Wabunge 19 wa CHADEMA watinga Mlimani City

Wabunge 19 wa CHADEMA watinga Mlimani City

mkalamo

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2013
Posts
340
Reaction score
359
Zikiwa zimesalia saa kadhaa mkutano wa baraza kuu la Chadema Kuanza,wabunge 19 wa bunge la Jamhuri ya Muungano wanaotokana na Chama hicho wamewasili maeneo jirani na kunapofanyika mkutano huu hapa Mlimani City.

Awali kulikuwa na sintofahamu ikiwa watahudhuria mkutano huo,walioalikwa kwa barua Rasmi za Chama zikiwatambua kuwa wanachama tofauti na kauli za awali kuwa si wanachama wa Chama hicho.

Wakati wabunge hao wakiwa maeneo haya ya Mlimani City,mjadala ulioanza usiku wa Jana na unaoendelea Sasa ni kama wabunge hao wahojiwe mbele ya baraza hilo,au wakahijiwe vyumbani ambapo tayari vyumba vitatu vimetemgwa kwa ajili hiyo.

Baadhi ya wajumbe wanaeleza ni muhimu wakahijiwa hadharani kila mmoja asikie kuliko kuitwa Chumbani na wajumbe kuja kupewa taarifa ya mahojiano hayo,huku kukiwa na taarifa za awali kuwa wabunge hao wameshafutwa uanachama na kinachosubiriwa ni baraza kuu kuhalalisha Jambo hilo.

Hisia hizo zinachangiwa zaidi na amaelezo ya John Mrema Mkuu wa Itifaki na mambo ya Nje Chadema wakati akizungumza na vyombo vya habari kuwa uamuzi umeshafanyika,na kinachosubiriwa ni kutangazwa.

Kauli ya Mrema inatakwa kupoka uamuzi wa baraza kuu hali iliyozua sintofahamu miongoni mwa wajumbe wa kikao hicho

Kwa Sasa viongozi wakuu tumekubaliana kuwatumia influence wa Chama kushawishi katika mitandao ya kijamii juu ya uamuzi huu ikiwa ni njia ya kuwaandaa wanachama kutohoji Jambo hilo kuamuliwa nje ya baraza kuu

Stay Tune
 
Kwa Sasa viongozi wakuu tumekubaliana kuwatumia influence wa Chama kushawishi katika mitandao ya kijamii juu ya uamuzi huu ikiwa ni njia ya kuwaandaa wanachama kutohoji Jambo hilo kuamuliwa nje ya baraza kuu
Nimependa hii ya Viongozi wakuu wachama mmekubaliana. Sasa kama mmekubaliana unakuja nini kutusumbua huku?
 
Sidhani kama CHADEMA wanao ubavu wa kuwatema hawa Covid-19. Sanasana watapewa onyo na kupewa Baraka za kuendelea na Ubunge wao. Mwisho wa siku Chama kuendelea kupokea ruzuku
 
Ni lazima wafukuzwe, mchakato halali kupata wabunge halali ufanyike, kwa sasa hawa uwepo wao bungeni wanajiwakilisha wao wenyewe, hivyo hata kupinga vitu ambavyo vinawaumiza wananchi hawawezi, miswada mibovu inapita bila wao kutoa neno. Ninataka mchakato halali ufanyike kupata wawakilishi halali!
 
Whatever the case, Mbowe ndio muamuzi! Tutulie na kusubiri nini ataamua. Akitaka kuwasamehe mtabadili gia angani penda msipende. Hizi siasa zetu usiwe na maneno mengi sana! Subiri matokeo!
Sio kweli.

Kama ni suala la kubadili gia angani hata yule "mzalendo" wenu Dr. Slaa alikuwepo ukumbini siku ya kumtambulisha Lowassa, akapiga nae picha na tabasamu la kutosha kuonesha aliridhia ujio wa Lowassa ndani ya Chadema.

Alivyokosa alichotaka ndio kisirani kikamuanza akaishia kufungiwa ndani na mkewe. Kama Mbowe angekuwa na mamlaka ya kufanya chochote anachotaka, naamini asingesubiri kuitisha Baraza Kuu ili aamue kuhusu hao wanawake 19, angeumaliza mchezo siku nyingi.
 
Zikiwa zimesalia saa kadhaa mkutano wa baraza kuu la Chadema Kuanza,wabunge 19 wa bunge la Jamhuri ya Muungano wanaotokana na Chama hicho wamewasili maeneo jirani na kunapofanyika mkutano huu hapa Mlimani City...
Yaan kuwafukuza uanachama, watu ambao wamewasupport miaka yote ni tena kwa nguvu ni UDHAIFU!
 
Zikiwa zimesalia saa kadhaa mkutano wa baraza kuu la Chadema Kuanza,wabunge 19 wa bunge la Jamhuri ya Muungano wanaotokana na Chama hicho wamewasili maeneo jirani na kunapofanyika mkutano huu hapa Mlimani City.

Awali kulikuwa na sintofahamu ikiwa watahudhuria mkutano huo,walioalikwa kwa barua Rasmi za Chama zikiwatambua kuwa wanachama tofauti na kauli za awali kuwa si wanachama wa Chama hicho.

Wakati wabunge hao wakiwa maeneo haya ya Mlimani City,mjadala ulioanza usiku wa Jana na unaoendelea Sasa ni kama wabunge hao wahojiwe mbele ya baraza hilo,au wakahijiwe vyumbani ambapo tayari vyumba vitatu vimetemgwa kwa ajili hiyo.

Baadhi ya wajumbe wanaeleza ni muhimu wakahijiwa hadharani kila mmoja asikie kuliko kuitwa Chumbani na wajumbe kuja kupewa taarifa ya mahojiano hayo,huku kukiwa na taarifa za awali kuwa wabunge hao wameshafutwa uanachama na kinachosubiriwa ni baraza kuu kuhalalisha Jambo hilo.

Hisia hizo zinachangiwa zaidi na amaelezo ya John Mrema Mkuu wa Itifaki na mambo ya Nje Chadema wakati akizungumza na vyombo vya habari kuwa uamuzi umeshafanyika,na kinachosubiriwa ni kutangazwa.

Kauli ya Mrema inatakwa kupoka uamuzi wa baraza kuu hali iliyozua sintofahamu miongoni mwa wajumbe wa kikao hicho

Kwa Sasa viongozi wakuu tumekubaliana kuwatumia influence wa Chama kushawishi katika mitandao ya kijamii juu ya uamuzi huu ikiwa ni njia ya kuwaandaa wanachama kutohoji Jambo hilo kuamuliwa nje ya baraza kuu

Stay Tune
Rubbish, takataka
 
Dalili zinaonesha hawafukuzwi, bado wapo sana nguzo za chama
 
Back
Top Bottom