Wabara ondoeni shaka, ardhi ya SMZ Bagamoyo si sehemu ya Zanzibar. SMZ haina hati; limetelekezwa miaka 45 ila Zanzibar inamiliki kihalali

Umelisoma bandiko hili tangu mwanzo?, hukuona the authority niliyoitumia?. Sii wengi wanajua kuwa sisi watu wa media we are an authority of our own!. Sisi ni mhimili!, the fourth Estate or the Fourth Protocol!.
P
Ngoja uitwe tena Bungeni kujieleza. Tanzania ina Wanahabari wangapi? Wote hawajui lolote zaidi ya wewe?
 
Hoja nyingine zinatia hasira!. Uraia wa JMT ni uraia wa aina moja!. Haki za kiraia kwa Mtanzania zinafanana kabisa!, kuna Watanzania bara wanajidhania wana haki zaidi kuliko Wanzanzibari!, ni wajinga tuu.
P
Kama raia wote wa Tanzania wana haki sawa, kwa nini raia kutoka Tanganyika hawaruhusiwi kumiliki ardhi kwenye baadhi ya meneo ya Tanzania? Haki za kirai za watanzania hazifanani hata kidogo. Kuna raia wana haki zaidi.

Point ya msingi ni kuwa nchi mbili ziliungana na kukubaliana kuwa hawatashirikiana ardhi, fullstop. Ndivyo inavyotakiwa kuwa. Mmoja akitaka ardhi ya mwenzake afuate utaratibu kama muwekezaji wa kigeni.
 
Hata Kama. wakienda kutafuta maisha zbar hawaruhusiwi kwa sheria za zbar kumiliki ardhi huko,
Kwa namna ulivyoliweka siyo kweli. Mtanzania kutoka bara akikaa Zanzibari miaka 10 au zaidi mfululizo huhesabika ametimiza shariti la kisheria la kuwa mkazi wa Zanzibari na hivyo kupewa kadi ya ukazi wa Zanzibar ambayo humpa stahili ya kumiliki ardhi na stahili zingine zote za wakazi (raia) wa Zanzibar. Ni ukazi mfululizo na siyo wa kwenda na kurudi bara. Hii ni kwa sababu Zanzibar ni eneo dogo sana (sawa na wilaya moja kama Bagamoyo). Bila sharti hili sasa hivi wazanzibari wote wangalikuwa ni wanyamwezi wa Tabora! Huku bara wakazi wa Zanzibari wanaruhusiwa kumiliki ardhi eneo lo lote bara kama watanzania wengine, wakati wo wote. Hii ni kutokana na kwamba wao ni wachache sana, ni kama a drop in the ocean.
 
Uchache wao siyo hoja. Mtu mmoja anaweza miliki hata ekari 10,000 au zaidi. Uchache kwenye ardhi siyo hoja.
 
Nimeshanga sana kuona watu huku wanaona jambo geni
Kweli watz wako nyuma sana kujua mambo

Ova
Nadhani wengi waliomo humu ni vijana waliozaliwa kuanzia miaka ya 1985 kuja hadi 2000s. Tatizo jingine hawajishughulishi na kufahamu historia za nchi zao zaidi ya yale waliyofundishwa shuleni. Halafu badala ya kutafuta ukweli wa hizo habari wanakuja na mihemko zaidi. Samahani kama nitawakwaza wanangu!!!😂😂😂
 
Hili sikuwahi kulijua ndio nalisikia leo, ila hakuna tatizo, hao wafungwa ni Watanzania hivyo wanaweza kufanyishwa kazi popote. Hata wale masheikh wa uamsho, tumewashikilia kwenye magereza ya huku bara!.
P
Hivi wale masheikh bado wako ndani mpaka sasa??? Nakumbuka kuna kipindi waliachiwa au ilikuwa ni baadhi tu???
 
Kumbe vyenu vinawauma eee watanganyika nyau Sana mbona huku mmejaa wasikuma mnalala mpaka barabarani ZANZIBAR inapoteza haiba imepotea ustaarabu wakinzanzibar umetoweka HESHIMA utu ukarimu vyote vimeondoka mijitu inaokula tumbaku na kufanya mauwani na ujambazi imetapakaa

Isiwe shida chukuweni Bagamoyo yenu tuachilieni visiwa vyetu
Mtanganyika go home
Zanzibar NI Ardhi yetu na tutarithisha vizazi vyetu

Mayala maanake NI NJAAAA
NJAAAA ya kututawala
NJAAAA ya kutuua katika chaguzi
NJAA yakutamani Mali zetu
 
JPM alikuwa mzalendo wa kweli wa Tanzania, wengi bado wanamuombea Mungu apumzike kwa amani, mimi nimeisha elezwa alipo Voices From Within: Je, wajua yuko Peponi, Mbinguni, Kwa Baba yake? Why kumshutumu, kumsakama na kumsimanga? Aachwe apumzike kwa amani ni anakula raha kwa kwenda mbele.
P
 

Mujarabu sana

Shukrani mkuu Pascal Mayalla
 
Muungano wa abracadabra tu

Hata haueleweki.

Kuna mmoja ni kupe mzee wa kujiliza Liza tu.

Mwengine anapenda visivyopendeka.

Nchi Ile Ina vituko sana aisee
 

Hadhira haikuelewi.

Maana maandiko haya ni utafiti na uchunguzi wa kina.

Hadhira haijazoea!

Fanani haya yaliyomo yamo.

Aksante
 
Ardhi sio issue ya muungano, Zanzibar ina Ardhi yake na Tanzania bara ina Ardhi yake.
P
Ardhi sio suala muungano.

Mzanzibar anamilika ardhi Tanganyika.

Mtanganyika harusiwi kumiliki ardhi Zanzibar na ikijulikana ni kimbembe. Ajabu.

Serikali ya SMZ wanamilika eneo kubwa ardhi Tanganyika.

Huu ni unyonyaji wa kimuumgano kama sio upendeleo usio na haki.
 
Slogan-fiche ya Wazanzibar ndani ya huu Muungano ni ile ya Changu Changu, vyao Vyetu.
 
Mkuu dega, kwanza ni nimekueditia andiko lako na kukupiga darasa
  1. Majina ya nchi yanaanza na capital letters.
  2. Neno la kawaida halihitaji capital letters
  3. Kama No.1
  4. Full capitals ni heading
  5. Kama No.2
  6. Ni two word
  7. Kama No.1
  8. Missing letter
  9. Kama No.4
  10. typo
rekebsha... mimi nilipaswa kuwa Mwalimu wa chekechea hadi darasa la 3!.
P
 
Ardhi sio suala muungano.
Ni kweli
Mzanzibar anamilika ardhi Tanganyika.
Kwanza hakuna Tanganyika, pili tuna uraia wa aina moja tuu, Mtanzania!. Kwenye haki za kiraia ikiwemo kumiliki ardhi, hakuna Mtanganyika, hakuna Mzanzibari, kuna mtu mmoja tuu, Mtanzania, awe alikuwa Mtanganyika au Mzanzibari wote wana haki sawa za uraia.
Mtanganyika harusiwi kumiliki ardhi Zanzibar na ikijulikana ni kimbembe. Ajabu.
Zanzibar ina special stutus ya utawala wa ndani ambapo ardhi yake ni mdogo, tiny very minutes, hivyo ni kwa Wanzanzibari wakaazi pekee!.
Serikali ya SMZ wanamilika eneo kubwa ardhi Tanganyika.
Ni kweli ni haki yao na halali yao, walipewa zawadi na Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere.
Huu ni unyonyasaji wa kimuungano kama sio upendeleo usio na haki.
Sio unyanyasaji wa kimuungano ni faida na matunda ya muungano.
P
 
visiwa vyao ni very tiny, tukiruhusu kila Mtanzania kumiliki ardhi Zanzibar, itaelemewa na kuvizamisha visiwa vile!.

Wakati wa kuumbika nchi, Zanzibar ilikuwa eneo la bara likamegeka kwa sea erosion

Hapa Paskali unaweza kutuweke proof? Dhana ya kwamba Unguja/Pemba zilikuwa Part ya Ardhi ya Tanganyika before erosion au ndiyo Elimu ya kukariri "Big Bang Theory"?

Visiwa vitazama kwa kuzidiwa na nini? Hiyo erosion ilitokeaje? Hivi unajua kwamba maji yakitoka ardhi ya Unguja/Pemba kuja Tanga/Dsm ni flat tu wala hakuna bonde? Na yakijaa unaweza kuzamisha hata minazi mitatu kwenda chini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…