Wabunge 30 wa Tanzania kwenda Dubai safari ya kimya kimya si kawaida

Wabunge 30 wa Tanzania kwenda Dubai safari ya kimya kimya si kawaida

LOBBYIST KUCHOMOZA NDANI YA BUNGE LA 11 LA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO

Siku ya jumamosi tarehe 10 June 2023 tutasikia wabunge Influencers-mitandaoni walioenda Dubai kwa siri wakigonga meza wakati mawasilisho ya Kamati ya Kudumu ya Miundo-Mbinu ya Bunge ikiwa bungeni Dodoma Tanzania kuhusu mapendekezo yao ya kubariki mradi wa bandari za Tanzania chini ya usimamizi wa DP World
 
LOBBYING NDANI YA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Wachagiza muelekeo wa kushawishi (lobbyists) matokeo ya bungeni kuanikwa

Toka maktaba
22 May 2023

Mbunge Assenga - Wasitucheleweshe mradi wa DP World kuhusu mapinduzi ya Bandari kuongezea mapato serikali


Mbunge wa Kilombero, Abubakar Assenga ameitaka serikali kuacha kujivuta kwenye masuala yanayoweza ongezea nchi mapato hususan uendeshaji wa bandari, akisema kuna fursa nyingi za kupata fedha za kutosha kama mchakato wa kumpata mbia wa kuendesha bandari utaharakishwa.


Lobbyist - a person who takes part in an organized attempt to influence legislators
 
Mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Joseph Kasheku Musukuma akiongea bungeni amesema walikwenda Dubai kuona mafanikio ya bandari za huko.

ZIARA YA KAMATI YA MH. PROF. MBARAWA YA WABUNGE 30 DUBAI




Jambo la kushangaza ni kuwa kamati ya Bunge wakitembelea miradi ndani ya Tanzania huwa tunaona habari hizo katika media zetu mfano kamati ya Bunge imetembelea mradi wa SGR Reli au Kamati ya Wabunge ikiongoza na mwenyekiti wa kamati maalum wametembelea mradi wa ujenzi wa meli kubwa ziwa Victoria n.k

Lakini ziara hii ya kutembelea Dubai ilikuwa ya
kimya kimya na usiri mwingi inaacha maswali mengi sana miongoni mwa watanzania wengi wanaofuatilia sakala hili la bandari kuuziwa DP World ya Dubai.

Haraka ya Bunge kufanya overtime siku ya jumamosi tarehe 10 Juni 2023 kupitia mkataba huu wa mradi wa bandari za Tanzania huku tayari ma 'influencers' 30 waliozuru Dubai wakiwa wakali wanataka haraka kuchagiza kukamilisha utekelezaji wa miradi kama mbunge Joseph Kasheku Musukuma alivyosema bungeni siku chache kuhusu 'ucheleweshaji' wa miradi.

TOKA MAKTABA :
Kamati ya Bunge LAAC ya wabunge kadhaa ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yatembelea Miradi ya Maendeleo Mtwara

View attachment 2650841
29 Mar2023
Kamati ya Kudumu ya Bunge Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) imekataa taarifa ya mkurugenzi wa halmashauri ya manipsaa ya Mtwara Mikindani kwa kushindwa kutekeleza agizo la kupeleka milioni 600.2 (40%) za fedha za miradi ya maendeleo badala yake ametoa 400.7 (16%) tu kati ya makusanyo ya shilling billion 2.6 kwa mwaka wa fedha 2020-2021.

tuwekee majina ya hao wasaliti tuwajue ili tukawashtaki kwa wananchi wao ili wawakatae akiwa mjinga msukuma.
 
Kwahiyo hao wabunge 30 ndo walipewa kila mtu V8 km ya msukuma, tena 0 kilometers??

Tumekwishaaaaaaaaa!! Woiiiiiii
 
tuwekee majina ya hao wasaliti tuwajue ili tukawashtaki kwa wananchi wao ili wawakatae akiwa mjinga msukuma.

Picha za wana kamati ya 'Mbarawa' ya miundo mbinu inaelezea majina.
 
Walivotoka huko msukuma akajakuvuta shangingi zero kilometa.
 
Waandishi wetu wa habari wanaposhindwa kuhoji wabunge wetu kuhusu mambo mbalimbali ikiwemo ukwasi wao mpya



 
LOBBYING NDANI YA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Wachagiza muelekeo wa kushawishi (lobbyists) matokeo ya bungeni kuanikwa

09 June 2023

Mbunge Joseph K . Musukuma hatimaye ajitokeza na kuwa mtetezi wa mkataba wa mradi wa bandari



Mbunge wa Geita Vijijini (CCM) Joseph Musukuma amesema kuwea mkataba wa uwekezaji wa bandari bado haujasainiwa na hakuna anayeujua kwani bunge litajadili maazimio ambapo baada ya maazimio hayo ndio mkataba wa uwekezaji utaandaliwa.
 
Wakili Fatma Karume - Suala la Kuuzwa Bandari kwa DP World



Wakili Fatma Karume mbobezi wa Investment law na mikataba ya kimataifa
  • Nafasi ya mwanasheria mkuu wa serikali jaji Feleshi kuwa mshauri mkuu katika jambo hili
  • Nakubali na kuielewa kauli ya Freeman Mbowe kumtaka Rais kuwa makini kwani pia waziri wa masuala ya bandari ni mzanzibari hivyo politically/ kisiasa linaleta hisia za kitaifa
  • Kitu kinachosumbua sijawahi kuona bilateral agreement treaty iliyo one-sided kiasi ya kuwa Tanzania haitaambulia chochote
  • Bilateral agreement hii inalenga kuilinda kwa namna yoyote ile
  • Hakuna reciprocation baina ya pande mbili
  • Mkataba ni wa kikoloni
  • Dubai kutaka DP World ilindwe na sheria za kimataifa ni matunda ya mfumo wa mahakama wa Tanzania kutoaminika
  • Inasikitisha kuona karne hii Tanzania inaingia mikataba ya kikoloni ya 1884 ya mabeberu wakoloni kujipendelea kwa kila hali
  • Serikali ya Tanzania ina sifa ya kuwa Gas Lighting per extraordinary kupita nchi yoyote ya kiafrika yaani kujikausha kila kitu kipo sawa wakati kila mmoja anaona haupo sawa kabisa
  • Attorney General ameipa sovereignty yote ya Tanzania kwa Dubai kwa mujibu wa Article 7(3) katika mkataba kumpa veto rights haki isiyo na kikomo aliouingiza Tanzania
  • Guarantee ya stabilisation kwamba concession baina ya Tanzania na DP World maana yake sheria vilizoingia wakati wa mkataba zibaki hivyo milele
  • Ingawa DP world wamekubali kutumia sheria za kodi za Tanzania lakini ndani ya mkataba kipengele cha Tax regime is stabilised maana yake kodi za Tanzania wakati mkataba unaingiwa utabaki vilevile na hawezi kubadilisha siku za usoni
  • Bilateral investment treaty ulitakiwa kuwabeba hata waTanzania waliowekeza / invest huko Dubai na siyo kwa DP World pekee, huu ni unyonge usiokubalika katika mkataba huu wa baina ya nchi mbili
 
Back
Top Bottom