyo nyinyi, na sisi tunaona nyinyi bado hamjui kitu na mmepotea kama nyinyi mtuonavyo sisi

dini ni suala mtambuka ndugu yangu lila mtu aamini yake
 
same way kama warumi walivyopinga wakristo wa mwanzo na baadae wakristo wakafanikiwa kuiweka Roma chini ya ukristo.
Kuna mambo mengi hapo juu umeandika ambayo hayaendani kabisa na historia ya jinsi uislamu ulivoanza na historia ya muhammad, lakini kwa sababu hata nikivisema bado itakuwa ni mitazamo ya wanahistoria, kwa sababu nyie waislamu hamuamini historia yeyote ya uislamu ambayo iko nje ya Qur'aan na hadith zenu hata kama ni authentic, bac kwa hilo ngoja nisiyaseme.
Lakini hilo swala hapo juu nililo-qoute umedanganya wanajukwaa, wakristo hawajawahi kuiweka rome chini yao, rome adapted Christianity, soma historia ya Mfalme wa roman empire Constantine ambaye alibadili dini kuwa mkristo na warumi wote baadae wakamfatisha, Romans killed christians brutally(soma history of the colosseum) ukisema christians walifanikiwa ukiweka rome under their grasp wanahistoria watachanganyikiwa kwasababu Christianity was very weak back then, kiufupi that was impossible, rome walikuwa na miungu yao na Jews walimkataa yesu, so they were helpless.
Kilichomfanya Constantine awe mkristo ni story ndefu ambayo haina maana hata nikiizungumzia, ipo nje ya mada.
 
Back
Top Bottom