Uchaguzi 2020 Wabunge wa CCM na waliohamia CCM, walioangushwa kura za maoni 2020

Sikio la kufa halisikii dawa
 
Duh! Hadi Maige naye kala za uso, kweli Middle Income inakuja na mengi.

Ila jirani yake Seleman Zedi wa Bukene kapenyaje?

Ombi kwa Kamati kuu imfyeke kwa ustawi wa wana Bukene.
 
Yule jangili mkoani Shinyanga inaonekana amepita-huu ndiyo mtihani kwa CCM, ni matumaini yangu huko Dodoma ataangukia pua, vinginevyo CCM sitawaelewa.
 
William Mganga Ngeleja (35) pamoja na tambo za shekeli zake,bado kwa wajumbe wanaojitambua haikuwa sababu ya kutompa adhabu aliostahili ndani ya ukumbi wa COTC.kujinadi kwake ilikuwa kama kuendesha baiskeli ziwani.
 
Sijamuona mbunge wa Nkasi Kusini nasikia naye kaangukia pua. Hebu fuatilia mkuu.
Kweli bwana Mipata wamekula kichwa bila kumsahau mbunge wa kwela aliyemrithi mzindakaya anaitwa Malocha nae wamekula kichwa
 
Mboni mhita ni handeni vijijini,
Handeni mjini omary kigoda, naona naye kaangukia pua.
 
Baadhi watarudishwa kwenye ubunge na Magufuli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…