Waasi waalika jumuiya za EAC na SADC waje maeneo yaliyokombolewa na AFC/M23

Waasi waalika jumuiya za EAC na SADC waje maeneo yaliyokombolewa na AFC/M23

Hujasikia habari za huko Kongo Wanamgambo wa Wazalendo wamekuwa wakiua na kuwala raia wa Kitutsi?!
Vipi wazalendo wamebadili tabia, maana Kuna mahala uwapongeza Kwa uzalendo wao wakupiga jeshi la Congo.
 
19 February 2025
New York

Balozi wa Kudumu wa Rwanda katika Umoja wa Mataifa alaani serikali ya DR Congo kwa 'kutumia njia ya kijeshi' katika mzozo wa ndani ya nchi hiyo

View: https://m.youtube.com/watch?v=Urb9VHRkxQ0

Akizungumza katika mkutano wa Baraza la Usalama kuhusu DR Congo Februari 19, 2025, Mwakilishi wa Kudumu wa Rwanda katika Umoja wa Mataifa Ernest Rwamucyo alisema .. mazungumzo ni njia sahihi siyo njia za kijeshi

Balozi Ernest Rwamucyo ameongeza kuwa njia sahihi ni kwa wadau wote walio katika mzozo wa Congo wakae katika meza ya mazungumzo ikiwemo makundi yote wakiwemo M23 ili kupata suluhisho la mgogoro huo wa ndani ya nchi ya Congo kama ambavyo mkutano wa Dar es Salaam wa tarehe 8 February 2025 wa viongozi wa nchi za EAC na SADC Juu ya Mzozo wa Congo ulivyopendekeza..

Rwanda pia imemtaka rais wa DR Congo kuacha mtindo wake wa kukacha mikutano muhimu kama ile ya kikanda ya Dar es Salaam na Addis Ababa juu ya mzozo wa DR Congo. Hivyo kutokuwapo kwa rais wa Congo katika mokutano hiyo Felix Tshisekedi anahujumu na ameua nafasi nzuri ya kutatua mzozo huo kikanda.

Utawala wa Kinshasa umeamua kugawa ovyo silaha kwa silaha kwa vijana na watoto kuchochea zaidi vita vya ndani ya nchi ya Congo, na tunaona hali hiyo imetumiwa kusambaza taarifa potofu za watoto kuuawa wakati ni jeshi la serikali la FARDC kugawa silaha kwa vikundi vya mgambo kwa jina la wazalendo na watoto ambao hawajapitia mafunzo rasmi ya kijeshi wala kuongozwa na mfumo rasmi wa kijeshi umekoleza moto mauaji ya kikabila na matumizi yasiyo sahihi ya silaha zilizozaga ovyo kwa makusudi

Rwanda pia imeshambuliwa na majeshi ya kigeni yaliyopo ndani ya DR Congo na kuua raia 16 wa Rwanda pia mali zao kuharibiwa. Hili jambo linahitaji kulaaniwa na Jumuiya ya Kimataifa

Kuwepo kwa mamluki, askari wa kukodiwa, MONUSCO, SAMIDRC, Majeshi ya Mamluki ya Nje kumefanya eneo hili la Mashariki ya Congo kukosa utulivu kutokana na mchanganyiko wa majeshi haya ya kila aina. Hali hii imekuwa tishio kwa nchi ya Rwanda
 
Vipi wazalendo wamebadili tabia, maana Kuna mahala uwapongeza Kwa uzalendo wao wakupiga jeshi la Congo.
Sijawahi kuwapongeza Wazalendo Millitias nisome vizuri wao na askari wa FRDC wamepora maduka ya Wananchi huko Goma Bukavu na Miji na Vijiji,baada ya hii Vita kuisha kuna haja ya sisi Nchi za Africa ya Mashariki tukawasaidie DRC kujenga Jeshi lenye NIDHAMU na lenye uwezo wa Kudefend Borders liwe kama JWTZ RDF UPDF KDF nk.
 
Senge hawaaa

Naangalia MAITI zaidi ya 140 zimekutwa kanisan na zingine ziko uchi zilibakwa alafu mnashabikia ungese

Shame n u
 
Kwa hali ilivyofikia binafsi sitaki aongee na waasi. Natamani M23 wafike Kinshaza na kuiteka Congo yote. Huenda Congo ikaja kupata Serikali mpya itakayojumuisha makabila yote, yenye vyombo imara vya ulizni na usalama na itakayoleta amani ya kudumu kwa mara ya kwanza.
Waafrika daima tuwe tunaweka Dialogue mbele huu muungano wa Waasi wa AFC unaweza kufika Kinshasa halafu ukaanza kugeukana kama wakati wa Hayati Laurent Desiree Kabila.
 
20 February 2025

DR Congo: Usafiri wa meli unaanza tena kwenye Ziwa Kivu baada ya marufuku ya wiki nne​


View: https://m.youtube.com/watch?v=Qv7zgIVlQSY
Usafiri umeanza tena katika Ziwa Kivu baada ya kupigwa marufuku kwa wiki nne kutokana na mapigano katika eneo hilo.

Biashara imeruhusiwa kwa mara nyingine tena kati ya Goma na Bukavu ambayo ni miji miwili mikubwa mashariki mwa nchi katika fukwe za pande mbili za ziwa Kivu, inayodhibitiwa na M23, wakishirikiana na wanajeshi wa Rwanda.

Kuna barabara ya kuunganisha miji hiyo miwili ila usafiri wa majini ni wa uhakika na salama zaidi ya usafiri wa barabara.

Abiria waliosafiri kwa meli wamesema wanashukuru amani pia usalama imerudia eneo hilo na sasa wanaweza kuendelea na maisha kama kawaida.

Bukavu inategemea mazao ya chakula yanayozalishwa kwa wingi katika maeneo yanayozunguka mji wa Goma ulio upande wa pili wa ziwa hilo.
 
Back
Top Bottom