Wabunge msiotosheka na 12M, achieni ngazi young graduates wachukue nafasi zenu

Wabunge msiotosheka na 12M, achieni ngazi young graduates wachukue nafasi zenu

moyafricatz

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2015
Posts
2,904
Reaction score
4,902
Wanabodi,

Nimesikitishwa sana na kitendo cha yule Mbunge juzi kutoa hoja ya wao wabunge waongezewe mishahara maana wana kazi nyingi sana.

Kama hilo halitoshi Mbunge yule ameenda mbali akisema hata malipo ya mishahara yao yafanyike kwa malipo ya dola za kimarekani. Kwa jinsi hasira zilivyokaba sikutaka kujua jina la Mbunge wala jimbo lake na wananchi wake anaowawakilisha.

Ifike hatua wabunge waache "ubinafsi" Miaka nenda rudi wamekua wakitumia nafasi zao kama watunga sheria..wakitunga sheria zinazowapendelea wao kwenye suala la malipo.

Leo hii mshahara wa Mbunge haukatwi kodi yeyote. Mbunge anapata posho (allowances) ya laki tatu kwa kila kikao anachoingia. Na anaweza akaja akasaini akaondoka asikae mpaka mwisho au anaweza akahudhuria na akakaa kimya mpaka kikao kikaisha.

Wabunge wengi wamekaa tu pale,wakipigwa na Viyoyozi huku wakiwa wamesinzia. Kweli mshahara wa 12 millions ambao hauna statutory deductions nyie hauwatoshi?

Kweli posho ya laki 3 kwa kila kikao haziwatoshi? Kweli posho kwenye hizi standing committees za bunge nazo haziwatoshi? Hebu muogopeni MUNGU.

Sasa ni muda sahihi wa wabunge wote wanaoona mshahara wa Million 12 hauwatoshi WAACHIE NGAZI ili Young Graduates waje kushikilia nafasi hizo za ajira.

Nyie mmekaa hapo miaka zaidi ya mitano na hakuna mabadiliko yeyote kwenye majimbo. Sasa ni wakati muhimu Vijana wahitimu washike nafasi zenu.

ONDOKENI

Hivi ni Graduate gani ataacha mshahara wa 12M? Rais Samiah alisema kwenye hotuba ya men Mosi kwamba hatopandisha mishahara sababu nchi haina hela.

Uchumi umeshuka mpaka 04%, wewe ni nani wa kuomba uongezewe zaidi. Graduates, chukueni nafasi zao hawa wanasema 12M ndogo sana.
 
Mimi ningeshauri majimbo yapungue ili hata wakiongezewa mishahara wawe wachache, angalau Jimbo liwe ni mkoa mzima, na viti maalum visiwepo, mawaziri hizo nafasi wawe wanaziomba, kk wa maana mawazizi wasiwe wabunge.

Kunanaana gani majimbo mengi hapo hapo kuna wabunge nafasi maalum?
 
'
20210608_103756.jpg
 
Hao wabunge hata wakilipwa 4m, na posho na mikopo ya magari na pensheni ya 250 M baada miakaI5 tu', bado wabunge wako vizuri zaidi ya wafanyakazi wengi muhimu zaidi kama madaktari, wahandisi, walimu nk.

Na wala usitegemee atoke mtu pale, eti mishahara hautoshi. Thubutu, vijana bado mtasubiri sana manake tatizo lingine nyie ndio mliowapigia debe kuingia mjengoni, na hizo ni kejeli zao na ubinafsi uliozidi, kwa wananchi tu. Kubalini yaishe. Kazi iendelee.
 
Inasikitisha sana kwa kweli, Luka 3:14 Nao askari wakamwuliza, “Na sisi tufanye nini?” Naye akawajibu, “Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu.” Kodi zetu wanachukua kwa nguvu na mabavu, mishahara yao haikatwi kodi 3.8m bado posho n.k kwa mwezi anauhakika wa kuingiza 11m harafu anakwambia haumtoshi mshahara [emoji54]

Eti sababu akiamka asubuhi anakuta watu wanakuja na shida zao mara misiba wanaomba msaada.

Hivi amefikiria Mama anaeuza machungwa stand kwa siku anaweza akapata kiasi gani na huyuhuyu Mama anamudu kulipa bill ya umeme, maji, anasomesha, anawanunulia watoto mahitaji na bado ikitokea mchango wa msiba au michango ya kanisa anaimudu?

Anakwambia mtangazaji angalia hotel ninayokaa hapa dodoma kwa siku nalipa bei gani !, Hivi kunaulazima gani wakulala hotel ya 5* 200k -300k per day ilihali mshahara haukutoshi wakati kuna hotel/lodge za 20,000 - 40,000 na unapata service nzuri tu.
 
Mimi ningeshauri majimbo yapungue ili hata wakiongezewa mishahara wawe wachache, angalau Jimbo liwe ni mkoa mzima, na viti maalum visiwepo, mawaziri hizo nafasi wawe wanaziomba, kk wa maana mawazizi wasiwe wabunge. Kunanaana gani majimbo mengi hapo hapo kuna wabunge nafasi maalum?
Hii ngumu sana kwenye administration kupunguza majimbo japo inawezekana.

Sababu tuna majimbo mengine makubwa ki jografia.
 
Hao wabunge hata wakilipwa 4m, na posho na mikopo ya magari na pensheni ya 250 M baada miakaI5 tu', bado wabunge wako vizuri zaidi ya wafanyakazi wengi muhimu zaidi kama madaktari, wahandisi ,walimu nk. Na wala usitegemee atoke mtu pale, eti mishahara hautoshi....thubutu, vijana bado mtasubiri sana manake tatizo lingine nyie ndio mliowapigia debe kuingia mjengoni, na hizo ni kejeli zao na ubinafsi uliozidi,kwa wananchi tu. Kubalini yaishe... kazi iendelee.
Ubinafsi umezidi .

Hapo nimekuelewa.

Lakini hii keki ya taifa iliwe kwa staha.

Sio kila mtu akijisikia kuongeza kijiko kingine au mkono mwingine wa ziada basi afanye hivyo .

Vijana kuwasaidia hawa wazee ilikua lazima tu iwe hivyo,maana vijana walikua wanapata visenti vya kubadilishia mboga kwenye kuwasaidia wale wazee waukwae ubunge .

Hawakua na option.
 
Punguza kwanza viti Maalum vyote na Majimbo yawe ni machache yawe 74
 
Hawa Wabunge wengepewa Toyota Corrola na la pili unapewa mwaka mmoja kama hudilivery katika jimbo lako unafukuzwa kutokana na ahadi ulizotoa nafikiri jeuri ingewatoka wanatakiwa watiwe pressure ya hali ya juu .Unajua kwenye Bunge kuna pesa ndio maana kila mtu anapigania kuwa mbunge plus hakuna kazi yyote ni sehemu ya starehe na kuparty tu .
 
Badala ya kuongezwa mishahara inapaswa kupunguzwa na kukatwa kodi ili miradi mikubwa itimie kwa wakati, na hiyo itakuwa ni mbadala wa kwenda kukopa nje huko
 
Hii ngumu sana kwenye administration kupunguza majimbo japo inawezekana.

Sababu tuna majimbo mengine makubwa ki jografia.
Kuna wakuu wa wilaya na madiwani wahusike kuchakata michakato jurahisisha shunguli za mbunge, kila mkoa awepo mbunge mmoja, kusiwe na wabunge wa viti maalum, kusiwe na wateuliwa, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na mawaziri hizo nafasi ziwe wanaziomba kitaaluma. Wawe waajiriwa, wasiwe na upande wowote kisiasa. Wabunge pia wasaidiwe na makatibu wakuu wa mikoa na wilaya kwenye vyama vyao. Itawezekana kabisa.
 
Hili likatiba bovu la ccm ndio linafanya hawa wazee wawepo bungeni kina zungu wamechoka na kuchakaa mawazo yao ni pesa tuu bajeti mbovu inapita wao wan at a bora liende tuu
 
Back
Top Bottom